Rest in peace comrade Chacha Wangwe

Rest in peace comrade Chacha Wangwe

Joined
Jul 6, 2014
Posts
5
Reaction score
6
KUMBUKUMBU YA HAYATI CHACHA WANGWE

Ni miaka sita(6) sasa tangu alipotutoka aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Tarime,Diwani wa kata ya Tarime Mjini, Waziri kivuli wa Maji, Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mara na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Baba yetu mpendwa Hayati Chacha Zakayo Wangwe kwa kifo kilichogubikwa na sintofahamu mpaka leo,kilichotokea mnamo tarehe 28/07/2008 maeneo ya Pandambili,wilayani Kongwa.

Kwa niaba ya Familia ya Wangwe, wananchi wa Tarime na wanachama wa CHADEMA napenda kusema kuwa tanakumbuka sana uwepo wako Comrade Wangwe,na tutakukumbuka na kukuenzi daima..Mbele yako,nyuma yako.

REST IN PEACE TATA.
M B O R A K E (KUTAKUCHA)
 
Alale kwa amani naomba kumbukumbu ya kifo chake isihusishwe na mambo mengine ya ajabu ajabu
 
Apumzike kwa amani! Lakini vibaka wa buku 7 watapata mtaji wa kisiasa sasa hivi...

Tuliwapuuza tumewapuuza na tutaendelea kuwapuuza kinyago ulichokichonga kamwe hakiwezi kukutisha
 
Punzika kwa amani kamanda wetu sisi bado tunaendelea na mapambano dhidi ya interahamwe hawa
 
KUMBUKUMBU YA HAYATI
CHACHA WANGWE

Ni miaka sita(6) sasa tangu alipotutoka
aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Tarime,Diwani
wa kata ya Tarime Mjini, Waziri kivuli wa
Maji, Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Mara
na Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa,
Baba yetu mpendwa Hayati Chacha Zakayo
Wangwe kwa kifo kilichogubikwa na
sintofahamu mpaka leo,kilichotokea mnamo
tarehe 28/07/2014 maeneo ya
Pandambili,wilayani Kongwa.

Kwa niaba ya Familia ya Wangwe, wananchi
wa Tarime na wanachama wa Chadema
napenda kusema kuwa tanakumbuka sana
uwepo wako Comrade Wangwe,na
tutakukumbuka na kukuenzi daima..Mbele
yako,nyuma yako..REST IN PEACE TATA.

M B O R A K E (KUTAKUCHA)
Nimepata mashaka na nia yako kwa uzi huu. Hiyo tarehe ambayo nimeibold kweli ndio tarehe husika? Kama umeleta mada yako kwa hila ona wewe muhusika unavyoanza kujichanganya katika kitu muhimu kama hicho. BTW ni kweli kuwa wewe ni mmoja wa waratibu wa ACT?
 
Ni matumaini yangu kule aliko ndugu yetu Chacha Wangwe anapumzika kwa amani huku akiangalia jinsi Sheria ya Karma inayosema ''Whatsoever a man soweth, that shall he also reap''. inavyowatafuna viongozi na wanachama wa CHADEMA kwa sasa kama ilivyofanyika pia hivi karibuni kwa Zitto, Dr. Kitila, Samson Mwigamba na wengine wengi.

Kila tunapokutana na jina lako, hutufanya vile vile kuzilejea kumbukumbu za andiko lako linalosema ''JARIDA LA CHACHA ZAKAYO WANGWE MBUNGE WA TARIME'' ambalo linapatikana hapa,

Chacha Wangwe aibuka toka kuzimu | Tarishi Hauwawi

Katika Jarida hili, kuna kipande cha paragraph ambacho tulikichunguza na kugundua ndiyo kitovu cha mwanzo wa sheria ya Karma kwa baadhi ya viongozi na wanachama wa CHADEMA ambapo umesema,
Ofisi ya Katibu Mkuu (Ofisi ya Slaa) ndiyo ya kwanza kunituhumu kuwa nawaingilia majukumu yao katika suala zima la matumizi mabovu ya fedha za ruzuku ya chama. Chama hupata zaidi ya milioni 60 kila mwezi. Ni fedha nyingi sana kukijenga chama kama zikipata mipango mizuri na kuachana na matumizi mabovu kama matumizi ya helkopta kwenye kampeni kama ilivyotokea kwenye chaguzi zetu pamoja na baadhiya viongozi kudai kuwa wanajilipa madeni waliokikopesha chama wakati wa kampeni za 2005.

Mhe. Philemon Ndesamburo Mbunge wa Moshi Mjini inadaiwa kuwa anakidai chama milioni 100 alizokopesha wakati wa kampeni za 2005.

Mhe. Philemon Ndesamburo Mbunge wa Moshi Mjini inadaiwa kuwa anakidai chama milioni 100 alizokopesha wakati wa kampeni za 2005, Freeman Mboe ambaye hadi sasa ni Mwenyekiti wa chama changu katika ngazi ya Taifa naye kwa taarifa nilizo nazo ni kwamba kila mwezi hulipwa shilingi milioni 10 ili kufidia fedha anazodai kukikopesha chama ambazo ni zaidi ya milioni 500 katika kampeni hizo hizo na hadi sasa anaendelea kukidai chama mamilioni ya shilingi.

Mimi nilipoonyesha wasiwasi juu ya madeni haya yasiyoisha, ikaundwa tume ya kampeni za kutokuwa na imani na mimi. Binafsi sijui kama viongozi wanaojiita makini kama kina Dr. Slaa na Kabwe Zitto wangeweza kuusimamia ufisadi mkubwa kama huu ndani ya chama huku wakiwa mstari wa mbele kuwafichua mafisadi Serikalini. Au ni kawaida kuwa Mganga hajigangi? CHADEMA kuna ufisadi wa aina nyingi sana kuanzia uchapaji bendera hadi manunuzi ya vifaa vya chama!

Katika ofisi ya Vijana nako kunanuka ufisadi kwani ni vijana wachache sana ambao hupata nafasi ya kwenda nje ilhali mikoani nako kuna vijana wanaohitaji kujifunza. Ofisi hii ina watu maalumu wa kwenda kwenye Semina na Matamasha mbalimbali. Na watu hao hupangwa na John Mnyika.

Suala la ukabila ni jambo ambalo halihitaji kupingwa kwani asilimia 85 ya viongozi wa CHADEMA wametoka katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha pamoja na kwamba baada ya mimi kulishupalia jambo hili wameanza kubadilisha majina.
WAPENDA HAKI NA USAWA TUTAZIDI KUKUKUMBUKA DAIMA!
 
RIP Comrade, makamanda wa chadema tunakukumbuka sana, tunakumbuka uwezo wako wa kuipigania haki za wanyonge
 
Tujuwe nani kausika na kifo cha chacha wangwe anaejuwa ataje

Mkuu unauliza makofi polisi,waliofnya unyama ni viongoz wa chadema akiwemo mbowe na mwenzake slaa na baadhi ya viongoz wengine,ila naona damu ya zakayo chacha inawatafuna na ndio hyo mpaka leo inawakosesha amani kwenye chama chao cha kikabila
 
Mkuu unauliza makofi polisi,waliofnya unyama ni viongoz wa chadema akiwemo mbowe na mwenzake slaa na baadhi ya viongoz wengine,ila naona damu ya zakayo chacha inawatafuna na ndio hyo mpaka leo inawakosesha amani kwenye chama chao cha kikabila

A failure always have a reason to back up his folly.
 
Mkuu unauliza makofi polisi,waliofnya unyama ni viongoz wa chadema akiwemo mbowe na mwenzake slaa na baadhi ya viongoz wengine,ila naona damu ya zakayo chacha inawatafuna na ndio hyo mpaka leo inawakosesha amani kwenye chama chao cha kikabila

Mbowe na Slaa! Kwa hiyo serikali inawaogopa hawa jamaa hata wakiua hawakamatwi! Mhh! Tuache kufike huko siasa za namna hii hazijengi bali hata wewe nafsi yako kuna wakati inalipuka na kukusuta.

R.I.P Kamanda chacha wangwe
 
Back
Top Bottom