Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Hii game kama tulicheza kipindi cha kwanza kama tulivyocheza cha pili, ingekuwa imeisha mapema sana, shida tuliwapa nafasi Sevilla yakuona na wao wana uwezo wa kushinda,
Courtois kama kawaida Save yake ya mwisho ndio imetupatia ushindi, Militao hajafanikiwa kufunga ila goli zote mbili mipira ilitokea kwake.,
Huu ni ushindi muhimu sana ukizingatia tuna game ngumu zaidi zinazofuata.,
#HalaMadrid
 
Ili li timu linazidi kuchana mawimbi huku laliga sina hofu napo. Changamoto iko ukikutana na miamba huko uefa ndio inaweza tufanya kitu mbaya
Huko Uefa sio shida sana, kwasababu ukikutana na wakubwa wenzio hawatakuwa na shida ya kupack basi, zaidi itakuwa ni nani amemzidi mwenzie mbinu.,
Sasa huku La Liga ndio panakuwa pagumu, unakutana na Granada huko jamaa kuanzia game inaanza mpaka inaisha wapo golini kwao tu, hapo hata ufundi huwa unaisha.
 
Huko Uefa sio shida sana, kwasababu ukikutana na wakubwa wenzio hawatakuwa na shida ya kupack basi, zaidi itakuwa ni nani amemzidi mwenzie mbinu.,
Sasa huku La Liga ndio panakuwa pagumu, unakutana na Granada huko jamaa kuanzia game inaanza mpaka inaisha wapo golini kwao tu, hapo hata ufundi huwa unaisha.

Tusubiri hatua zinazofuata
 
1638386175477.png
 
Real Madrid's starting line-up (4-3-3): Thibaut Courtois; Dani Carvajal, Eder Militao, David Alaba, Ferland Mendy; Toni Kroos, Casemiro, Luka Modric; Rodrygo Goes, Karim Benzema, Vinicius Junior
 
Ni siku nyingine tena, na LA Liga inaendelea, Leo tupo ugenini dhidi ya Real Sociedad, line up ni kama ilivyo hapo juu., mabadiliko ni kidogo tu, na hii ndio huwa ninaamini ndio kikosi chetu rasmi.,
 
Hatukuwa na kipindi cha kwanza kizuri, team haijacheza vizuri, jamaa wametulia kweli kweli, na kiungo wapo Wanne so Luka na Toni hawatoshi kuwadhibiti, ingekuwa vema wakati Benzema ametoka angeingia. Either Camavinga ama Valverde, hiyo sub ingetusaidia kuweka mambo Sawa pale kati.,
Bahati mbaya ameingia Jović, shida ni kwamba kijana hana match fitness, sijui ni kwasababu imekuwa haraka sana ama laa, acha tuone kipindi cha pili kama atachangamka.,
Ila so far La Real wamekuwa na kipindi cha kwanza kizuri.
 
Ninaona hawa wachezaji wa Real Sociedad mpira umewashinda sasa wana kazi ya kumtafutia Casemiro kadi ya njano ili mechi inayofuata asicheze
 
Back
Top Bottom