Regia Mtema, John Mnyika, Zitto Kabwe na 90mil

Nimetoka kwenye Sports kule.. nimevutiwa na hili.. ! Hivi mishahara ya wakubwa kule mjengoni inakatwa kodi.
 
Ndugu wana JF ni wiki ya Tatu sasa tangu wabunge wetu waingiziwe kwenye akaunti zao kiasi cha Milioni 90,nimetaja wabunge hawa vijana watuambie hivi wanajisikiaje kupata kiasi hicho wakati wakijua hali ya maisha ya Watanzania kwa sasa? Ndugu zangu hivi tuige nini hasa tunapo ona wapiganaji wetu nao wanafanya makosa yaleyale ambayo ni sawa na Wabunge wa CCM! Dr slaa hivi umehoji kwa nini wabunge wako wamekubali kuingiziwa kiasi hicho bila kuangalia maisha yetu watanzania ambao wengi kwa sasa tuna weza kupata mlo mmoja kwa siku? Milioni 90 najua imetokana na jasho la walipa kodi! Nashauri kamati kuu ya Chadema ikae iliangalie suala hili lasivyo linatutia matope na kupoteza hata ile maana ya Chadema kuwa chama cha ukombozi kwa Watanzani! Mh Mnyika,Mh Zitto na Mh Mtema najua safari yenu bado ndefu kisiasa hivi kweli mumekubali kula hii hela haramu ya maskini wa kitanzania? Mh Regia Mtema hivi kweli Aluta Kontinua kwa namna hii! Mandela aliwahi kusema makaburu hawana uwezo wa kutuhonga kwa garama yeyote ile bali kilicho na thamani ni Maisha ya Watu wetu! Mmekubali kuhongwa kwa mkate kama askari wa kihindi! My take: ni mhimu tujipime kama chama cha ukombozi wa maskini wa watanzania walio wengi!


Where is your argument? Ulitaka wavunje sheria iliyopo wasilipwe hizo fedha?? maana malipo hayo ni kwa mujibu wa sheria iliyopo. Mimi nilifikiri unawashauri wakipata fedha hizo wazitumie kwa ajili ya kusaidia mkakati wa ukombozi wa tanzania mpya wanayoipigania!!!!!!!!!!!!
 
Huu ni wizi tu!!...kila jimbo liwe na gari la ofisi ya mbunge!.we did that during nyerere times...acheni kutafuta ujiko!

Kipindi cha Nyerere wabunge walikuwa wachache na pengine ndio maana ilikuwa rahisi kuwa na gari la ofisi ya mbunge katika kila jimbo. Sasa hivi ni majimbo yameongezeka na wabunge wa viti maalum na wale 10 wa kuteuliwa na rais wamefanya idadi iwe kubwa zaidi na kufanya ugumu wa wazo lako. Lakini pia kama Tsh.90 million zinatolewa kwa wabunge kwaajili ya gari litakalotumika kwa miaka mitano tatizo liko wapi? Ni afadhari wamepewa hela kila mmoja ajinunulie mwenyewe kuliko wangenunuliwa na bunge hicho kiwango kingeongezeka kutokana na ufisadi ambao ungefanyika katika manunuzi. Kama tuna dhamira ya kweli, basi tupinge mashangingi ya 200million ya mawaziri badala ya kuwabana wabunge na 90million!
 
Pendekeza wafanyie nini sio kulalamika tu.
Ulitaka wakatae au?

Husnina, ule ni mkopo watalipa, ni ngumu wao kuutumia kwa shuguli za umma ila ni makosa kUUKUBALI hapa chadema wametuangusha, inatupa tafsiri kwamba hata wao kama wabunge wengine wte walikuwa wanapigana kwenda mjengoni kwa maslahi binafsi zaidi
 
kama issue ni magari wangeweza kuchukua ikopo midogo, au wangefanya utaratibu mwingine b'se mbali na hiyo mikopo ya mil 90 bado wabunge wanalipwa pesa nyingi sana kama posho
 
Kipindi cha Nyerere wabunge walikuwa wachache na pengine ndio maana ilikuwa rahisi kuwa na gari la ofisi ya mbunge katika kila jimbo. Sasa hivi ni majimbo yameongezeka na wabunge wa viti maalum na wale 10 wa kuteuliwa na rais wamefanya idadi iwe kubwa zaidi na kufanya ugumu wa wazo lako. Lakini pia kama Tsh.90 million zinatolewa kwa wabunge kwaajili ya gari litakalotumika kwa miaka mitano tatizo liko wapi? Ni afadhari wamepewa hela kila mmoja ajinunulie mwenyewe kuliko wangenunuliwa na bunge hicho kiwango kingeongezeka kutokana na ufisadi ambao ungefanyika katika manunuzi. Kama tuna dhamira ya kweli, basi tupinge mashangingi ya 200million ya mawaziri badala ya kuwabana wabunge na 90million!
Ubunge siku hizi ni ulaji tu!...nakumbuka wakati wa vikao vya bunge gesti za uswazi zilikuwa zinapata sana biashara,na wabunge wengi wakitoka mikoani walikuwa wanakuja na public transportation,na hospitali tulikuwa hatulipi hata sentano!...shule daftari likiisha anapeleka kwa mwalimu anakupa jipya halafu unatafuta jalada kutoka gazeti la uhuru,hasa likiwa la ukurasa wa mwisho wa michezo.
Nilidhani hawa jamaa wangesusia mikopo hii ya kidizaini,ila nimegundua ndio walewale,leteni hela jimboni ,tutawalipia nauli ya treni.
 
Wakuu.Salaam.

Nimeona nichangia post hii kidogo.

Kwanza kabisa niweke rekodi sawa Fedha hizi za Gari hazijaanza kuigia kwa wiki tatu zilizopita kama mtoa mada alivyosema.Cheki zimeanza kutolewa kama siku nne au tatu zilizopita na zaidi ya asilimia 80 ya Wabunge bado hawajapata cheki zao,hata mimi bado sijapata.

La pili ni hili Milioni 90.Ifahamike kwamba Milioni hizi 90 wabunge hawapewi Bure tunakopeshwa na tunakatwa kupitia mishahara yetu.Bunge linalipa nusu ya pesa hizo yaani Milioni 45,Milioni 45 nyingine kila Mbunge anakatwa karibu shilingi 866,000 kwa mwezi kupitia mshahara wake.Kwahiyo Bunge linatoa shilingi Milioni 45 tu kwaajili ya gari.

La tatu Kimsingi Bunge limeweka Utaratibu ili kumsaidia Mbunge afanye vizuri kazi zake za Kibunge ilipendekezwa awe anatumia gari aina ya Toyota Hard Top Mpya ambayo kwa sasa gari hili linauzwa shiingi Milioni 112.Bunge likatafakari ikaonekana ni gharama kubwa kumpa kila Mbunge shilingi Milioni 112 hivyo busara ya wahusika wanaopanga maslahi ya wabunge wakaja na kiwango hiki cha Milioni 90 na Bunge kuchangia nusu ya pesa hizi. Bunge limependekeza aian hii ya gari kwakuwa ni imara inayoendana na miundumbinu ya majimbo mengi hapa nchini.Lakini kwa hali ilivyo watakao nunua ni wale wenye uwezo kipesa wengine trutakimbilia kwenye magari ya bei rahisi.

La nne ni mapendekezo ya baadhi ya watu eti wabunge wa CHADEMA wasichukue pesa hizo.Kimsingi hili sio pendekezo sahihi sasa wabunge hawa wa CHADEMA wasipochukua pesa hizi za gari nani atawanunulia magari ya kurahisisha kazi zao?hivi milioni 45 ni nyingi sana kwa kununua gari?kwa yeyote anayefahamu vizuri kazi ya Mbunge ndani ya Jimbo na miundombinu yetu hawezi kulalamika kuhusu hili. Gari imara kwa miaka 5 ni muhimu sana kwa Mbunge. Kwa wanaojua magari vizuri wanajua vizuri magari imara na mazuri kwa kazi za kisiasa zinauzwa shilingi ngapi. Vile vile Wabunge wa CHADEMA wasipochukua pesa hizi za magari itakuwa haina maana kwani Wabunge wa CHADEMA tuko 48 tu kati ya Wabunge 353 hivyo sisi tukikataa haitabadilisha chochote na badala yake pesa hizi zitaishia kwenye mikono ya wachache ambao hatutajua zimetumika vipi.Kuna msemo unasema ukisusa wenzio wala.Hoja ya msingi hapa ni kuwa Wabunge wa CHADEMA wapeleke hoja Bungeni ya Kupitia Upya Maslahi ya Wabunge ili kama kuna pesa zisizo na maana kwa mbunge basi ziondolewe kwa maslahi ya umma,hoja si kukataa milioni 90 kwa sasa.

La tano kwa upande wangu kwa kuwa mimi ni Mbunge maskini siwezi kuzipeleka Milioni 90 zote kwenye gari.Nitanunua gari la bei nzuri la kini lazima liwe imara na la kuvutia.Zingine zitafanya mambo ya msingi ndani ya Jimbo la Kilombero na mambo mengine madogo madogo.

Lasita mkubuke vile vile siku hizi hela imeshuka sana thamani Milioni 90 zinaisha ndani ya wiki moja na unaweza ukajikuta hakuna la maana ulilolifanya.

La mwisho kabisa hivi siku hizi ndio imekuwa mtindo wa kuwataja Zitto,Mnyika and Regia?Kuna Wabunge wengi sana humu Wanawake kwa Wanaume amabo ni wanachama tena wazuri tu isipokuwa hawatumii majina yao halisi.Ukija na taito yako ikataja jina la ujumla Wabunge utapata majibu mazuri toka kwao.Mkiwa very specific mnawabana wao wanaona kama hawahusiki hivyo hawatoi ushirikiano wa kutosha,sio lazima wajitaje majina yao sisi tunataka michango yao. Ni vizuri tukawa tunapanua wigo mpana wa kuruhusu Wabunge wengine wachangie kwa majina yao bandia.

Aluta Continua

Kutoka Miti Mirefu Mwanza
Regia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira
 
Husnina, ule ni mkopo watalipa, ni ngumu wao kuutumia kwa shuguli za umma ila ni makosa kUUKUBALI hapa chadema wametuangusha, inatupa tafsiri kwamba hata wao kama wabunge wengine wte walikuwa wanapigana kwenda mjengoni kwa maslahi binafsi zaidi

ni makosa kivipi wewe? Unataka wenzio waende bungeni na vibajaji au?
Mimi naomba roho za kwanini bado zinatusumbua watz.
Haya Regia huyo kashasema wanapewa 45 na 45 wanakopeshwa.
 
Ndugu wana JF ni wiki ya Tatu sasa tangu wabunge wetu waingiziwe kwenye akaunti zao kiasi cha Milioni 90,nimetaja wabunge hawa vijana watuambie hivi wanajisikiaje kupata kiasi hicho wakati wakijua hali ya maisha ya Watanzania kwa sasa? Ndugu zangu hivi tuige nini hasa tunapo ona wapiganaji wetu nao wanafanya makosa yaleyale ambayo ni sawa na Wabunge wa CCM! Dr slaa hivi umehoji kwa nini wabunge wako wamekubali kuingiziwa kiasi hicho bila kuangalia maisha yetu watanzania ambao wengi kwa sasa tuna weza kupata mlo mmoja kwa siku? Milioni 90 najua imetokana na jasho la walipa kodi! Nashauri kamati kuu ya Chadema ikae iliangalie suala hili lasivyo linatutia matope na kupoteza hata ile maana ya Chadema kuwa chama cha ukombozi kwa Watanzani! Mh Mnyika,Mh Zitto na Mh Mtema najua safari yenu bado ndefu kisiasa hivi kweli mumekubali kula hii hela haramu ya maskini wa kitanzania? Mh Regia Mtema hivi kweli Aluta Kontinua kwa namna hii! Mandela aliwahi kusema makaburu hawana uwezo wa kutuhonga kwa garama yeyote ile bali kilicho na thamani ni Maisha ya Watu wetu! Mmekubali kuhongwa kwa mkate kama askari wa kihindi! My take: ni mhimu tujipime kama chama cha ukombozi wa maskini wa watanzania walio wengi!

Mmh Sijui....

yangu macho.
 
hv kila mmoja akinunua cresta inabaki sh ngap? Hao watu wanapaswa wakae watulie, wafanye maamuz ya busara, 90mls ni nyingi sana, 35 ml unapata cruser v8 used safi. WATUMIE HZ PESA KTK MAMBO YA MSINGI.
 
Tofautisha kati ya gari mpya,na gari inayoonekana mpya.......
Toyota rav 4 ya mil 24 ni ile inayoonekana mpya(second hand)
toyota rav 4 mpya ni kama mil 35 hadi 40
......na hiyo rav 4,zito atatoka nayo kigoma dodoma daresalaam mara ngapi?na yule jamaa wa kagera?.....hahahaha

Hapo bado hujaona tutakuwa tumesave kama 50M ? Kama ushawai kuitumia rav-4 nazani ungekuwa unajua uwezo wake! Mie binafsi nishapiga nayo misele kutokea dar mpaka bukoba,ni gari ya field kwakweli; hata mafuta watatumia vema sio kama v8.

Kwaio wangepewa mayb hio 40M nyingine watop-up wenyewe kama wanataka ufahari! Ah kwanza hio hela ipewe jimbo husika, na wengine nao wanaomfuata walitumie;ili likichoka litangamzwe mnada jimboni,chochote kipatikanacho kitumike kutop-up kununua lingine! Sio mambo ya ujanja ujanja tuuuu
 
Wakuu.Salaam.

Nimeona nichangia post hii kidogo.

Kwanza kabisa niweke rekodi sawa Fedha hizi za Gari hazijaanza kuigia kwa wiki tatu zilizopita kama mtoa mada alivyosema.Cheki zimeanza kutolewa kama siku nne au tatu zilizopita na zaidi ya asilimia 80 ya Wabunge bado hawajapata cheki zao,hata mimi bado sijapata.

La pili ni hili Milioni 90.Ifahamike kwamba Milioni hizi 90 wabunge hawapewi Bure tunakopeshwa na tunakatwa kupitia mishahara yetu.Bunge linalipa nusu ya pesa hizo yaani Milioni 45,Milioni 45 nyingine kila Mbunge anakatwa karibu shilingi 866,000 kwa mwezi kupitia mshahara wake.Kwahiyo Bunge linatoa shilingi Milioni 45 tu kwaajili ya gari.

La tatu Kimsingi Bunge limeweka Utaratibu ili kumsaidia Mbunge afanye vizuri kazi zake za Kibunge ilipendekezwa awe anatumia gari aina ya Toyota Hard Top Mpya ambayo kwa sasa gari hili linauzwa shiingi Milioni 112.Bunge likatafakari ikaonekana ni gharama kubwa kumpa kila Mbunge shilingi Milioni 112 hivyo busara ya wahusika wanaopanga maslahi ya wabunge wakaja na kiwango hiki cha Milioni 90 na Bunge kuchangia nusu ya pesa hizi. Bunge limependekeza aian hii ya gari kwakuwa ni imara inayoendana na miundumbinu ya majimbo mengi hapa nchini.Lakini kwa hali ilivyo watakao nunua ni wale wenye uwezo kipesa wengine trutakimbilia kwenye magari ya bei rahisi.

La nne ni mapendekezo ya baadhi ya watu eti wabunge wa CHADEMA wasichukue pesa hizo.Kimsingi hili sio pendekezo sahihi sasa wabunge hawa wa CHADEMA wasipochukua pesa hizi za gari nani atawanunulia magari ya kurahisisha kazi zao?hivi milioni 45 ni nyingi sana kwa kununua gari?kwa yeyote anayefahamu vizuri kazi ya Mbunge ndani ya Jimbo na miundombinu yetu hawezi kulalamika kuhusu hili. Gari imara kwa miaka 5 ni muhimu sana kwa Mbunge. Kwa wanaojua magari vizuri wanajua vizuri magari imara na mazuri kwa kazi za kisiasa zinauzwa shilingi ngapi. Vile vile Wabunge wa CHADEMA wasipochukua pesa hizi za magari itakuwa haina maana kwani Wabunge wa CHADEMA tuko 48 tu kati ya Wabunge 353 hivyo sisi tukikataa haitabadilisha chochote na badala yake pesa hizi zitaishia kwenye mikono ya wachache ambao hatutajua zimetumika vipi.Kuna msemo unasema ukisusa wenzio wala.Hoja ya msingi hapa ni kuwa Wabunge wa CHADEMA wapeleke hoja Bungeni ya Kupitia Upya Maslahi ya Wabunge ili kama kuna pesa zisizo na maana kwa mbunge basi ziondolewe kwa maslahi ya umma,hoja si kukataa milioni 90 kwa sasa.

La tano kwa upande wangu kwa kuwa mimi ni Mbunge maskini siwezi kuzipeleka Milioni 90 zote kwenye gari.Nitanunua gari la bei nzuri la kini lazima liwe imara na la kuvutia.Zingine zitafanya mambo ya msingi ndani ya Jimbo la Kilombero na mambo mengine madogo madogo.

Lasita mkubuke vile vile siku hizi hela imeshuka sana thamani Milioni 90 zinaisha ndani ya wiki moja na unaweza ukajikuta hakuna la maana ulilolifanya.

La mwisho kabisa hivi siku hizi ndio imekuwa mtindo wa kuwataja Zitto,Mnyika and Regia?Kuna Wabunge wengi sana humu Wanawake kwa Wanaume amabo ni wanachama tena wazuri tu isipokuwa hawatumii majina yao halisi.Ukija na taito yako ikataja jina la ujumla Wabunge utapata majibu mazuri toka kwao.Mkiwa very specific mnawabana wao wanaona kama hawahusiki hivyo hawatoi ushirikiano wa kutosha,sio lazima wajitaje majina yao sisi tunataka michango yao. Ni vizuri tukawa tunapanua wigo mpana wa kuruhusu Wabunge wengine wachangie kwa majina yao bandia.

Aluta Continua

Kutoka Miti Mirefu Mwanza
Regia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira

Umejibu hoja dada regia lakini wabunge wa viti maalum na wa kuteuliwa na rais nao wanahitaji magari hayo imara na mazuri? wao wanashughuli hizi za wabunge wa majimbo? au labda sijui kazi zao naomba kuelimishwa.
 
Huyu Apollnary either ni mbunge au baba yake ni mbunge au kwa namna yoyote anafaidi gari la mbunge. Unategemea mh mbunge atoke Kigoma kwa gari!! Ni wachache sana wanaotumia barabara kwenda bungeni. Kama ulishawahi kutembelea bungeni huwezi kuona magari sawa na idadi ya wabunge. Wabunge wetu wankwea pipa kwenda bungeni bana.

Kwa nini unatetea magari ya kifahari tu Rav 4 ina matatizo gani, mimi naona inafaa kabisa kwa vile umetolea mfano wa rav 4. Lakini zipo alternatives kibao.

Halafu swala la mishahara, kwa nini walipwe mishahara mikubwa hivyo?? Nasikia kila mh anakomba mil 12 kwa mwezi!! Kwa kazi ipi??. Huyu si mtendaji, ni mwanasiasa tu, na bado baada ya miaka 5 anakabidhiwa kiinua mgongo nacho ni kati ya 50 hadi 70mil, za nini hizi?? Na mtu huyu huyu kwenye uchaguzi unaofuata anashinda na kurudi mjengoni tena.

Mimi nadhani kiinua mgongo kilipwe kwa wale wabunge wanaoshindwa kurudi bungeni, kwa maana ya kushindwa kwa kura ama kwa kuamua kutogombea. Otherwise kwa wabunge waliokaa bungeni kwa vipindi 8 (Wajijua),wameshakula hivyo viinua mgongo bil ngapi. Wabunge wetu wafike mahala waache ULAFI.

Namkumbuka Dr Slaa enzi zake alipinga hoja ya wabunge kuongezewa mishahara na posho. Kwa waliofuatilia hiyo watakumbuka alivyosakamwa na wabunge wenzake. Oh anatoa siri za mishahara yetu, oh sijui nini, hakuungwa mkono na hoja ya kuongezewa mashahara na posho ilipita. Nasikia posho ya siku moja kwa kuingia na kulala/kusinzia au kupiga makofi yale ya kwenye meza au kwa kusema tu naunga mkono hoja asilimia mia kwa mia na ukaendelea kuuchapa usingizi inakaribia sh 200,000. Hao ndo wengi wa wabunge wetu.
 
Wakuu.Salaam.

Nimeona nichangia post hii kidogo.

Kwanza kabisa niweke rekodi sawa Fedha hizi za Gari hazijaanza kuigia kwa wiki tatu zilizopita kama mtoa mada alivyosema.Cheki zimeanza kutolewa kama siku nne au tatu zilizopita na zaidi ya asilimia 80 ya Wabunge bado hawajapata cheki zao,hata mimi bado sijapata.

La pili ni hili Milioni 90.Ifahamike kwamba Milioni hizi 90 wabunge hawapewi Bure tunakopeshwa na tunakatwa kupitia mishahara yetu.Bunge linalipa nusu ya pesa hizo yaani Milioni 45,Milioni 45 nyingine kila Mbunge anakatwa karibu shilingi 866,000 kwa mwezi kupitia mshahara wake.Kwahiyo Bunge linatoa shilingi Milioni 45 tu kwaajili ya gari.

La tatu Kimsingi Bunge limeweka Utaratibu ili kumsaidia Mbunge afanye vizuri kazi zake za Kibunge ilipendekezwa awe anatumia gari aina ya Toyota Hard Top Mpya ambayo kwa sasa gari hili linauzwa shiingi Milioni 112.Bunge likatafakari ikaonekana ni gharama kubwa kumpa kila Mbunge shilingi Milioni 112 hivyo busara ya wahusika wanaopanga maslahi ya wabunge wakaja na kiwango hiki cha Milioni 90 na Bunge kuchangia nusu ya pesa hizi. Bunge limependekeza aian hii ya gari kwakuwa ni imara inayoendana na miundumbinu ya majimbo mengi hapa nchini.Lakini kwa hali ilivyo watakao nunua ni wale wenye uwezo kipesa wengine trutakimbilia kwenye magari ya bei rahisi.

La nne ni mapendekezo ya baadhi ya watu eti wabunge wa CHADEMA wasichukue pesa hizo.Kimsingi hili sio pendekezo sahihi sasa wabunge hawa wa CHADEMA wasipochukua pesa hizi za gari nani atawanunulia magari ya kurahisisha kazi zao?hivi milioni 45 ni nyingi sana kwa kununua gari?kwa yeyote anayefahamu vizuri kazi ya Mbunge ndani ya Jimbo na miundombinu yetu hawezi kulalamika kuhusu hili. Gari imara kwa miaka 5 ni muhimu sana kwa Mbunge. Kwa wanaojua magari vizuri wanajua vizuri magari imara na mazuri kwa kazi za kisiasa zinauzwa shilingi ngapi. Vile vile Wabunge wa CHADEMA wasipochukua pesa hizi za magari itakuwa haina maana kwani Wabunge wa CHADEMA tuko 48 tu kati ya Wabunge 353 hivyo sisi tukikataa haitabadilisha chochote na badala yake pesa hizi zitaishia kwenye mikono ya wachache ambao hatutajua zimetumika vipi.Kuna msemo unasema ukisusa wenzio wala.Hoja ya msingi hapa ni kuwa Wabunge wa CHADEMA wapeleke hoja Bungeni ya Kupitia Upya Maslahi ya Wabunge ili kama kuna pesa zisizo na maana kwa mbunge basi ziondolewe kwa maslahi ya umma,hoja si kukataa milioni 90 kwa sasa.

La tano kwa upande wangu kwa kuwa mimi ni Mbunge maskini siwezi kuzipeleka Milioni 90 zote kwenye gari.Nitanunua gari la bei nzuri la kini lazima liwe imara na la kuvutia.Zingine zitafanya mambo ya msingi ndani ya Jimbo la Kilombero na mambo mengine madogo madogo.

Lasita mkubuke vile vile siku hizi hela imeshuka sana thamani Milioni 90 zinaisha ndani ya wiki moja na unaweza ukajikuta hakuna la maana ulilolifanya.

La mwisho kabisa hivi siku hizi ndio imekuwa mtindo wa kuwataja Zitto,Mnyika and Regia?Kuna Wabunge wengi sana humu Wanawake kwa Wanaume amabo ni wanachama tena wazuri tu isipokuwa hawatumii majina yao halisi.Ukija na taito yako ikataja jina la ujumla Wabunge utapata majibu mazuri toka kwao.Mkiwa very specific mnawabana wao wanaona kama hawahusiki hivyo hawatoi ushirikiano wa kutosha,sio lazima wajitaje majina yao sisi tunataka michango yao. Ni vizuri tukawa tunapanua wigo mpana wa kuruhusu Wabunge wengine wachangie kwa majina yao bandia.

Aluta Continua

Kutoka Miti Mirefu Mwanza
Regia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira

Ni kweli kabisa dada Regia,upo sawa! Msiwe kama Pinda aliyekataa V8 wakati mawaziri wake wote wamepewa maV8. La msingi ni kupeleka hio hoja bungeni ili mswada uwe sawa kwa wote.

Ni kweli sio vema kuwataja kwenye mada wabunge wachache ungali tunajua bunge letu lina wabunge 400 na zaidi hivi, kwani hao wengine walichaguliwa na nani? Na kwa maslahi ya nani?
 
Umejibu hoja dada regia lakini wabunge wa viti maalum na wa kuteuliwa na rais nao wanahitaji magari hayo imara na mazuri? wao wanashughuli hizi za wabunge wa majimbo? au labda sijui kazi zao naomba kuelimishwa.

Kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA Mbunge wa Viti Maalum anaanzia Wilayani kwake then unakwenda ngazi ya taifa na kupitishwa na vikao husika kwa kuomba kura kwa wajumbe wa vikao vyote hivi.Kwahiyo kama niliptia Wilayani kwangu hivyo ni wajibu wangu pia kutekeleza majukumu yaliyopo kwenye Wilaya yangu.Kanuni za kitaifa zimempa Mbunge wa Viti Maalum kutumikia Mkoa ndio maana utasikia Regia Mtema Mbunge Viti maalum toka Mkoa wa Morogoro.Mkoa Mmoja una Wilaya kati ya 4 mpaka 8 hivi unafikiri Mbunge huyu atafanyaje kazi?lazima awe na usafiri kwa kuwezeshwa na ofisi yake anayoitumikia.Wabunge wa Kuteuliwa na rais na wenyewe wanapewa majukumu katika kazi zao hivyo lazima wawe na nyenzo za kuwarahishia kazi. Mimi Kama Mbunge wa Viti Maalum natumikia Mkoa Mzima wa Morogoro. Unajua jinsi Morogoro ilivyokubwa na miundo mbinu ilivyomibovu,tunahitaji magari imara.
 
Tumeshaona mifano ya Mil. 90 kwa jinsi wabunge wa chadema wanavyozitumia kwa wa vitendo. Huku Arusha sisi hatuna questions kuhusu hizo hela. juzi juzi tu mheshimiwa Lema mbunge wetu kijana mchapakazi kwa vitendo kazindua mfuko maalum kwa kutumia pesa hizo, hasa kuwasomesha watoto wa wazazi wasio na uwezo kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa elimu yao. siku ya kwanza tu, watoto 416 walijiandikisha na wamepewa mahitaji yao yote, huu ni mfano wakuigwa ndg zangu.
Lema ametuonyesha, Lema ametukumbusha.

Ee Mwenyenzi Mungu wa Mbinguni Umbariki Mbunge Wetu Godbless Jonathan Lema, Umpe Ulinzi wako, maana tunajua wewe ni mtakatifu na wewe ndiye mungu wetu wa kweli uishiye milele, Umwepushe na Maadui wasije kumdhuru, kama ulivyomlinda Samweli asiliwe na simba wakali. Amen!
 
Kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA Mbunge wa Viti Maalum anaanzia Wilayani kwake then unakwenda ngazi ya taifa na kupitishwa na vikao husika kwa kuomba kura kwa wajumbe wa vikao vyote hivi.Kwahiyo kama niliptia Wilayani kwangu hivyo ni wajibu wangu pia kutekeleza majukumu yaliyopo kwenye Wilaya yangu.Kanuni za kitaifa zimempa Mbunge wa Viti Maalum kutumikia Mkoa ndio maana utasikia Regia Mtema Mbunge Viti maalum toka Mkoa wa Morogoro.Mkoa Mmoja una Wilaya kati ya 4 mpaka 8 hivi unafikiri Mbunge huyu atafanyaje kazi?lazima awe na usafiri kwa kuwezeshwa na ofisi yake anayoitumikia.Wabunge wa Kuteuliwa na rais na wenyewe wanapewa majukumu katika kazi zao hivyo lazima wawe na nyenzo za kuwarahishia kazi. Mimi Kama Mbunge wa Viti Maalum natumikia Mkoa Mzima wa Morogoro. Unajua jinsi Morogoro ilivyokubwa na miundo mbinu ilivyomibovu,tunahitaji magari imara.
Nimekuelewa Dada Regia, watumikie wananchi wa Morogoro na watanzania kwa ujumla, Mungu atakubariki.
 
Kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA Mbunge wa Viti Maalum anaanzia Wilayani kwake then unakwenda ngazi ya taifa na kupitishwa na vikao husika kwa kuomba kura kwa wajumbe wa vikao vyote hivi.Kwahiyo kama niliptia Wilayani kwangu hivyo ni wajibu wangu pia kutekeleza majukumu yaliyopo kwenye Wilaya yangu.Kanuni za kitaifa zimempa Mbunge wa Viti Maalum kutumikia Mkoa ndio maana utasikia Regia Mtema Mbunge Viti maalum toka Mkoa wa Morogoro.Mkoa Mmoja una Wilaya kati ya 4 mpaka 8 hivi unafikiri Mbunge huyu atafanyaje kazi?lazima awe na usafiri kwa kuwezeshwa na ofisi yake anayoitumikia.Wabunge wa Kuteuliwa na rais na wenyewe wanapewa majukumu katika kazi zao hivyo lazima wawe na nyenzo za kuwarahishia kazi. Mimi Kama Mbunge wa Viti Maalum natumikia Mkoa Mzima wa Morogoro. Unajua jinsi Morogoro ilivyokubwa na miundo mbinu ilivyomibovu,tunahitaji magari imara.


Dada Regia nakuunga mkono 100% kwa kweli kazi wanazofanya wabunge wa viti maalum ni kubwa sana ukilinganisha na wabunge wa kuchaguliwa, ambao kwa sehemu kubwa wanashughulika na majimbo yao ya uchaguzi.
Hongera, endelea na moyo huo wa kuwatumikia wananchi wa mkoa wako, bila kusahau jimbo la kilombero, na kwa neema ya mungu utakuwa mbunge wa jimbo la kilombero 2015, mteketa akatafute shughuli ya kufanya.
Naamini kuwa wewe ni moja wa wanawake wachache jasiri nchi hii, endelea kuwaamsha na wengine waliolala, wanaoridhika na khanga pea moja itakayowagharimu maisha kwa muda wa miaka 5.

I support kilombero for change dada Regia! this change is very near!
 
HII MADA KICHAA KABISA,YAANI WAKATAE HELA ILI CCM WACHUKUE ZOTE??AU ILI WASHINDWE KUFIKA KIJIJINI ILI CCM WAFIKE NA WAENDELEE KUWADANGANYA WATANZANIA??HII NI NAFASI NA LAZIMA WAITUMIE

USHAURI WANGU;;

CHADEMA CHUKUENI HELA ZOTE MNAZOPEWA NA CCM,KAMA NI MAGARI CHUKUENI ,KAMA NI POSHO CHUKUENI KWA SANA,KAMA NI RUZUKU OMBENI IONGEZWE HAITOSHI ILA ;;NARUDIA TENA ILA;;FANYENI KAZI KWELI KWELI HIZO HELA ZIWE NYENZO MUHIMU YA KUWAFIKISHA KILA MAHALI NA KUELEZA UKWELI KILA KONA YA NCHI HII,VIONGOZI WETU WAENDE NA NJE YA NCHI MKAELEZE UKWELI HUKO,MKASOME AMBAO ELIMU SIO YA JUU SANA MJIONGEZEE ELIMU,MJENGE NYUMBA NI AIBU MBUNGE UNAKAA NYUMBA YA KUPANGA,MNUNUE MAGARI MAZURI IMARA YATAKAYOWAFIKISHA NCHI NZIMA

ushauri wangu ,Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom