Peter Msigwa
Kwa HESHIMA zote, napinga mtazamo wa prof. Issa Shivaji, kuwa eti, uzalendo ni kuitii serikali iliyokomadarani. Na utaifa eti ni ukereketwa wa nchi yako hata Kama huipendi serikali. Kwa mtazamo huu, Nyerere hakuwa mzalendo kwa kuwa aliipinga serikali ya mkoloni? Vipi Mandela aliyepinga serikali ya kibaguzi kule bondeni naye hakuwa mzalendo? Vipi waganda walioipinga serikali ya Idd Amini? Vipi serikali Kama ya Mabutu wa DRC?
Kuna wakati kuichukia serikali serikali iliyopo madarakani ni uzalendo, serikali huja na kuondoka, ila taifa hubaki, serikali yoyote ambayo, inatumia vibaya raslimali za nchi yake, ikichukiwa ni uzalendo. Serikali ya kifisadi, inayoendekeza ujangili, wizi na uporaji wa Mali za umaa inafaa kuchukiwa kwa nguvu zote na huo ndio uzalendo.
Serikali inayokiuka haki za binadamu, inayokandamiza demokrasia, kuitii serikali Kama hiyo sio uzalendo. Ndugu Issa Shivji... Sijakuelewa hasa msomi Kama wewe. ..how would you say that? saw you on news yesterday (ITV).
Kwa HESHIMA zote, napinga mtazamo wa prof. Issa Shivaji, kuwa eti, uzalendo ni kuitii serikali iliyokomadarani. Na utaifa eti ni ukereketwa wa nchi yako hata Kama huipendi serikali. Kwa mtazamo huu, Nyerere hakuwa mzalendo kwa kuwa aliipinga serikali ya mkoloni? Vipi Mandela aliyepinga serikali ya kibaguzi kule bondeni naye hakuwa mzalendo? Vipi waganda walioipinga serikali ya Idd Amini? Vipi serikali Kama ya Mabutu wa DRC?
Kuna wakati kuichukia serikali serikali iliyopo madarakani ni uzalendo, serikali huja na kuondoka, ila taifa hubaki, serikali yoyote ambayo, inatumia vibaya raslimali za nchi yake, ikichukiwa ni uzalendo. Serikali ya kifisadi, inayoendekeza ujangili, wizi na uporaji wa Mali za umaa inafaa kuchukiwa kwa nguvu zote na huo ndio uzalendo.
Serikali inayokiuka haki za binadamu, inayokandamiza demokrasia, kuitii serikali Kama hiyo sio uzalendo. Ndugu Issa Shivji... Sijakuelewa hasa msomi Kama wewe. ..how would you say that? saw you on news yesterday (ITV).