Mkuu wa Mkoa wa Singida, kwa kuwa leo unafanya mkutano na wakaazi wa Singida mjini, pale viwanja vya Stend ya Zamani. Kwanza asante kwa kuitisha Mkutano, tunaomba kama una ujasiri kweli wa kuita mkutano uwaombe radhi wana Singida kwa kujipatia tenda ya Kuzoa Taka katika Manispaa wakati haujamiliki hata toroli la kuzolea Taka.
Uliingia Ubia na Mkurugenzi mkawa mnatumia gari ya Halmashauri na kujaza mafuta kwa pesa ya Halmashauri wakati inaonekana pesa ulikuwa unakwapua wewe kwa kutumia kampuni ya (PAVICO Ltd) (Perseko Vincent Kone) na kuonekana umeshinda tenda ya kuzoa taka. Uliwalazimisha madiwani kukubali ufedhuli huu.
Kama hiyo haikutosha uliposhindwa hiyo kazi umelalamikiwa na wafanyakazi wa Kampuni yako, na Mtoto wako alijichukulia madaraka mikononi kuwamwagia sumu vijana wetu wa Singida. Kesi imefunguliwa Polsi, mkaamua kuifuta haraka pamoja na fomu za daktari kuonyesha kuwa wamedhuriwa na sumu, sasa mmewatisha vijana wa watu.
Tunazidi kukuambia kuwa damu ya wana Singida itakulilia. Na kwa kuwa Kikwete anajidai hajui haya mabaya unayotutendea ndo maana amekubakiza ila yote yana Mwisho na Mungu hata Singida yupo. Ukiweza omba radhi leo....................
Uliingia Ubia na Mkurugenzi mkawa mnatumia gari ya Halmashauri na kujaza mafuta kwa pesa ya Halmashauri wakati inaonekana pesa ulikuwa unakwapua wewe kwa kutumia kampuni ya (PAVICO Ltd) (Perseko Vincent Kone) na kuonekana umeshinda tenda ya kuzoa taka. Uliwalazimisha madiwani kukubali ufedhuli huu.
Kama hiyo haikutosha uliposhindwa hiyo kazi umelalamikiwa na wafanyakazi wa Kampuni yako, na Mtoto wako alijichukulia madaraka mikononi kuwamwagia sumu vijana wetu wa Singida. Kesi imefunguliwa Polsi, mkaamua kuifuta haraka pamoja na fomu za daktari kuonyesha kuwa wamedhuriwa na sumu, sasa mmewatisha vijana wa watu.
Tunazidi kukuambia kuwa damu ya wana Singida itakulilia. Na kwa kuwa Kikwete anajidai hajui haya mabaya unayotutendea ndo maana amekubakiza ila yote yana Mwisho na Mungu hata Singida yupo. Ukiweza omba radhi leo....................