Redio zenu siku hizi ni sawa na kusikiliza maongezi ya vijiweni

OLS

JF-Expert Member
Oct 12, 2019
419
670
Utangazaji wa sasa ni kama unasikiliza majibizano ya vijiweni. Mbali na watangazaji kutojipanga ila mara nyingi wamekuwa wakiongea wao kwa wao huko studio, mara nyingine wanajisahau kuwa kuna watu wanawasikiliza

Yaani unakuta wanaongelea suala la msingi lakini wanaweka mambo mepesi sana katika masuala hayo, Redio zoe zinakuwa kama zipo kwenye kupotosha au kiudaku zaidi kuliko kuhabarisha na kuelimisha

Ofcourse burudani ni muhimu lakini kupitia burudani inabidi kuwe na elimu humo kwa humo. sio burudani tu muda wote

Pia wengine hudhihirisha ujinga wao kwa kuongelea mambo ambayo hata hawayajui au hawajayatafiti kabla ya kwenda kuyazungumza redioni. Unasikiliza redio kama unasikiliza vijana walioko kwenye kijiwe cha kahawa au kwenye maeneo ya kubeti wakiwa wanabishana wampe nani wamuue nani

Kwa kusema haya wala sishadadii suala la serikali kutaka vijana wote wawe ni wale waliosoma masuala ya habari. Bali naamini katika ule mtindo wa Kimarekani, kwamba mtu anasomea kitu fulani kama masuala ya watoto, halafu anasoma habari ili atoe elimu kuhusu masuala ya watoto

Huo ndio muarobaini wa kufanya watu wasitangaze vipindi kama wako vijiweni. Anasema kuwa na Astashahada, Stashahada au shahada ya habari haitoshi kumfanya mtu kuwa mtaalamu wa jambo analolizungumza

Signed

Oedipus
 
Kuna kizazai tunapata shida sana kusikiliza hizi redio,Ikifika saa nane mchana mpaka saa kumi kama si mpenzi wa bongo fleva itakubidi tu uzime radio, ni muziki kila radio , bahati mbaya nyimbo zinazochezwa ni zilezile,mpaka unajiuliza kwanini wote wamechagua kipindi cha aina moja na muda ule ule,bahati mbaya hata TBC taifa imefuata mtindo huo huo.Sikiliza ijumaa na jumamosi kuanzia saa tatu usiku vipindi ni muziki tu redio zote.Watangazaji sasa, kuna mada wanazianzisha na hawana weledi nazo, ndipo sasa wataishia kupgishana story humo huku wakidanganya.
 
Kuna kizazai tunapata shida sana kusikiliza hizi redio,Ikifika saa nane mchana mpaka saa kumi kama si mpenzi wa bongo fleva itakubidi tu uzime radio, ni muziki kila radio , bahati mbaya nyimbo zinazochezwa ni zilezile,mpaka unajiuliza kwanini wote wamechagua kipindi cha aina moja na muda ule ule,bahati mbaya hata TBC taifa imefuata mtindo huo huo.Sikiliza ijumaa na jumamosi kuanzia saa tatu usiku vipindi ni muziki tu redio zote.Watangazaji sasa, kuna mada wanazianzisha na hawana weledi nazo, ndipo sasa wataishia kupgishana story humo huku wakidanganya.
Nimewaza kuiuza hii redio kwa negative price,ili nisiendelee kusikiliza hizi redio. Kama taarifa nitapata mtandaoni tena kwenye sites zinazojielewa
 
mfano RFA kipindi cha Showtime. Ni uharooooooo. wajirekebishe.
 
Redio zote utupolo tu, muhimu matangazo ndo kitu hawasahau... ni kama wanapiga stori ili kusubiri muda wa-play tangazo.
 
Hizi media karibia zote tu zina shida kubwa.
IMG_20200426_203416.jpeg
IMG_20200426_203148.jpeg
IMG_20200426_202732.jpeg
IMG_20200426_202608.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom