Akutukanae, hakuchagulii tusi

Akutukanae, hakuchagulii tusi

Mkandara

Platinum Member
Joined
Mar 3, 2006
Posts
15,961
Reaction score
9,345
Nimekuwa nikifuatilia mijadala mingi inayoendelea nchini kuhusu Utanganyika na Uzanzibar kiasi kwamba sasa mijadala hiyo imeingia kwenye Muungano wenyewe!

Madai ya mwanzo kabisa ilikuwa kutaka muundo wa Muungano wetu uwe wa Shirikisho (Federal Union) Serikali 3, badala ya huu uliopo wa NCHI moja (Unitary State) Serikali2 na walijenga hoja zao kwa kufuata mfumo wa Shirikisho iilihali huo sio mfumo wetu. Inawezekana hawakujua kwamba Muungano wetu wa mwaka 1964 haukuwa wa Shirikisho kama walivyo aminishwa.

Hata hivyo, binafsi nimekuwa nikipingana na mawazo yao nikiamini kwa dhati kabisa hsamira yao haikuwa njema, mwisho wa siku patakuwa hakuna Muungano kwa sababu madai ya Serikali 3 ni lugha ya kistaarabu au kiungwana iliyotumiwa Kuficha dhamira yao ya kweli. Na sasa hivi wamechoka kujificha nyuma ya pazia la Muungano.

Namshukuru Mwenyezi Mungu, kuwasikia sasa hivi wakifunguka wazi kanisa kwa madaha wakidai kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar haukuwa Halali toka uliposainiwa mwaka 1964.

Tena baadhi viongozi wanasema wazi wazi kuwa Muungano ule Baraza la Malinduzi walilazimishwa kuukubali lakini haukupata ridhaa yao. Sijui hawa pia walikuwa katika Baraza lile Mpinduzi la kwanza lenhe wajumbe 29 ama nao walihadithiwa.

Kifupi, Haya ni matusi mazito sana kwa Taifa letu nanhasa katika jamii ambayo tumeishi zaidi ya miaka 60 tukiamini sisi wote ni Watanzania.
Kumbe nyuma ya pazia, kuna wale wanaodai Serikali 3 ndio wao wasoutambua Muungano.

Ukisikia Wazanzibar wanadai NCHI yao na Watanganyika wanadai NCHI yao. Muungano haramu hauwezi kuunda Serikali ya Shirikisho kwenye Muungano Haramu.

Kama hutuutambui Muungano, tunawezaje kuunda Serikali zozote ndani ya Muungano usotambuliwa? Kama hutuutambui Muungano wetu wala hauna ridhaa yetu, tunataka Serikali 3 za kitu gani?

Namshukuru Mungu wachawi wameanza kutua juu ya paa mchana kweupe. Na kibaya zaidi zile sifa za KiongoI tumtakae, alizosema Mwalimu mwaka 1995 kabla ya Uchaguzi Mkuu wa Chama chake zimebakia kuwa hadithi nyingine ndani ya Kitabu.

Tuliombee taifa letu, aidha maneno ya Mwalimu yametimia, tunasubiri Utabiri wa Sheikh Yahya Hussein.

Masalaam
 
Maamuzi magumu hayahitaji vikao....🫤
20260612_141140.jpg
 
Kwa sasa nikiona Mzenji anatetea muungano namuelewa, maana wao wanafaidi pesa na raslimali za Tanganyika, nk. Hata waziri wa fedha wameweka Mzenji mwenzao kabisa.

Ila kwa Mtanganyika kutetea huo muungano, duh. Laana ya uchawa is real
Funguka yalokuwa moyoni mwako siku zooote, ndio picha ninayoiweka hapa..
 
Serikali tatu ni ngumu,maana hapo rais wa Tanzania atamezwa na rais wa Tanganyika,hapo ili muungano unoge zaidi lazima serikali moja iwe,ila kwa ninavyowafahamu wazenji, sdhani kama watakubali serikali ya mapinduzi ya z'bar ibomolewe.
 
Funguka yalokuwa moyoni mwako siku zooote, ndio picha ninayoiweka hapa..
Siyo ya moyoni mkuu, tunaongelea uhalisia. Nchi ya Tanganyika/shamba la Bibi inapukutishwa waziwazi na haina mtetezi...

Bajeti ya Tanzania (Raia 65M) ni Trilion 31, ya Zanzibar ni 8.5Trilion (Raia 1.3M) wakati huo huo wa Zanzibar wanahesabika tena kwenye Tanzania | JamiiForums Tanzania Bajeti ya Tanzania (Raia 65M) ni Trilion 31, ya Zanzibar ni 8.5Trilion (Raia 1.3M) wakati huo huo wa Zanzibar wanahesabika tena kwenye Tanzania
 
Serikali tatu ni ngumu,maana hapo rais wa Tanzania atamezwa na rais wa Tanganyika,hapo ili muungano unoge zaidi lazima serikali moja iwe,ila kwa ninavyowafahamu wazenji, sdhani kama watakubali serikali ya mapinduzi ya z'bar ibomolewe.
Kama watu hawautambui Muungano mnaunda Serikali za nini?
 
Siyo ya moyoni mkuu, tunaongelea uhalisia. Nchi ya Tanganyika/shamba la Bibi inapukutishwa waziwazi na haina mtetezi...

Bajeti ya Tanzania (Raia 65M) ni Trilion 31, ya Zanzibar ni 8.5Trilion (Raia 1.3M) wakati huo huo wa Zanzibar wanahesabika tena kwenye Tanzania | JamiiForums Tanzania Bajeti ya Tanzania (Raia 65M) ni Trilion 31, ya Zanzibar ni 8.5Trilion (Raia 1.3M) wakati huo huo wa Zanzibar wanahesabika tena kwenye Tanzania
Sasa mkuu wangu ugumu wa hesabu uko wapi? Bajeti ni makadirio ya matumizi kwa mwaka. Hata sisi tunakadiria tril. 31 tuaipozipata kwankodi zetu tunaomba nchi za nje!

Bajeti ya Zanzibar kama ni tril.8 na hawakukisanya wataomba Serikali Kuu, iwe imetokana ma fedha za ndani au Mikopo.

Na tunaweza kukopa tril.10 zote zikatumika upande mmoja, tena labda mkoa mmoja! Kama leo unalalamikia Zanzibar kesho itakuwa Dodoma au reli ya SGR ina manufaa gani kwa mtu wa Mtwara wakati gas na Korosho zake mmeuza nje!
 
Nia ni kurekebisha kasoro nyingi zilizopo. Au mnataka kasoro na kero lukuki ziendelee kutamalaki??

(4) Tetesi: - Inadaiwa 69% ya wakurugenzi wa wilaya bara ni kutoka Zanzibar | JamiiForums Tanzania Tetesi: - Inadaiwa 69% ya wakurugenzi wa wilaya bara ni kutoka Zanzibar
So what? Ni Watanzania au kumbe sio na Muungano haupo? Kosa lingekuwa waajiriwa hawana sifa za kuongoza ama kushika madaraka hayo kwa upendeleo.

Kumbuka wakati wa Magufuli mlidai Viongozi wengi walopewa nafasi wanatoka Kanda ya Ziwa mkawapachika jina 'Sukuma gang' Au mmeshasahau?

Wenye tatizo na Ubaguzi ni nyie mnaotazama watu kwa dini, kabila au Ukanda sababu zenu zikidhi tafsiri ya Upendeleo. Na sisemi Wabara ni nyote baina yenu Watanganyika na Wazanzibar.
 
Kwa ujumla, kwa mambo yanayofanyika sasa, ya kuitumia Tanganyika kwaajili ya kuinufaisha Zanzibar, na kuwafanya Watanganyika hawana akili, kama wanavyosema wenyewe Wazanzibari kuwa Tanganyika ni kubwa jinga, kuutetea muungano wa aina hii ni lazima uwe shetani, lazima uwe mwendawazimu.
Fikiria mambo ya ushetani mkubwa yanayoendele sasa: mikopo ya mamia ya mabilioni inachukuliwa na JMT, pesa inapelekwa Zanzibar, halafu wa kulipa ni Tanganyika. Kwa dharau kubwa, na bila aibu, wamethubutu kumweka mzanzibari kuwa waziri wa fedha, wakati wizara ya fedha siyo ya muungano. Kwenye mambo ya fedha, kilicho cha muungano ni benki kuu na sarafu, basi. Kwa sasa, Wazanzibari wamejazwa kwenye nafasi za uongozi Tanganyika kwenye mambo ya Tanganyika, mambo yasiyo ya muungano, huko kanda ya ziwa wazanzibari wamechukua mamia ya leseni za madini, huko Nyanda za juu wamechukua maelfu ya ekari za ardhi.
Huu uharamia wote unasababishwa na CCM. CCM kwa sasa ndiyo adui namba 1 wa Tanganyika.
 
So what? Ni Watanzania au kumbe sio na Muungano haupo? Kosa lingekuwa waajiriwa hawana sifa za kuongoza ama kushika madaraka hayo kwa upendeleo.

Kumbuka wakati wa Magufuli mlidai Viongozi wengi walopewa nafasi wanatoka Kanda ya Ziwa mkawapachika jina 'Sukuma gang' Au mmeshasahau?

Wenye tatizo na Ubaguzi ni nyie mnaotazama watu kwa dini, kabila au Ukanda sababu zenu zikidhi tafsiri ya Upendeleo. Na sisemi Wabara ni nyote baina yenu Watanganyika na Wazanzibar.

Rudi kwenye uelewa, wakati unaundwa huo muungano, tuliungana kwenye mambo 17 tu, baadaye yameongezeka mpaka 21 tu. Hivyo kwenye mambo au wizara ambazo siyo za muungano, kila upande ushughulike wenyewe. Kuwaweka Wazanzibari kwenye mambo yasiyo ya muungano, ni ujuha ambao hakuna mwenye akili timamu anaweza kukubali. Tanganyika haina uhaba wa watu mpaka ikahitaji mzanzibari kwenye mambo yasiyo ya muungano. Hao wazanzibari kwenye mambo gasiyo ya muungano, ndio wanaosimamia uporwaji wa rasilimali za Tanganyika kwa faida ya wazanzibari. Kama wanataka waingie kila eneo la Tanganyika, wakubali muungano wa Serikali moja. Hapo hakutakuwa na mipaka ya rasilimali wala uongozi au ajira kwa ujumla.
 
Wanaoutetea muungano ni wanufaika wa huo muungano.
Uharamu wa muungano ulianzia pale wazenji walipoamua kuwa na serikali yao na ndipo Tanganyika tulianza kupigwa
Sijui nyie mnaojiona mnaakili hamkuliona hili. Hawa Wazenji hata watimiziwe nini hawatalizika nadhani inasababishwa na dini pia kupenda ugomvi.
 
Back
Top Bottom