Hivi kwanini mtu yeyote yule akiongelea UFISADI wana-CCM wote (I believe mafisadi ni wachache sana) wake kwa waume wanachamaa, lete ushahidi, wataje majina, wapaeleke mahakamani etc.
Hivi mnataka kutuaminisha wengine kwamba UFISADI ni sera ya CCM?! Kwa mawazo yangu UFISADI hauna rangi wala chama cha siasa, badala ya kuwakingia kifua mafisadi tupigane nao bila kujali ni CCM, CDM, CUF, NCCR etc vinginevyo tutaonekana Taifa la ajabu linalolea na kushabikia UFISADI wakati wanaoshabikia UFISADI miguuni wamevaa kandambili zilizofungwa kwa wire.