'Reputation-Personal Branding' aka 'The Mhogo Mchungu's'

'Reputation-Personal Branding' aka 'The Mhogo Mchungu's'

Kongosho

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2011
Posts
35,987
Reaction score
24,226
MMh, sijui kama nitaelezea kwa ufasaha.
Ila nalenga kwenye mahusiano ya kimapenzi zaidi.

Kuna hii tabia ya baadhi ya watu 'kuji-brand' kama bidhaa ili kwendana na soko la eneo hilo hasa mnapokutana kwa mara za mwanzo, mnaanza kutongozana, nia ikiwa ni kuelekea kwenye mapenzi. Unakuta mtu kajipimp personality kuanzia jina, harufu, mwonekano(Brazillian inahusu kidogo ili kuwa uantingisha kichwa nywele zikija usoni), mtembeo(kuna ule mtembeo wa haraka haraka wa kizungu na high heels kama farasi vile), accent, na hata story anazoongelea ili kupata market penetration ya kutosha

Mfano, unaweza kuta binti ana-adopt tabia mpya kama mavazi, kuongea na interest ili kwendana na mabinti waliomzunguka ambao anadhani wana soko kwenye mahusiano. Simaanishi kwamba anajiuza,hapana. mtu anabadili tu tabia ili apate mtu wa aina fulani waweze kuendana. Wakati mwingine inapunguza ile 'being yourself'

Katika kuji-brand huku, ambako ni 'superficial', ukianza kumzoea unaanza kugundua kuwa zile si tabia zake halisi, unaanza muona kama alikuwa feki. Lakini ukimuuliza yeye anaweza kuwa hajui ama anajua kama kajibrand.
Kama ujuavyo, huwezi kuwa kwenye 'brand mode' 24/7, kuna saa 'wewe' wa ukweli atajitokeza tu.

Hii imepelekea baadhi ya watu kuwatungia jina la 'The Mhogo Mchungu's', hii inatokana na lile tangazo la wakala wa Mpesa kujiita Branch Manager wa NMB, ni kweli anafanya kazi za NMB lakini kiuhalisia yeye ni wakala tu.

Branding ipo sana online pia.

Swali langu, je personal branding inasaidia kwenye mahusiano? Long term? Short term?
Ukikutana na mpenzi ambaye alijibrand na ikakudissapoint, what to do kama unataka kuendelea naye?

Msaada tafadhali
 
as for me i like someone who is smart, but sipendi kabisa mtu anayejibadilisha just for the sake ya kutaka attention za watu fulan ama mtu fulan.

i like being i hasa kimwonekano like hata ngozi, nywele, kucha, macho, meno, matiti, makalio etc viwe vile nilivyozaliwa navyo. kuvipamba kwa namna ya rangi like nail polishing, hair curling, kutream/shaping ya nnyusi to me ni urembo.

but ukijiweka kimuhogo mchungu's kwangu huna taste kabisaaaaaaaaaaaa manake nikikuona ni mdada halafu umeweka makucha ya bandia, nyusi za bandia, ukapigilia mawigi nitasema umependeza ila kukupa credit ya uzuri siwez hata kidogo.

kwangu mimi huwa nasemaga wanaume ni viumbe walioumbwa wazuri sana, sana, hawana brands za kujipigilia kuharibu walivyo and huwaga na assume wangekuwa na wao wanajipigilia mafake kama sisi wanawake sijui ingekuwaje. but real wanaume ni wazuri sana wa sura na mwonekano wao wa kiume na wanawake ni warembo tu.
 
Watu wenyewe wa siku hizi, ujue ukiwa "muhogo mchungu" unapata mahusiano fake kutoka kwa "muhogo mchungu" vile vile.

Napenda mtu asiyenifaham ani underestimate kuliko nikijibrand zaidi ya uhalisia wangu, akija kujua uhalisia wangu atakua na brand nyingi mbaya za kunibrand. Hii sio kwenye mapenzi tu, hata kwenye mahusiano ya kawaida.

Nakumbuka mambo ya Mtambuzi kwenye "shemeji piga mzigo"
 
He he he, makucha na kope hoyee
Anyway siongelei urembo sana hapa[

Naongelea kubrand personality ili kuendana na soko

Unaweza kuta mtu kaupura kweli kweli, ila anaendelea kuwa 'yeye'

Wanamme hawaupuri, ila na wao wapo kibao wanajibrand

as for me i like someone who is smart, but sipendi kabisa mtu anayejibadilisha just for the sake ya kutaka attention za watu fulan ama mtu fulan.

i like being i hasa kimwonekano like hata ngozi, nywele, kucha, macho, meno, matiti, makalio etc viwe vile nilivyozaliwa navyo. kuvipamba kwa namna ya rangi like nail polishing, hair curling, kutream/shaping ya nnyusi to me ni urembo.

but ukijiweka kimuhogo mchungu's kwangu huna taste kabisaaaaaaaaaaaa manake nikikuona ni mdada halafu umeweka makucha ya bandia, nyusi za bandia, ukapigilia mawigi nitasema umependeza ila kukupa credit ya uzuri siwez hata kidogo.

kwangu mimi huwa nasemaga wanaume ni viumbe walioumbwa wazuri sana, sana, hawana brands za kujipigilia kuharibu walivyo and huwaga na assume wangekuwa na wao wanajipigilia mafake kama sisi wanawake sijui ingekuwaje. but real wanaume ni wazuri sana wa sura na mwonekano wao wa kiume na wanawake ni warembo tu.
 
Unachojaribu sema kuwa Brand anapata brand mwenzie?

Is it always the case?

Watu wenyewe wa siku hizi, ujue ukiwa "muhogo mchungu" unapata mahusiano fake kutoka kwa "muhogo mchungu" vile vile.

Napenda mtu asiyenifaham ani underestimate kuliko nikijibrand zaidi ya uhalisia wangu, akija kujua uhalisia wangu atakua na brand nyingi mbaya za kunibrand. Hii sio kwenye mapenzi tu, hata kwenye mahusiano ya kawaida.

Nakumbuka mambo ya Mtambuzi kwenye "shemeji piga mzigo"
 
Its easy being your self huh?!

Kuna wengine huwa wanasema kwenye mahusiano 'The No-Strategy Strategy' pays.

Simple and clear being "me, myself and i" keeps life stresses away.
 
Unachojaribu sema kuwa Brand anapata brand mwenzie?

Is it always the case?

Hapo kuna mawili, kama mwanaume ameshajua umejibrand na yeye atakupa mahusiano ya brand hiyo hiyo au ataachana na wewe.
 
Biashara matangazo, kama mtu ameweza kujibrand na akatoka, hayo mengine mbele kwa mbele!
 
kwakweli kuwa mhongo mchungu's hiyo haileti picha nzuri kwa mwanamke hayo ni mapenzi kizushi:frusty:
 
Mtu akiwa yuko update na life style ni vizuri kwani anakuwa anaweza kujiintroduce kwa watu na watu wakamkubali kupitia looking appearance yake, unamkuta mtu yuko smart kuanzia chini hadi juu, ukija kwenye speaking style yake ndo usiseme yaani akianza kuongea na wewe unajikuta mawazo yanahama na kuona kama vile umehamia sayari nyingine.

Mtu anakuwa ana manjonjo fulani mpaka anakufanya uzidishe mapenzi kwake like (dressing style, motion, ubunifu wa mambo).
Kwanza hata ukitembea nae unajiona ni mtu kati ya watu ukilinganisha na ukitembea mwenyewe. Anakufanya na wewe uanze kujitreat vizuri like kupiga pamba za ukweli ili uweze himili level standard yake. Hii inakusaidia na wewe kujiweka safi muda(unakuta mtu ulikuwa hujijali uli ulivyompata huyo mbunifu wa mambo sasa hivi na wewe unakuwa smart muda wote).

Ukikutana na mtu aliyejibrand alafu akakudisappoint chakufanya ni kuangalia nini kilimpelekea akakudissapoint, labda ni wewe ulishindwa kumpa vile vitu alivtotaka ili aendelee na swagger zake za kawaida au huenda amekua mtu mzima na amaeona hayo mambo hayamfai kwa wakati huo.
 
Ha ha ha, haya bana

Lakini je, kwenye kumaintain mahusiano? Hasa kama unalenga ya muda mrefu?

Biashara matangazo, kama mtu ameweza kujibrand na akatoka, hayo mengine mbele kwa mbele!
 
Biashara matangazo, kama mtu ameweza kujibrand na akatoka, hayo mengine mbele kwa mbele!

hapa kwa hiyo unafanya kazi ya kumrusha roho mtu angali haupo kiivo sasa ndio unauliza kwa nini ujibrand na usioneshe yourr original colour hii ni hali ya kutojiamini men..
 
MMh, sijui kama nitaelezea kwa ufasaha.
Ila nalenga kwenye mahusiano ya kimapenzi zaidi.

Kuna hii tabia ya baadhi ya watu 'kuji-brand' kama bidhaa ili kwendana na soko la eneo hilo hasa mnapokutana kwa mara za mwanzo, mnaanza kutongozana, nia ikiwa ni kuelekea kwenye mapenzi. Unakuta mtu kajipimp personality kuanzia jina, harufu, mwonekano(Brazillian inahusu kidogo ili kuwa uantingisha kichwa nywele zikija usoni), mtembeo(kuna ule mtembeo wa haraka haraka wa kizungu na high heels kama farasi vile), accent, na hata story anazoongelea ili kupata market penetration ya kutosha

Mfano, unaweza kuta binti ana-adopt tabia mpya kama mavazi, kuongea na interest ili kwendana na mabinti waliomzunguka ambao anadhani wana soko kwenye mahusiano. Simaanishi kwamba anajiuza,hapana. mtu anabadili tu tabia ili apate mtu wa aina fulani waweze kuendana. Wakati mwingine inapunguza ile 'being yourself'

Katika kuji-brand huku, ambako ni 'superficial', ukianza kumzoea unaanza kugundua kuwa zile si tabia zake halisi, unaanza muona kama alikuwa feki. Lakini ukimuuliza yeye anaweza kuwa hajui ama anajua kama kajibrand.
Kama ujuavyo, huwezi kuwa kwenye 'brand mode' 24/7, kuna saa 'wewe' wa ukweli atajitokeza tu.

Hii imepelekea baadhi ya watu kuwatungia jina la 'The Mhogo Mchungu's', hii inatokana na lile tangazo la wakala wa Mpesa kujiita Branch Manager wa NMB, ni kweli anafanya kazi za NMB lakini kiuhalisia yeye ni wakala tu.

Branding ipo sana online pia.

Swali langu, je personal branding inasaidia kwenye mahusiano? Long term? Short term?
Ukikutana na mpenzi ambaye alijibrand na ikakudissapoint, what to do kama unataka kuendelea naye?

Msaada tafadhali

ina saidia in short term running hasa anapokuwa anatafutwa mtu either muke au mume chezea wadada na wakaka wa mujini wewe..
 
Ha ha ha, haya bana

Lakini je, kwenye kumaintain mahusiano? Hasa kama unalenga ya muda mrefu?
Hapo itategemea zaidi anawezekana akawa na artifial kibao but ukatokea kumpenda kwa kakitu kadogo tu na ukaamua kumrekebisha na akarudi normal!

Chezea soko huria weye?

Hujaona dem wa uswaz kaenda ushuani anataka salad ya moto na anapenda kwenda london na si UK!

So nikumrekebisha tu kama unaona analipa !
 
Mtu akiwa yuko update na life style ni vizuri kwani anakuwa anaweza kujiintroduce kwa watu na watu wakamkubali kupitia looking appearance yake, unamkuta mtu yuko smart kuanzia chini hadi juu, ukija kwenye speaking style yake ndo usiseme yaani akianza kuongea na wewe unajikuta mawazo yanahama na kuona kama vile umehamia sayari nyingine..
Labda cha kujiuliza, ni ku-update lifestyle ni nini? Na kujibrand ni nini?
Naona kama unanichanganya ama unaniwekea mada 2 tofauti

Mfano, nilipokuwa nasoma sababu ya ukata nilikuwa nanyoa, navaa viatu vya 10,000 tu
Sasa nina kazi nasuka, na navaa kiatu cha 100,000. Hii ni brabding au kuji-update sababu waweza afford?

Mtu anakuwa ana manjonjo fulani anakufanya uzidishe mapenzi kwake like dressing style, kwanza hata ukitembea nae unajiona ni mtu kati ya watu ukilinganisha na ukitembea mwenyewe. Anakufanya na wewe uanze kujitreat vizuri like kupiga pamba za ukweli ili uweze himili level standard yake. Hii inakusaidia na wewe kujiweka safi muda wote na muda mwingine unakuwa na swagger flani..

Kuwa na manjonjo ni sawa, je ni mamnjonjo ya asili au ni ya kujipaka?
Hivi, unaweza kukopa swagger kwa muda Karucee nisaidie hapa

Ukikutana mna mtu aliyejibrand alafu akakudisappoint chakufanya ni kuangalia nini kilimpelekea akakudissapoint, labda ni wewe ulishindwa kumpa vile vitu alivtotaka ili aendelee na swagger zake za kawaida au huenda amekua mtu mzima na maeona hayo mambo yameshapitwa na wakati.

Hivi mtu mwenye swagger zake, mie wa pembeni kuna ninachotakiwa kumsaidia ili ameintain hizo swagger?
Je swagger = personality?
 
Last edited by a moderator:
He he he, makucha na kope hoyee
Anyway siongelei urembo sana hapa[

Naongelea kubrand personality ili kuendana na soko

Unaweza kuta mtu kaupura kweli kweli, ila anaendelea kuwa 'yeye'

Wanamme hawaupuri, ila na wao wapo kibao wanajibrand
hivi mtu unaweza kujibrand utu wa ndani??
mara nyingi naona ni utu wa nje na ndio maana mm naona huwa unaendana na mapambo zaid.
 
Kuna vingine vinarekebishika hasa kama ni material things

Lakini kuna 'the inner' person ukikuta siye ulyedhani ndiye?

Hapo itategemea zaidi anawezekana akawa na artifial kibao but ukatokea kumpenda kwa kakitu kadogo tu na ukaamua kumrekebisha na akarudi normal!

Chezea soko huria weye?

Hujaona dem wa uswaz kaenda ushuani anataka salad ya moto na anapenda kwenda london na si UK!

So nikumrekebisha tu kama unaona analipa !
 
He hujaona?

Ndo maana nasema utu wa ndani unaubrand kwa muda, ila haiwezi kuwa 24/7

Hujawahi kakopa 'uelewa' kwa masaa?

Au huwahi kuta mtu kakopa reputation?

hivi mtu unaweza kujibrand utu wa ndani??
mara nyingi naona ni utu wa nje na ndio maana mm naona huwa unaendana na mapambo zaid.
 
Back
Top Bottom