Mphamvu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 10,702
- 3,288
Sio mbaya nikitoa ilmu kidogo.
Watu huwa wanashindwa kutofautisha matusi na maneno ambayo kwa kizungu huiwa 'taboo words', sifahamu Kiswahili chake. Kwa kizungu, matusi huweza kufasiriwa kama 'insults' au 'abusive language/words' na 'taboo words' ni maneno ambayo hayawezi kutamkwa hadharani kwa kuwa yanagusa faragha za watu, mfano maungo ya siri ya binadamu. Kwa fasili za namna hii, tunaona kuwa tusi ni dhana ya kiuamilifu zaidi, yaani ni mpaka lipewe kazi maalumu, nayo ni kukejeli, kudhalilisha au kulenga faragha za mhusika kwa namna isiyopendeza. Haya ambayo tunadai kuwa ni matusi ni sehemu ya leksikoni (jumla ya msamiati wote katika lugha) yetu, na ni haki yetu kuyatumia bila kulenga 'abuses' kwa yeyote.
Sawasawa?
Pia kuna maneno ambayo si 'taboo language/words' lakini yakipangwa vema yanaweza kutumika kama 'insults', mfano, kishazi "...unapakuliwa kisamvu cha kopo.", hakuna 'taboo word' hapo, lakini kishazi chenyewe ni 'insult' ya hali ya juu. Mfano mwingine ni neno 'fu.ck' katika Kiingereza cha Amerika, neno hili linaweza kutumika kama 'insult' au kama neno la kawaida. Tizama uamilifu wake katika "...**** you!" na "...this government ****s big time!"
Kwa leo nikomee hapo, halafu tutizame upya tafauti hizi.
Wakatabahu,
Mphamvu Letsholonyane!
Watu huwa wanashindwa kutofautisha matusi na maneno ambayo kwa kizungu huiwa 'taboo words', sifahamu Kiswahili chake. Kwa kizungu, matusi huweza kufasiriwa kama 'insults' au 'abusive language/words' na 'taboo words' ni maneno ambayo hayawezi kutamkwa hadharani kwa kuwa yanagusa faragha za watu, mfano maungo ya siri ya binadamu. Kwa fasili za namna hii, tunaona kuwa tusi ni dhana ya kiuamilifu zaidi, yaani ni mpaka lipewe kazi maalumu, nayo ni kukejeli, kudhalilisha au kulenga faragha za mhusika kwa namna isiyopendeza. Haya ambayo tunadai kuwa ni matusi ni sehemu ya leksikoni (jumla ya msamiati wote katika lugha) yetu, na ni haki yetu kuyatumia bila kulenga 'abuses' kwa yeyote.
Sawasawa?
Pia kuna maneno ambayo si 'taboo language/words' lakini yakipangwa vema yanaweza kutumika kama 'insults', mfano, kishazi "...unapakuliwa kisamvu cha kopo.", hakuna 'taboo word' hapo, lakini kishazi chenyewe ni 'insult' ya hali ya juu. Mfano mwingine ni neno 'fu.ck' katika Kiingereza cha Amerika, neno hili linaweza kutumika kama 'insult' au kama neno la kawaida. Tizama uamilifu wake katika "...**** you!" na "...this government ****s big time!"
Kwa leo nikomee hapo, halafu tutizame upya tafauti hizi.
Wakatabahu,
Mphamvu Letsholonyane!