Revolution strategy: Kutoka kuchagua viongozi wa wanyonge hadi kumaliza unyonge wenyewe

Mkuu umeibua hoja za msingi. Labda tukuulize wewe ushauri wako ni nini sasa? Je! unakubali kuna tatizo la ukosefu wa ajira na linaongeka? unakubali kuwa mfumo wa elimu hauwezeshi vijana kujiajiri na kuingiza elimu hiyo kwenye matendo labda waajiriwe na nafasi za kuajiriwa ni chache sana? unakubaliana kuwa wanaotakiwa wajiajiri hawana mtaji na hawawezi kupata mtaji mpaka pawe na 'external force'? tunafanyaje sasa? Unaamini maono ya kisiasa yanayotoa muelekeo wa kisera yanaweza kusaidia kitu?

Umetoa mfano wa udaktari na urubani. Kuna aina ya fani ni lazima kusoma darasani. kwa watakaochagua fani husuka watasoma darasani lakini kwa kuspecialize kutokea mapema kabisa kwa mfano udaktari. Lakini ushangae sasa, huo udaktari wenyewe mfano kwenye korona tumerudi kwenye tiba asili na zimesaidia kwa kiasi flani. Waliozibuni walisoma kwa utaratibu gani? Urubani kwa mfano uliousema, hivi unajua urubani ni kama udereva? unahitaji zaidi 'skills' na sio 'academics' yaani la saba anaweza kuwa dereva mzuri kuliko PhD holder?

Mwisho wa siku, ili tuweze kufanikiwa kama taifa, tunatakiwa kujifunza kufanya vitu vyetu sisi kama sisi na sio kuiga wengine. Hakuna namna tunaweza kufanikiwa kwa kufuata mkumbo, tujifunze kwa wengine lakini tufanye kivyetu na kwa ubunifu wetu wenyewe.
Kwanza kabisa mfumo wa awamu ya Kwanza wa kuwa na vyuo vya Ufundi na kilimo ndio tuufuate, elimu ya msingi iimarishwe kwa kuwa na waaalimu bora sio waalimu wa upe, jingine na kuna baadhi ya mitaala iimarishwe zaidi kuwa na practical zaidi kuliko theory, na tatizo jingine ni ya na la rushwa na kifamilia ambalo huwafanya vijana kutokujitambua,
Na kufikiria misheni town ndio uvumbuzi wa Maisha na mahali pa familia ndio halali yake , matokeo yake Mzee wa miaka 60-70 bado analisha vijana wake badala ya wao kuwa wanamsaidia yeye au kumpisha Mzee apangishe baadhi ya vyumba walivyokuwa wanakaa walipokuwa wadogo.
Katika hali kama hii vijana kama hao kuwakopesha inakuwa ngumu , ingawa inaweza kuwa kikwazo kwa wanaojitambua kutoka na kujiajiri.
Ingawa hilo lina kuwa addressed kwa kuwaaambia vijana kujiunga ktk vikundi, kutumika kwa vitambulisho cha taifa kuweka taarifa za mtu n.a. ufuatiliaji.
Kwa ufupi rushwa na upendeleo ndio zilizoharibu maono ya wazazi na vijana kuhusu Maisha binafsi na maendeleo
 
Tuondokane na CCM sasa imekuwa aibu kuwa na chama madarakani kwa miaka 60.
Wameshindwa kututoa kwenye umaskini,ujinga na maradhi,huku bado wanang'ang'ania madaraka.Hawana mawazo mapya wa dhamira ya kweli ya kuondoa kero za wananchi,wanafanya yale yanayowakabili Watanzania.
 
Malawi wamepiga hatua kubwa na kuna uhuru na demokrasia sana kuliko Tanzania, haya ni maendeleo. Malawi siku hizi wana production kubwa ya sukari kumbuka tumenunua sukari kutoka kwao pamoja na udogo wa nchi yao kulinganisha na ya kwetu. Kumbuka Malawi wana population density kubwa kuliko sisi. Zambia, nenda kaone wana mipango mizuri zaidi kuliko sisi iwe mipango miji, matumizi ya ardhi n.k.

China wanamaendeleo ndio lakini kumbuka China ni nchi ya dunia ya tatu sio first world. Pia jua kwamba China kwasababu ya utawala wa chama cha kikomunist kuna uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu. Mambo mengi yanayotendekea China hayatangazwi; watu wananyongwa bila vigezo vya kutosha, kuna ukandamizaji mkubwa sana wa wanyonge, watu wana uawa kama kuku, kumbuka wakati corona ilianza kama uliona ile video ungedodosha machozi jinsi watu waliambukizwa walivyokuwa wakikamatwa na kupelekwa kwenye chumba cha kuuwawa, kisa wana corona. Kuna uovu mwingi mno unaotokea China. Ndani ya china kuna mamia ya mamilioni maskini wa kutupa usione majengo makubwa na miji mizuri ukafikiri basi kila mtu anaishi hivyo China. Wachina wengi wamekimbia China na wanaishi kila mahali duniani, hii sio dadili nzuri, wengi ni wakimbizi wa umaskini na ubabe wa kikomunist huko China.

Russia ilikuwa vizuri miaka ya 80, na ilikuwa superpower wakati demokrasia ikitawala Russia, watu wengi walikwenda kusoma Russia lakini sana wamekuwa authoritarian, chama kimoja cha Putin na huwezia amini Russia imeangukia kwenye ukabila na tena vita ya koo, na imerudi kuwa dunia ya pili. Demokrasia ni muhimu sana na ndio tatizo la nchi za Afrika.
Demokrasia haiongezi uzalishaji, bali mfumo wa uchumi na usimamizi.
Capitalism by nature inasimamia na kuenzi tija, wakati socialism inaenzi social life , kwanza inakosa kumpa mtu utashi wa kufikia malengo labda kwa kupitia brutality
 
Demokrasia haiongezi uzalishaji, bali mfumo wa uchumi na usimamizi.
Capitalism by nature inasimamia na kuenzi tija, wakati socialism inaenzi social life , kwanza inakosa kumpa mtu utashi wa kufikia malengo labda kwa kupitia brutality
Huwezi kuwa na mfumo mzuri wa uchumi bila uhuru na demokrasia. Demokrasia huzalisha uongozi mzuri, na uongozi mzuri huzalisha mipango mizuri, uhuru na mipango mizuri hupelekea uchumi mzuri.
 
Mkuu denooJ umeongea jambo la msingi sana. Lakini pia wanaosema kilimo hawasemi watu wote wakalime. Hakuna sekta inayoweza kusimama peke yake, kwa hiyo uko sahihi kabisa. Suala ni kwa namna gani tunaweza kuwa na viwanda vingi zaidi? hapo ndio tunazungumzia ubunifu. Tunakuwaje na ubunifu? hapo ndio tunazungumzia mfumo wa elimu? tunaboreshaje mfumo wa elimu? hapo ndio tunazungumzia sera na mfumo wa elimu.

lakini vipi viwanda bila mtaji? hapo ndio tunajaribu kufikiri ni vipi vijana wanaweza kupata mikopo ambayo ni productive. Kwa hiyo unachosema ni kweli kwamba kuna vitu vingi vinategemeana.
Hapa ndio utatambua kumbe elimu ya darasani (theory) na ya vitendo (practical) zote zinatakiwa kupewa kipaumbele kwa wakati mmoja. Kwenye viwanda watu kama wahasibu, na managers watatakiwa kusimamia hivyo viwanda effectivelly, lakini pia upande wa kilimo lazima pawepp na mabwana shamba ( japo watakuwa wamepatia elimu yao darasani) lakini pia watatakiwa kwenda field kutoa elimu kwa wakulima namna gani wafanye ili waweze kupata mazao kwa wingi na yenye ubora.

Hapa pia, sekta ya miundo mbinu ina umuhimu wake mkubwa sana, barabara nyingi hasa wakati wa masika huwa hazipitiki hivyo kuchelewesha mazao kufika sokoni kwa wakati, hili husababisha kupunguza ubora wa mazao na hivyo kushusha thamani yake hivyo kilimo kutomsaidia mkulima aliyekusudiwa.

Hapa kwa kifupi ni kwamba, serikali lazima ifikirie namna bora ya kutawanya rasilimali ilizonazo ili kuweza kukabiliana na tatizo la ajira, kwasababu sekta nyingi zinategemeana ili kufikia lengo.

Hivyo serikali wakifikiria kuzalisha wakulima kwa kuwapa elimu na mitaji, lazima pia waangalie sekta ya miundombinu ili kuwezesha mazao kufika viwandani na masokoni kwa wakati, na pia wakati huo huo wawe wameshajenga au kufufua viwanda kwa asilimia kubwa, hapa ndio tutaweza kukabiliana na tatizo la ajira kwa vitendo.

Kuwapa vijana mikopo unayoiita productive hakuwezi kusaidia kama hizo changamoto nilizozitaja hapo juu hazitafanyiwa kazi mapema, kilichopo sasa, utawapa vijana mikopo lakini mwisho wa siku watakwama wasijue pa kupeleka mazao yao kutokana na hizo changamoto nilizoorodhesha juu.
 
Huwezi kuwa na mfumo mzuri wa uchumi bila uhuru na demokrasia. Demokrasia huzalisha uongozi mzuri, na uongozi mzuri huzalisha mipango mizuri, uhuru na mipango mizuri hupelekea uchumi mzuri.
South Africa walivyo endelea kabla ya Mandela, ilikuwa ni sababu ya demokrasiaaaa, you ought to be day dreaming instead of dreaming at night.
Or u don't even the meaning of economics , ndio maana unafikiria kila kitu ni demokrasia , iwe kutafuta mchumba demokrasia n.k
 
South Africa walivyo endelea kabla ya Mandela, ilikuwa ni sababu ya demokrasiaaaa, you ought to be day dreaming instead of dreaming at night.
Or u don't even the meaning of economics , ndio maana unafikiria kila kitu ni demokrasia , iwe kutafuta mchumba demokrasia n.k
Nafikiri hujui unaongea nini. Afrika ya Kusini walikuwa na demokrasia tangu miaka ya 1800 kati ya wazungu. Kwa weusi ambao hawakuhesabiwa kuwa watu kamili ilionekana kuwa hakuna haja ya kuwapa demokrasia. Ndio maana watu weusi waliteseka na kubaki kwenye umaskini mkubwa. Baada ya demokrasia kuingizwa kwa watu wote leo SA watu weusi nao wanaheshimika na wameanza kumiliki uchumi mkubwa pia.
 
South Africa walivyo endelea kabla ya Mandela, ilikuwa ni sababu ya demokrasiaaaa, you ought to be day dreaming instead of dreaming at night.
Or u don't even the meaning of economics , ndio maana unafikiria kila kitu ni demokrasia , iwe kutafuta mchumba demokrasia n.k
Huyo bwana kuna namna anachanganya vitu. Anachomeka demokrasia isipohusika
 
Nafikiri hujui unaongea nini. Afrika ya Kusini walikuwa na demokrasia tangu miaka ya 1800 kati ya wazungu. Kwa weusi ambao hawakuhesabiwa kuwa watu kamili ilionekana kuwa hakuna haja ya kuwapa demokrasia. Ndio maana watu weusi waliteseka na kubaki kwenye umaskini mkubwa. Baada ya demokrasia kuingizwa kwa watu wote leo SA watu weusi nao wanaheshimika na wameanza kumiliki uchumi mkubwa pia.
Mkuu hakuna uhusiano kati ya demokrasia na maendeleo ya kiuchumi. Unachanganya hayo mambo. Yaani ni sawa na chai na mkate kila kimoja kina mahali pake lakini kuongezeka kwa kimoja hakupelekei kuongezeka kwa kingine
 
Mkuu hakuna uhusiano kati ya demokrasia na maendeleo ya kiuchumi. Unachanganya hayo mambo. Yaani ni sawa na chai na mkate kila kimoja kina mahali pake lakini kuongezeka kwa kimoja hakupelekei kuongezeka kwa kingine
Wewe hujui kwamba ustaarabu wote Ulaya unatokana na demokrasia? Au unataka kurudishwa kwenye utumwa ufanye kazi kwa ajili ya makabaila na wala usipewe haki na uhuru wa kuzungumza? Acha ujinga ndugu demokrasia ni muhimu sana. Nashangaa mnafurahia jiwe kuwa dikteta! Ujinga mkubwa huu.
 
Nafikiri hujui unaongea nini. Afrika ya Kusini walikuwa na demokrasia tangu miaka ya 1800 kati ya wazungu. Kwa weusi ambao hawakuhesabiwa kuwa watu kamili ilionekana kuwa hakuna haja ya kuwapa demokrasia. Ndio maana watu weusi waliteseka na kubaki kwenye umaskini mkubwa. Baada ya demokrasia kuingizwa kwa watu wote leo SA watu weusi nao wanaheshimika na wameanza kumiliki uchumi mkubwa pia.
Inabidi nikuache na kukusikitia
 
Watu wanafikiri China imeendelea sana, ni nchi ya dunia ya tatu hadi ya pili. Maendeleo ni kwa watu wachache tu hasa mijini. Ni kama mtu aje Dar alafu afikiri Tanzania nzima ndio hivyo. Ndio maana wachina wanatorokea nchi nyingine kutafuta maisha.
 
Watu wanafikiri China imeendelea sana, ni nchi ya dunia ya tatu hadi ya pili. Maendeleo ni kwa watu wachache tu hasa mijini. Ni kama mtu aje Dar alafu afikiri Tanzania nzima ndio hivyo. Ndio maana wachina wanatorokea nchi nyingine kutafuta maisha.
Exposure yako ipo mufilisi au hujui nini mana ya maendeleo , na ingredients za maendeleo
 
Exposure yako ipo mufilisi au hujui nini mana ya maendeleo , na ingredients za maendeleo
Wewe na ccm mnafikiri maendeleo ni maghorofa na treni za umeme na ndege na madaraja ilhali watu wakikosa maji, nyumba, nk. Leta maana yako ya maendeleo na ingredients zake tuone.
 
Watu wanafikiri China imeendelea sana, ni nchi ya dunia ya tatu hadi ya pili. Maendeleo ni kwa watu wachache tu hasa mijini. Ni kama mtu aje Dar alafu afikiri Tanzania nzima ndio hivyo. Ndio maana wachina wanatorokea nchi nyingine kutafuta maisha.
Ni nchi gani ambayo watu wake wote ni matajiri? Na nchi hiyo iko hivyo kwa sabahu ya demokrasia?
 
Ni nchi gani ambayo watu wake wote ni matajiri? Na nchi hiyo iko hivyo kwa sabahu ya demokrasia?
Hakuna nchi ambayo watu wake wote ni matajiri. Marekani, Canada, Australia, nchi nyingi za Ulaya zina watu wengi walio na hali nzuri kiuchumi na kitu kimoja common kwenye nchi hizi ni uhuru na demokrasia.
 
Wewe na ccm mnafikiri maendeleo ni maghorofa na treni za umeme na ndege na madaraja ilhali watu wakikosa maji, nyumba, nk. Leta maana yako ya maendeleo na ingredients zake tuone.
Sasa wewe umeweka vizuri concept yako ya nyumba na maji , lakini hujafikiria source of income ya ku finance hivyo vitu viwe sunstainable , ndio maana nakwambia
Maendeleo na uchumi na ingredients zake sasa wewe ukifikiria nyumba inakuja kama uyoga sawa endelea na hizo
 
Hapa kama kuna kitu ambacho nakiona kigumu kueleweka kwa wengine.

Siasa + Demokrasia = Maendeleo.

Siasa - Kwa kifupi hii inaunganisha ideology ya watu, kuwa na utaratibu na mfumo unaofanana ukiongozwa na kanuni na sheria walizojiwekea ili kufikia lengo walilokusudia, kama ni chama cha siasa basi lengo hilo inakuwa ni kushika dola, au kama tayari kina dola basi kupeleka maendeleo kwa wananchi wake.

Demokrasia - Huu ni uhuru wa kutoa maoni waliojiwekea watu ndani ya siasa, haya maoni hutofautiana lakini mara zote huongozwa na kanuni ya wengi wape, wachache wasikilizwe.

Maendeleo - Haya huja baada ya kufuata hiyo mifumo miwili niliyoizungumzia hapo juu, kwa mfano;

Kama chama cha siasa kinachounda serikali wakiamua kutengeneza ilani yao kuelekea uchaguzi, mfano, tukishinda uchaguzi tutajenga reli SGR, tutajenga Stiglers Gorge, na tutanunua ndege zetu, hili wazo huja mwanzo kabisa kwenye process ya kwanza niliyoizungumzia (Siasa) hiki kikundi cha watu baada ya kukutana wanatengeneza mawazo yao ili kuwapelekea wananchi wao maendeleo.

Stage ya pili ya demokrasia ndio itakayoamua, je, hilo wazo la kujenga stiglers litekelezwe au liachwe, hapa ndipo mawazo ya wengi yatafuatwa na mawazo ya wachache yatasikilizwa, hii ni ndani ya chama cha siasa kinachounda serikali, au kama sio chama basi ni kutoka ndani ya serikali yenyewe mfano wenu wa China. Kama wengi wakiona kuna umuhimu wa kujenga hivyo vitu hapo juu ili kuwahudumia wananchi wao, then mawazo hayo ya ujenzi yatasikilizwa na kupitishwa, hii ndio maana ya demokrasia inayoleta maendeleo ambapo wengi hapa mnaonekana mmeshindwa kupaelewa.

Stage ya tatu ndio maendeleo yenyewe; hii inatokana na kutimizwa kwa stage ya pili hapo juu, yaani baada ya wengi kuamua kwa umoja wao nini wafanye kuwapelekea wananchi wao maendeleo, ndio mawazo kama kukuza sekta ya kilimo yanatokea, na wanaweka njia zipi wazipitie ili kuweza kufanikisha hilo lengo ili kuondokana na matatizo mfano la ukosefu wa ajira.

Kwa kifupi kwa mtazamo wangu kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya demokrasia na maendeleo, kwani watu wakitofautiana mawazo kwenye decision making ni vigumu sana kuyafikia maendeleo, lazima mawazo ya maendeleo yapate uungwaji mkono wa wengi (demokrasia) ili yatekelezeke kirahisi.
 
Back
Top Bottom