Rev. Msigwa dhidi ya Prof. Shivji

Rev. Msigwa dhidi ya Prof. Shivji

Kinachoimaiza hii nchi ni unafiki na kuwaogopa watu kiasi cha kushindwa kuwashauri wanapokosea kwa sababu wanawadhifa fulan au tuna maslahi nao.
Kama Pro. kakosea naye anakosolewa kwa sababu si kwamba alikuwa anaongelea ndani ya fani yake ya sheria. \
Tuache ujinga wa kuogopa majina ya watu.
Kama baba yako ni mlevi anampiga mama yako kila siku bila sababu utanyamaza kwa sababu yeye ni baba?
INAUMIZA KWA SABABU HAYA YANASHABIKIWA NA VIJANA AMBAO WATAENDELEA KUWEPO MIAKA MINGI IJAYO,NI HERI WANGEKUWA WAZEE AMBAO TUNAJUA KIZAZI CHAO KITAKWISHA.
NAOMBA TUAMKE SI KUSHABIKIA NA KUONA NI SAHIHI KWA KILA JAMBO LINALOSEMWA NA MTU KWA SABABU YA JINA AU WADHIFA WAKE.

KWELI MKUU Kijana kushabikia UJINGA NI HATARI SANA, huyu SHIVJI tangu ayakana maandiko yake nilimfuta kabisa TZ wachumia tumbo ni wengi na hasa hawa wasomi wetu BURE KABISA
 
Wosomi tuliowategemea watatukomboa kwenye majanga haya... Ndo wamekuwa wa kwanza kujaza matumbo yao kupitia kodi za walala hoi..
 
Peter Msigwa

Kwa HESHIMA zote, napinga mtazamo wa prof. Issa Shivaji, kuwa eti, uzalendo ni kuitii serikali iliyokomadarani. Na utaifa eti ni ukereketwa wa nchi yako hata Kama huipendi serikali. Kwa mtazamo huu, Nyerere hakuwa mzalendo kwa kuwa aliipinga serikali ya mkoloni? Vipi Mandela aliyepinga serikali ya kibaguzi kule bondeni naye hakuwa mzalendo? Vipi waganda walioipinga serikali ya Idd Amini? Vipi serikali Kama ya Mabutu wa DRC?

Kuna wakati kuichukia serikali serikali iliyopo madarakani ni uzalendo, serikali huja na kuondoka, ila taifa hubaki, serikali yoyote ambayo, inatumia vibaya raslimali za nchi yake, ikichukiwa ni uzalendo. Serikali ya kifisadi, inayoendekeza ujangili, wizi na uporaji wa Mali za umaa inafaa kuchukiwa kwa nguvu zote na huo ndio uzalendo.

Serikali inayokiuka haki za binadamu, inayokandamiza demokrasia, kuitii serikali Kama hiyo sio uzalendo. Ndugu Issa Shivji... Sijakuelewa hasa msomi Kama wewe. ..how would you say that? saw you on news yesterday (ITV).

Hata mimi nilishangaa pia kwa maana iliyotolewa kwa shule yangu ndogo. Naomba kusahihishwa kama uzalendo hauna maana ya PATRIOTISM ambayo iko ndani ya UTAIFA ikiwa na maana ya MOYO WA MWANANCHI KUIPENDA NCHI YAKE AU TAIFA LAKE na kuwa tayari hata kuifia nchi yake. Kwa maana hiyo a patriotic man hawezi kuwa fisadi, hawezi kuona rasilimali za nchi zinachukuliwa na wageni kwenda kuendeleza nchi zao nk.
 
Wana JF hebu nisikizeni kwa makini sana!

Huo Uprofesa wa Shivji ulikuwa huko nyuma yaani majuzi ile, mtondogoo na jana. Kwani Shivji wa leo kwa kifupi ni
'Profedha' na sio Professa.

Shivji wa leo hana tofauti na p*o*njolo mwingine yeyote mfanya biashara anyehujumu uchumi kwa kukosa uzalendo au kwa kuweka 'faida kwanza'. Mwisho wa siku lengo kuu ni kufunga biashara na kuhesabu faida tu.

Shivji wa leo ameamua kulivua na kuliweka pembeni 'koti la uzalendo'. Shivji ameamua kutokufa katika lindi la umasikini kwa kisingizio cha uzalendo ati kwa kutegemea ile pesheni ya UDSM na mapato ya kuuza vitabu na majarida tu. Shivji amegundua hiyo hailipi na sasa ameona fursa ya kumtumikia fisadi mtawala ili awini 'jakipoti' la chapu chapu. Hivyo ameamua kuweka usomi na vyeti pembeni afanye dili la chapu chapu kwanza🙂

Shivji ameamua kuwa... kama 'mbwai ni mbwai bwana' au 'isiwe taabu' au 'Liwalo na liwe" style kuwa wacha nae ale keki moja na mafisadi watawala vinginevyo anaona atafia kwenye lindi la umasikini.
Kuna kila dalili kuwa yuko kwenye hatua za mwisho mwisho za kukusanya chenji yake ya
mwisho mwisho. Kwa Shivji hii ni 'takrima' na kwetu Watanzania ni malipo ya usaliti. Kwa kifupi malipo ya usaliti huu ni sawa na malipo ya 'kima cha damu ya mtu".

Kitakachofatia ni yeye kuishia kwenda kumalizia ngwe ya maisha yake ughaibuni (UK au Canada) na huku nyuma WaTanzania wakianza kuchinjana ile "Ntarahamwe' staili, Nayote hayo ikiwa ni matokeo ya kazi yake na wenzake walioamua kuuweka uzalendo pembeni.

Na hili si uzushi mtasikia tu, jamaa ameishia. You stay tuned!
 
Nimegundua kuna kusoma na kuelimika
 
.... Kumbe Unaweza Kusoma Lakini Usielimike.! Huyu Prof Arudi Shule
 
Shivji ni mhindi tu arudi kwao india.hivi watanzania wanaruhusiwa kujadili au kutoa maoni kuhusu katiba ya india?
 
Mbangaizaji Msigwa uwezo wa kuelewa na kutafsiri mantiki ya alichokisema Prof Shifji. Ni wa kumpuuza tu kama wapuuzi wengine. Na hajui kuwa anachokisema kina maana gani katika Sheria za Uhaini.
Damn you and damn you again!! afadhali kuwa mhaini kwa serikali ya majambazi kuliko mnafiki kama huyu prof.
Tunafahamu tabia za huyu!! huyu ndiye aliyekuwa anawabebea ZNZ kapu la madaraka kamili kwenye midahalo sasa anachumia tumbo kwa mikate ya majangili!!
 
Prof. shivji..mnafki tu akifikiria na uraia wake lazima akubali unafki na uzandiki....
 
Katiba na dhana ya kigeugeu cha Shivji kimeporomosha sifa yake kabisa. Anaonekana mtu mwepesi katika macho ya wenye kupenda nchi yao. NINA SHAKA NA UTANZANIA WAKE!
 
Prof shivji si yule tumjuaye....trust me!!

sijajua nini kimempata?
 
Iko siku watanzania watamkumbuka na kumlilia Professor Shivji. Katika Maprofessa ninaowaheshimu nchini na kuwakubali katika taaluma zao ni huyu jamaa pamoja na rafiki yake Professa Haroub Othman (marehemu). Ila kwakuwa watanzania sisi wengi wetu tunasukumwa na mihemko ya kisiasa mnamtukana na kumdhalilisha sasa!!!
 
Mbona mnataka kumvunjia heshima Prof. Shivji kumfananisha na Msigwa.

Shivji ana heshima gani katika nchi hii? kwa hiyo maana ya uzalendo aliyoizungumzia huyo prof. kilaza mchumia tumbo kupitia CCM ndio unaona yupo sahihi huyo Shivj anajikomba kwa CCM ili kulinda uraia wake na si vinginevyo na kwangu mimi ninaulinganisha Uprof. wake na ule wa Maji Marefu kwani hauna tija kwa taifa unamsaidia yeye tu kushibisha tumbo lake.
 
Back
Top Bottom