Recategorization baada ya kuajiriwa serikalini

Recategorization baada ya kuajiriwa serikalini

MZIBHAZI

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
520
Reaction score
139
Jamani,

Mimi naomba kufaham hivi kufanyiwa recategorization kazini wanafanyaje mimi nimeajiriwa kama Mwalimu lakini sina teaching subjects za Sekondari sasa.

Je kuna namna ya kufanya recategorization kwenye halmashauri husika?
 
@MZIBHAZ

Sasa umeajiriwa vipi kama mwalimu huku huna teaching subjects.
 
Sasa umeajiriwa vipi kama mwalimu huku huna teaching subjects.

mimi ni mwalimu wa primary bagamoyo nataka kuhamia uhasibu maaana nilisoma accounts level ya degree je barua ya recategorization ipite kwa nani kati ya afisa elimu,mkurugenz au afisa utumish
 
Fafanua vzr tukuelekeze

mimi nimesoma bed psychology sina teaching subject sekondari nilipangiwa kazi halmashauru X kama mwalimu wapsychology na sasa wananipa somo wakat mimi sina somo la sekondari nilitakiwa kwende kufundisha vyuo vya ualimu na kufanya kazi zingine maana nimesoma content nying sana sasa ndio naomba ufafanuzi wenu
 
mimi ni mwalimu wa primary bagamoyo nataka kuhamia uhasibu maaana nilisoma accounts level ya degree je barua ya recategorization ipite kwa nani kati ya afisa elimu,mkurugenz au afisa utumish

Nadhan atakua kwa afisa utumishi mkuu maana hapo unaachana na afisa Elimu any way subiri wanafahamu wakuelekeze
 
MZIBHAZI

Nakushaur kubali ufundishe kwanza masomo uliyosoma a level at least a year ili upate barua ya kudhibitishwa kazin then ndo uanze process hizo kupitia kwa afisa utumishi wa wilaya mambo mengine ya kufanya atakuelekeza yeye.kila la kheri
 
Last edited by a moderator:
Taratibu za UTUMISHI ni kwamba ukienda kujiendeleza katika kada ambayo Si Ualimu elimu uliyosomea haitakupa sifa ya kupanda cheo, Na kuhusu kubadilishiwa kazi Hilo jukumu atafanya mwajiri wako akiona Ana ikama katika eneo ulilojiendeleza.
 
mimi ni mwalimu wa primary bagamoyo nataka kuhamia uhasibu maaana nilisoma accounts level ya degree je barua ya recategorization ipite kwa nani kati ya afisa elimu,mkurugenz au afisa utumish

Mwajiri wako ni mkurugenzi ila barua yako itapitia kwa m/ mkuu then afisa elimu kwenda kwa mkurugenzi
 
mimi ni mwalimu wa primary bagamoyo nataka kuhamia uhasibu maaana nilisoma accounts level ya degree je barua ya recategorization ipite kwa nani kati ya afisa elimu,mkurugenz au afisa utumish
Andika barua ya maombi kwenda kwa mkurugenzi kupitia kwa mkuu wako wa idara ambae ni afisa elimu unaweza pia kuipitisha kwa mkuu wa idara na afisa utumishi wakishasaini ndo inakwenda kwa mkurugenzi wa halmashauri
 
Ni vema kwa unaefahamu taratibu na pengine hata ukaweka sample ya baruua hapa ingemsaidia ukizingatia barua nyingi za kiofisi kwenye hizi ofisi za halmashauri wanataka zitumie lugha ya Taifa yaani kishwahili.

Mfano Yah: .......................
 
Andika barua ya maombi kwenda kwa mkurugenzi kupitia kwa mkuu wako wa idara ambae ni afisa elimu unaweza pia kuipitisha kwa mkuu wa idara na afisa utumishi wakishasaini ndo inakwenda kwa mkurugenzi wa halmashauri

sasa hapo umenichanganyakidogo maana barua ni moja ila unaandika anuani zaid yamoja sasa nataka mfuatano mzuri mfano mkurugenz kk afisaelim kk afisa utumish then yah: sasa hapo huu nani anaanza nani anafuata
 
Nakushaur kubali ufundishe kwanza masomo uliyosoma a level at least a year ili upate barua ya kudhibitishwa kazin then ndo uanze process hizo kupitia kwa afisa utumishi wa wilaya mambo mengine ya kufanya atakuelekeza yeye.kila la kheri

Asante sana mkuu kwa ushaurii wako sasa baada ya hapo ukithibitishwa unaweza kwenda kufanya kazi gani halmashauri??tofautu na kufundisha vyuoni?
 
sasa hapo umenichanganyakidogo maana barua ni moja ila unaandika anuani zaid yamoja sasa nataka mfuatano mzuri mfano mkurugenz kk afisaelim kk afisa utumish then yah: sasa hapo huu nani anaanza nani anafuata

Afisa utumishi anafanyakazi kwa niaba ya mkurugenzi hivyo hakuna barua hata moja ya kikazi halmashauri inayopitia kwake
 
sasa hapo umenichanganyakidogo maana barua ni moja ila unaandika anuani zaid yamoja sasa nataka mfuatano mzuri mfano mkurugenz kk afisaelim kk afisa utumish then yah: sasa hapo huu nani anaanza nani anafuata

Adress:

Mkurugenzi

Kk Afisa elimu
Kk mkuu/ shule

Hay: maombi ya kubadilishiwa Kazi ( recategorisation) baada ya kijiendeleza
 
sasa hapo umenichanganyakidogo maana barua ni moja ila unaandika anuani zaid yamoja sasa nataka mfuatano mzuri mfano mkurugenz kk afisaelim kk afisa utumish then yah: sasa hapo huu nani anaanza nani anafuata
inaanza mkurugenzi then kk afisa utumishi kk mkuu wa idara
 
inaanza mkurugenzi then kk afisa utumishi kk mkuu wa idara

Mkúu nadhani haiko sahihi kwani afisa utumishi hana nafasi yeye anafanyakazi ya kupewa na mkurugenzi. Mf: mkurugenzi kk afisa elimu kk m/mkuu. Ikifika kwa mkurugenzi ataisaini mwenyewe au atampatia afisa utumishi.
 
Mkúu nadhani haiko sahihi kwani afisa utumishi hana nafasi yeye anafanyakazi ya kupewa na mkurugenzi. Mf: mkurugenzi kk afisa elimu kk m/mkuu. Ikifika kwa mkurugenzi ataisaini mwenyewe au atampatia afisa utumishi.

Uko sahihi kabisa, huwezi kuadress barua kwa Afisa Utumishi. Anaweza kusaini kwa niaba ya Mkurugenzi.
 
Adress:

Mkurugenzi

Kk Afisa elimu
Kk mkuu/ shule

Hay: maombi ya kubadilishiwa Kazi ( recategorisation) baada ya kijiendeleza

Yaani vijana siku hizi hata kuandika barua hamfundishwi??

Aise Elimu ya Tanzania sijui inaelekea wapi!!

NB: Natumaini mleta mada atasaidiwa kupata ufumbuzi wa tatizo lake.
 
Yaani vijana siku hizi hata kuandika barua hamfundishwi??

Aise Elimu ya Tanzania sijui inaelekea wapi!!

NB: Natumaini mleta mada atasaidiwa kupata ufumbuzi wa tatizo lake.

Masanja samahani,
Inaandikwaje labda
 
Back
Top Bottom