Tume iliyoundwa kuchunguza ubadirifu wa fedha walizokula kina Jairo hawa kwanini hawakuhusishwa nao pia lazima sheria iwachukulie hatua tena kali sana ikiwezekana hata kufungwa!
Tume iliyoundwa kuchunguza ubadirifu wa fedha walizokula kina Jairo hawa kwanini hawakuhusishwa nao pia lazima sheria iwachukulie hatua tena kali sana ikiwezekana hata kufungwa!
Kuwatambua itakuwa issue maana wengi wao wametupa migongo!
Jairo Luhanjo na Ngeleja wanatosha kuwawakilisha hao
Mkuu, umasikini huu ni shida kweli, ukiwaona hao jamaa walivyotunisha masaburi yao utadhani wanatafuta promotion, nadhani na baba yao wizarani pia alikimbia bunge siku ile kwenda kuhudhuria mapokezi ya mdogo wake huyo.. gharama zote hizo zinalipiwa na sisi..duhKweli Permanent Secretaries ni miungu watu. Mtu mzima unatoka nyumbani unaaga familia unakwenda kazini halafu kamera inakuchukua uko kwenye shughuli ya aibu hivi? Kweli rushwa na ufisadi vinaleta upofu. Kama Mch. Israel Natse (Karatu) alivyosema kwenye kuchangia ripoti ya kamati teule (yeye alikuwa mjumbe), Mungu amependa kuleta ukombozi kwa waja wake kupitia uozo huu wa maadili. Hii ilikuwa dharau kubwa kwa Bunge. Itakumbukwa kuwa muda mfupi baada ya zoezi hili Jairo alitoka akachukua Taxi kuondoka ofisini baada ya JK kuagiza vinginevyo. Wanatakiwa wamalizie kazi ya kumsukuma kuelekea nyumbani na baadaye Segerea. Bahati mbaya ni hao hao wanafurika kwenye nyumba za Ibada kumwomba Mungu. Ni Mungu yupi wanayemlilia? Ni huyu huyu ambaye watoto wanaokaa chini darasani, wajawazito wanaojifungulia barabarani, wagonjwa wanaokufa bila dawa kwenye zahanati zetu, watu wanaochangia maji ay tope na wanyama hata baada ya miaka 50 ya uhuru?. Nadhani atakuwa Mungu tofauti.
Haya wakuu ile taarifa ya kamati teule kuchunguza uhalali wa uchangishaji feddha aliofanya Jairo hii hapa. Enjoy!!!!!
Lazima tumshinikize kwa sababu hiyo kazi siyo ya baba yake ni yetu.Mmejaa speculation zisizo na msingi. Mwacheni afanye maamuzi bila shinikizo lenu. Bunge limeshaamua, mnataka nini tena?