RC wa Iringa kafanya madudu gani?

RC wa Iringa kafanya madudu gani?

Watoto wachanga na wazee wenye hela wasiotaka usumbufu hata Muhimbili wanalipia huo utaratibu ni wa kawaida sana. Ingekuwa analipishwa mtoto aliyepewa rufaa kutoka Flerimo kwenda regional hospital hapo ndio ningekubaliana na Hapi. Nilichokiona hapo ni siasa za kuviziana na hii inaweza kumjenga Msigwa badala ya kumbomoa. Nimpongeze Waziri Jaffo katika hili!
Hivi kumbe lengo ni kumbomoa Msigwa?? Tanzania kuna viongozi "wapumbavu" kuliko India.
 
Hii ndio ile habari ya wakati ule alipowaadhibu kwa kujipangia tozo kwa kinamama mpaka watoto wengine wakafa kwa kukosa hela? Wakati ni bure kwa kila mtoto?

Au ni kisa kingine hiki
 
Kosa la Hapi ni kumuaibisha daktari hadharani. Kimaadili angeitisha mkutano na viongozi wa afya mkoa. Pale angewaahidi tu wanchi kulishughulikia swala hilo.
mzee wa chato atajuaje amefanya kazi?
atapata makofi ya wananchi saa ngapi?
cheo atapanda lini akifanya kwa mtindo huo?

hawa na aliewachagua akili zao sawa kabisa.
 
Ukiangalia hiyo video hapo juu utagundua kuwa HAPI hana kosa lolote

Kosa analo na amefanya makusudi ili apate platform ya kisiasa. Ni kwamba hospital ya rufaa ukienda bila kuwa na barua ya rufaa unalipa pesa kama kawaida
 
Jambo usilolijua. Ni hospital ya rufaa ya mkoa. Mtu ana ugonjwa unaotibika zahanati ya mkimbizi, ila anakuja hospital ya mkoa. Msongamano, watumishi kuelemewa, kupungua ubora wa huduma n.k.
Underfives, wajawazito na wazee yes inatajwa watibiwe bila kulipia ila kwa kufuata utaratibu.

Hospital zote ukija bila barua ya rufaa unalipa bila kujali uko katika kundi lipi.
Hilo ndio mh. RC hakujua au alijua akaamua kutafuta kick.
Watu hawafahamu wafanyakazi wa hospitali/afya wanavyokuna vichwa kuhudumia wananchi. Watu wasirukie kuchangia/kushabikia vitu wasivyovifahamu
.
 
Kwa lililotokea kwenye hiyo video,mimi nipo upande mmoja na Hapi...hata kama ni daktari bingwa haiwezekani awaumize ndugu zetu wakati serikali ilishatangaza matibabu bure kwa watoto chini ya miaka 5,wazee kuanzia miaka 60 na akina mama wajawazito afu mtu aje Awalaipishe hela,tena bila mganga mkuu wa hospital kushirikishwa,katibu mkuu wa wizara including waziri na boby ya hospital halafu mseme jamaa kakurupuka,hapana aisee,pia hajamfukuza kazi ili kamkataa ndani ya mkoa wake kutokana na utendaji wake mbovu,hata kama Hapi ana mapungufu mengine lakini sio kwenye hili aisee,tu`reason vitu bila chuki wakuu!
Una uhakika hizo fedha zinazotengwa kwa ajili ya kuhudumia hayo makundi zote zinafika? Una hakika hizo fedha zinakidhi mahitaji?
Kuhusu maslahi yetu umejiridhisha yameboreshwa?
 
SIJAONAKOSA LA API

MATAPELI WAMEJAASAANA WIZARA ZA AFYA...WASHENZI MNASHABIKIA UPUUMBAVU WA DK MNAJUA WATOTO WANGAPI WAMEKUFA KWA KOSA 12K

FANKURUMANYOYA NYIE...API PGAKAZI
Usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Hospitali ya rufaa inatibu bure mgonjwa mwenye barua ya rufaa kama umekuja kutibiwa bila rufaa UnafanyA malipo
 
Hivi kumbe lengo ni kumbomoa Msigwa?? Tanzania kuna viongozi "wapumbavu" kuliko India.
Siasa za kulenga watu badala ya issues ni mbaya sana!!.... Mimi ni mwanaccm niliyekabidhiwa kadi yangu ya uanachama na mwalimu Nyerere mwaka 1987 pale katika uwanja wa Samora lakini katika tukio hili nakubaliana na Waziri Jaffo!
 
Happy hana kosa hata kidogo ukiangalia creep nzima na ukaisikiliza kwa makin maamzi aliyoyachukua kwa mtu yoyote mwenye uchungu angeyafanya isitoshe Huyo Dk kapewa muda wa kutosha sana wa kujieleza kashindwa yaani happy hajakurupuka kusema ukwel tu bila kuegemea upande
Mtu mwenye uchungu kwa lipi? Unauelewa wowote kuhusu hamisha ya hosptali za mikoa kwenda wizarani toka tamisemi baada ya rais kutoa tangazo lake mwaka jana alipokuwa anazindua hosptali ya mloganzala!,kwa sasa hosptal za mikoa,zinakuwa za rufaa za mikoa,na zinahitajika ziongeze mapato na kuwa katika ngazi ya rufaa,inatakiwa zipokee wagonjwa wale wenye hadhi ya rufaa na sio kila mgonjwa anakwenda kutibiwa huko.Pia naomba uchunguze O.C(other charge) inayoletwa na serikali kuendesha hosptali ni kiasi gani kwa mwezi,nyingi huangukia chini ya 20 au 30 ml kwa mwezi,hapo kuna kuendesha huduma za maji,umeme,kununua madawa,kununua vifaa tiba,halafu unatumia sera ya bure ilihali hao wanasiasa hawaisemi serikali kuongeza O.C ili hosptali kujisimamia na kuweza kutoa huduma za bure kama sera yao.
 
Siasa za kulenga watu badala ya issues ni mbaya sana!!.... Mimi ni mwanaccm niliyekabidhiwa kadi yangu ya uanachama na mwalimu Nyerere mwaka 1987, lakini katika tukio hili nakubaliana na Waziri Jaffo!
Huyu ndo Johnthebaptist ninayemfahamu Mimi kama miongoni mwa wanaccm wenye uwezo wa kujenga hoja. Wiki iliyopita nilikushangaa kwa kutoka nje ya mstari kwa sababu za kisiasa nikakupiga lakini hukunijibu. Penye O tuseme O haina haja ya kusema ni sifuri hata kama zinafanana. Viongozi wa kisiasa wamekuwa na maamuzi ya ovyo dhidi ya watumishi kwa kusikiliza upande mmoja na kutoa maamuzi ya kuwaadhibu watumishi bila kuchimba ukweli. Mwanzo mwa utawala wa awamu hii Mh. Majaliwa alipotoshwa na mwananchi asiyejua taratibu za hospitali alipolipishwa 80,000/- ili ndugu yake afanyiwe operesheni ikiwa ni gharama ya op yenyewe, madawa na vifaa kwa kuambiwa aliombwa rushwa. Kwa kasi ya ajabu akatoa maamuzi ya kumaimamisha kazi Daktari yule na jambo hilo lililotokea mkoani Lindi lilileta mtafaruku mkubwa kiasi cha Madaktari kutishia kugoma hadi Mkuu wa Mkoa alipoingilia kati kupata ukweli na PM kutengua maamuzi yake kimya kimya. Tangu siku hiyo sijawahi kumuona Mh. Majaliwa akitoa maamuzi ya kukurupuka.
 
Ma DC+RC wa awamu hii wengi ni Malopolopo tu hawana lolote kichwani... wapo kwa kazi maalum tu ya mtu 1
 
Do not allow your emotions to interfere your judgement Mr Hapi!
 
Kama video inavyojieleza sijaona tatizo LA Hapi waungwana tujalibu kuacha siasa Kwa mambo ya msingi.
 
Kosa analo na amefanya makusudi ili apate platform ya kisiasa. Ni kwamba hospital ya rufaa ukienda bila kuwa na barua ya rufaa unalipa pesa kama kawaida

Angalia video husika, daktari mwenyewe ameulizwa utaratubu wa kutibia wazee na watoto amekiri ni bure ila wenyewe wamejipangia. Utaratibu huo si wa jana wala leo, ni wa miaka mingi sana
 
Mamanina yanatafuta sifa za kijinga!!
Kwa hali jinsi ilivyo mikoani kila mtu anataka kwenda kutibiwa hospitali ya mkoa
Sasa kupunguza utitiri wa wa watu serikali yenyewe imeweka utaratibu kuwa (kwa mfano morogoro) ukienda hospitali ya mkoa bila kupita hospitali ya kata ukapata rufaa kuandikishwa tu ni elfu10, lakini ukipata rufaa wala hulipiii
 
Kwa lililotokea kwenye hiyo video,mimi nipo upande mmoja na Hapi...hata kama ni daktari bingwa haiwezekani awaumize ndugu zetu wakati serikali ilishatangaza matibabu bure kwa watoto chini ya miaka 5,wazee kuanzia miaka 60 na akina mama wajawazito afu mtu aje Awalaipishe hela,tena bila mganga mkuu wa hospital kushirikishwa,katibu mkuu wa wizara including waziri na boby ya hospital halafu mseme jamaa kakurupuka,hapana aisee,pia hajamfukuza kazi ili kamkataa ndani ya mkoa wake kutokana na utendaji wake mbovu,hata kama Hapi ana mapungufu mengine lakini sio kwenye hili aisee,tu`reason vitu bila chuki wakuu!


HIYO BURE UNAYOISIKIA NI KISIASA TU ANACHOFANYA DR NI SAHIHI...
 
Back
Top Bottom