CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 6,087
- 5,352
Umasikini wa chakula umepungua kutoka 21.6% hadi 8.0%hii inamaanisha kwenye kila watanzania 100 ni 8 tu ndio wanashida ya mlokamili tunaposema CCM na Rais Samia wanachapa kazi muwe mnatuelewa,Benki ya Dunia sio CCM.
Hata kama mnapiga kelele ila mfahamu umasikini wa msosi Tanzania kwa mujibu wa Benki ya Dunia umeshuka sana chini ya CCM na Rais Samia.
Rais Samia kwa upande wa kumpiga vita adui UMASIKINI, Taifa limepiga hatua kubwa, ambapo takwimu rasmi zinaonesha kuwa kati ya mwaka 1991 na 2018, umasikini umepungua.
Mathalani katika kipindi hicho cha marejeo, asilimia ya watu waliokuwa wakiishi katika umasikini wa hali ya juu (umasikini wa chakula) ilipungua kwa kiasi kikubwa kutoka asilimia 21.6 hadi asilimia 8.0
Wakati huo huo kiwango cha umasikini wa mahitaji ya msingi kikishuka kutoka asilimia 38.6 hadi asilimia 26.4.