Rest in peace comrade Chacha Wangwe

Rest in peace comrade Chacha Wangwe

CHACHA WANGWE/ CHACHA RASTA

Ni miaka 6 imepita tokea ulipotutoka usiku ule wa tarehe 28/7/2008. Bado jina lako linakumbukwa na watanzania wengi ilihali ipo wazi kuwa, wabunge waliotukoka katika bunge lile la tisa walikuwa wengi lakini jina lako ni miongoni mwa majina machache ambayo bado yako vichwani mwa watanzania.

Hii ni kutokana na matendo yenu, misimama, ujasiri na umahiri wenu wa ujengaji na usimamiaji kuntu wa hoja kwa maslahi ya taifa letu.

Mzee, unakumbukwa sana na wanatarime waliokuamini na kukutunuku nafasi mbili za uongozi (Udiwani na Ubunge) na hatimaye na watanzania wengine kukufahamu.

Kumbukumbu hii hutokea hasa wanapokumbwa na mambo magumu yanayogusa maisha yao moja kwa moja. Hii ni kutokana na kutopata viongozi ambao hawako tayari kutetea maslahi yao (wananchi) kwa hali yoyote ile na hata kutokuwa tayari kuweka maisha yao rehani kwa maslahi ya wanyonge wa Tarime na Tanzania kwa ujumla. Wanatarime tumeendelea kukuso viongozi Wa kaliba yako.

Viongozi wengi ambao tumewapa ridhaa ya kututumikia ni wale ambao wanadhani kujipendekeza, kugawa watu katika makundi ili wakose umoja wa kusimamia uwajibikaji na mstakabali chanya wa maendeleo ya Tarime ndio mbinu mbadala ya utumishi. Viongozi wafyata mikia pale ujasiri wao unapohitajika, halikadhalika viongozi ambao wamekosa kabisa weledi wa ujengaji wa hoja na ushawishi wawapo ndani ya vyombo vya uwakilishi. HIVI NIVIKWAZO VINGINE VYA MAENDELEO.

Nyamongo kumegeuka kuwa dead zone ( sehemu ya kifo)

Vijana wetu wameendelea kuawa kama kuku kwa makusudi na polisi wasiokuwa na uzalendo, sio tu kwamba serikali yetu imeweka rehani maisha na utu wa watanzania kwa anasa za mtu mweupe, lakini pia imeendelea kuhatarisha maisha ya mifugo na mimea kwa maji yenye kemikali hatari za sumu yanayo tiririka kwenye makazi ya watu. Hata fedha ambazo Mgodi ulikuwa unatoa kwa halimashauri ya Tarime kwajili ya vijana wetu kusoma bure, leo zimekuwa ni ndoto. HAKUNA FEDHA TENA. Nina asilimia zote chini ya uongizi wako usingekubali kufyata mkia katika hili. HII NI FEDHEHA KWA TAIFA LETU.

Mzee, CHADEMA uliyoiacha Tarime siyo iliyopo kwa sasa. Hata vikao vilivyokuwa vinatumika kujadili mikakati jadidi namna gani ya kukabiliana na wadhalimu na wahujumu maendeleo ya Wanatarime, leo vimegeuka kuwa sehemu ya ndondi na kutupiana maneno kwa faida, anasa na fuaha ya watu wachache ambao wameendelea kuendeleza uhasimu ndani ya chama.

Hii dhambi ya makundi ya mahasimu imeendelea kudhorotesha ustawi wa chama na hatimae kutoa mianya hata watu wenye uwezo kiduchu kushinda uchaguzi. HII NI DHAMBI AMBAYO INAENDELEA KUKITAFUNA CHAMA licha ya jitihada za makusudi ambazo wanachama tusio amini kwenye dhambi hiyo kuendelea kukiunganisha Chama kwa maslahi ya kujenga demokrasia shindani (competitive democracy) kwa maslahi ya jimbo letu.

TUTAENDELEA KUKUENZI,
TUTAENDELEA KUKUMBUKA .

MUNGU AKULAZE MAHALA PEMA PEPONI,
Amen.

Zakayo Chacha Wangwe
 
Dj na SILAHA watoe ripoti ya ukweli chanzo cha KIFO chake maana kama Zito nae asingeaga kwao hii EID angeiskia kwenye bomba!!


Sent from my iPad Air using JamiiForums mobile app
 
CHACHA WANGWE/ CHACHA RASTA

Ni miaka 6 imepita tokea ulipotutoka usiku ule wa tarehe 28/7/2008. Bado jina lako linakumbukwa na watanzania wengi ilihali ipo wazi kuwa, wabunge waliotukoka katika bunge lile la tisa walikuwa wengi lakini jina lako ni miongoni mwa majina machache ambayo bado yako vichwani mwa watanzania.

Hii ni kutokana na matendo yenu, misimama, ujasiri na umahiri wenu wa ujengaji na usimamiaji kuntu wa hoja kwa maslahi ya taifa letu.

Mzee, unakumbukwa sana na wanatarime waliokuamini na kukutunuku nafasi mbili za uongozi (Udiwani na Ubunge) na hatimaye na watanzania wengine kukufahamu.

Kumbukumbu hii hutokea hasa wanapokumbwa na mambo magumu yanayogusa maisha yao moja kwa moja. Hii ni kutokana na kutopata viongozi ambao hawako tayari kutetea maslahi yao (wananchi) kwa hali yoyote ile na hata kutokuwa tayari kuweka maisha yao rehani kwa maslahi ya wanyonge wa Tarime na Tanzania kwa ujumla. Wanatarime tumeendelea kukuso viongozi Wa kaliba yako.

Viongozi wengi ambao tumewapa ridhaa ya kututumikia ni wale ambao wanadhani kujipendekeza, kugawa watu katika makundi ili wakose umoja wa kusimamia uwajibikaji na mstakabali chanya wa maendeleo ya Tarime ndio mbinu mbadala ya utumishi. Viongozi wafyata mikia pale ujasiri wao unapohitajika, halikadhalika viongozi ambao wamekosa kabisa weledi wa ujengaji wa hoja na ushawishi wawapo ndani ya vyombo vya uwakilishi. HIVI NIVIKWAZO VINGINE VYA MAENDELEO.

Nyamongo kumegeuka kuwa dead zone ( sehemu ya kifo)

Vijana wetu wameendelea kuawa kama kuku kwa makusudi na polisi wasiokuwa na uzalendo, sio tu kwamba serikali yetu imeweka rehani maisha na utu wa watanzania kwa anasa za mtu mweupe, lakini pia imeendelea kuhatarisha maisha ya mifugo na mimea kwa maji yenye kemikali hatari za sumu yanayo tiririka kwenye makazi ya watu. Hata fedha ambazo Mgodi ulikuwa unatoa kwa halimashauri ya Tarime kwajili ya vijana wetu kusoma bure, leo zimekuwa ni ndoto. HAKUNA FEDHA TENA. Nina asilimia zote chini ya uongizi wako usingekubali kufyata mkia katika hili. HII NI FEDHEHA KWA TAIFA LETU.

Mzee, CHADEMA uliyoiacha Tarime siyo iliyopo kwa sasa. Hata vikao vilivyokuwa vinatumika kujadili mikakati jadidi namna gani ya kukabiliana na wadhalimu na wahujumu maendeleo ya Wanatarime, leo vimegeuka kuwa sehemu ya ndondi na kutupiana maneno kwa faida, anasa na fuaha ya watu wachache ambao wameendelea kuendeleza uhasimu ndani ya chama.

Hii dhambi ya makundi ya mahasimu imeendelea kudhorotesha ustawi wa chama na hatimae kutoa mianya hata watu wenye uwezo kiduchu kushinda uchaguzi. HII NI DHAMBI AMBAYO INAENDELEA KUKITAFUNA CHAMA licha ya jitihada za makusudi ambazo wanachama tusio amini kwenye dhambi hiyo kuendelea kukiunganisha Chama kwa maslahi ya kujenga demokrasia shindani (competitive democracy) kwa maslahi ya jimbo letu.

TUTAENDELEA KUKUENZI,
TUTAENDELEA KUKUMBUKA .

MUNGU AKULAZE MAHALA PEMA PEPONI,
Amen.

Zakayo Chacha Wangwe

Kijana Zakayo Chacha Wangwe, piga kazi acha kutafuta huruma kupitia msiba wa Baba yako. Kama unaona kuna ombwe la siasa huko Tarime, si uingie wewe kwenye siasa halafu tuone mchango wako?
 
Last edited by a moderator:
mkuu, rekebisha huo mwaka aliofariki Mzalendo na kuwaacha wahafidhina wakiwatesa wazalendo wengine, siyo 2014
 
Kijana Zakayo Chacha Wangwe, piga kazi acha kutafuta huruma kupitia msiba wa Baba yako. Kama unaona kuna ombwe la siasa huko Tarime, si uingie wewe kwenye siasa halafu tuone mchango wako?

Anawakumbusha wahafidhina kwa kile walichokifanya, kamwe hatuwezi kunyamazishwa tusimkumbuke aliyekuwa mzalendo wetu wa Tarime na RORYA.
 
Kashawekwa kibindoni na Zitto huyo. Namfahamu vizuri! Njaa tupu huyo. Kwa maneno yupo chadema lakini ni mwana ACT mtiifu

Deus Mallya na Mbowe sijui wanajisikiaje sasa hivi..
 
Dj na SILAHA watoe ripoti ya ukweli chanzo cha KIFO chake maana kama Zito nae asingeaga kwao hii EID angeiskia kwenye bomba!!


Sent from my iPad Air using JamiiForums mobile app

kweli kabisa,, mbowe atueleze ukweli
 
KUMBUKUMBU YA HAYATI CHACHA WANGWE

Ni miaka sita(6) sasa tangu alipotutoka aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Tarime,Diwani wa kata ya Tarime Mjini, Waziri kivuli wa Maji, Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mara na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Baba yetu mpendwa Hayati Chacha Zakayo Wangwe kwa kifo kilichogubikwa na sintofahamu mpaka leo,
kilichotokea mnamo tarehe 28/07/2014 maeneo ya Pandambili,wilayani Kongwa.

Kwa niaba ya Familia ya Wangwe, wananchi wa Tarime na wanachama wa CHADEMA napenda kusema kuwa tanakumbuka sana uwepo wako Comrade Wangwe,na tutakukumbuka na kukuenzi daima..Mbele yako,nyuma yako.

REST IN PEACE TATA.
M B O R A K E (KUTAKUCHA)

Hebu rekebisha hiyo tarehe.......
 
Wacha wafu wazike wafu wao....Kesha kwenda(kufa) hakuna haja ya kumkumbuka...

Alazwe mahali anapostahil..
 
Anawakumbusha wahafidhina kwa kile walichokifanya, kamwe hatuwezi kunyamazishwa tusimkumbuke aliyekuwa mzalendo wetu wa Tarime na RORYA.

Aibu sana kijana mdogo anatumika kwa maslahi ya watu asiowajua, na yeye kwa njaa zake anakubali kutumiwa kama 'ndomu. bado narudia, suluhu ya shida zake siyo kutumia kifo ch baba yake kujidhalilisha, bali apambane kivyake ili kumuenzi baba yake , angalau tujue aliacha jembe nyuma kama yeye !
 
Dj na SILAHA watuambie ukweli wa KIFO chake!!


Sent from my iPad Air using JamiiForums mobile app
 
Nimepata mashaka na nia yako kwa uzi huu. Hiyo tarehe ambayo nimeibold kweli ndio tarehe husika? Kama umeleta mada yako kwa hila ona wewe muhusika unavyoanza kujichanganya katika kitu muhimu kama hicho. BTW ni kweli kuwa wewe ni mmoja wa waratibu wa ACT?
unamatatizo sana wewe,ulivyoandika kwa kurupuka mi nilijua una la kuongeza. haya taja basi iyo tarehe sahihi ya kifo cha wangwe!
 
Back
Top Bottom