kakuruvi
JF-Expert Member
- Sep 2, 2009
- 770
- 256
Katika mambo mengi yanayozuia wachumba au marafiki wengi kutofikia adhma ya kufunga ndoa mojawapo ni DINI. Kuna wakati wapendanao wenyewe wanafikia kikomo kwa sababu ya dini au wakati mwingine wao wako radhi ila wakileta suala la ndoa kwa wazazi au walezi wanapigwa stop.
Jana nilikuwa nasikiliza RFA usiku kuna kipindi cha nyimbo za zamani kila saa nne usiku alhamisi wimbo ulionivutia na kunikumbusha mbali ni ''Wazazi wake Jane - Msondo Ngoma''
wazazi wake Jane,
hawakupenda Jane aolewe nami na kipingamizi kwetu ni dini na kwamba sina pesa za kumtunza.
Jane alipowaelewa,
alijaribu kuwabembeleza na kwamba jambo la muhimu ni maelewano na hata hivyo hawakukubali.
CHORUS:
nilipokutana na Jane nilimshauri akubaliane na mawzo ya wazazi wake,
ni wao walikulea wakakupeleka shule wakakupa matunzo ya kila aina kipenzi...............
Narudi kwenu wana JF, Jambo kama hili lina suluhisho kweli? umewahi kukutwa na jambo kama hili? Nawatakia mwisho wa wiki mwema.
Jana nilikuwa nasikiliza RFA usiku kuna kipindi cha nyimbo za zamani kila saa nne usiku alhamisi wimbo ulionivutia na kunikumbusha mbali ni ''Wazazi wake Jane - Msondo Ngoma''
wazazi wake Jane,
hawakupenda Jane aolewe nami na kipingamizi kwetu ni dini na kwamba sina pesa za kumtunza.
Jane alipowaelewa,
alijaribu kuwabembeleza na kwamba jambo la muhimu ni maelewano na hata hivyo hawakukubali.
CHORUS:
nilipokutana na Jane nilimshauri akubaliane na mawzo ya wazazi wake,
ni wao walikulea wakakupeleka shule wakakupa matunzo ya kila aina kipenzi...............
Narudi kwenu wana JF, Jambo kama hili lina suluhisho kweli? umewahi kukutwa na jambo kama hili? Nawatakia mwisho wa wiki mwema.