Rc Mnyeti, Mbunge ole Milya waitwa Takukuru

buswelu moja

JF-Expert Member
Aug 24, 2014
226
147
Mwandishi wetu, Manyara

Siku chache baada ya Mbunge wa jimbo la Simanjiro mkoani Manyara, James Ole Milya na mkuu wa mkoa huo kushutumiana kwa rushwa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) imewaita ofisini.

Ole Milya na Mnyeti walishutumiana hivi Karibuni mbele ya Waziri wa madini, Dotto Biteko wakati wa uwasilishwaji wa Ripoti ya migogoro ya mipaka baina ya Tanzanite One na wachimbaji wadogo.

Katika shutuma hizo Ole Milya alimtuhumu hadharani Mnyeti kupokea rushwa kutoka kampuni ya Tanzanite One kwa lengo la kuwakandamiza wachimbaji wadogo huku akihoji ukaribu wa kiongozi huyo na wakurugenzi wa kampuni hiyo.

Hatahivyo, Mnyeti naye alimtuhumu Ole Milya kuwatishia kwa silaha ya moto (bastola) baadhi ya wafanyabiashara wa madini mkoani humo huku akienda mbali na kudai kwamba ana kesi tano ambazo zimewasilishwa mezani kwake zinazomhusu.

Taarifa kutoka Takukuru zinadai kwamba viongozi hao wameitwa mnamo Agosti 6 mwaka huu katika ofisi za Takukuru mkoani Manyara ili waweze kutoa maelezo ya kina kuhusu tuhuma hizo.

Hatahivyo taarifa zinadai kwamba tayari mkuu wa wilaya ya Simanjiro mkoani humo, Zephaniah Chaula ameanza kuwapigia simu baadhi ya wafanyabiashara kwa agizo la Mnyeti ili wajitokeze mbele ya Takukuru kutoa maelezo kwamba walitishiwa silaha na Ole Milya.

Hatahivyo, Takukuru pia inachunguza taarifa kuhusu utajiri wa Rc Mnyeti aliojipatia ghafla akiwa mkuu wa mkoa wa Manyara na endapo mali hizo ameziorodhesha Serikalini katika orodha ya mali anazomiliki.

Miongoni mwa mali hizo ni hoteli ya kitalii anayojenga kanda ya ziwa, shule ya sekondari, klabu ya soka ya Gwambina FCpamoja na mabasi mbalimbali ya kusafirisha abiria.

Mwisho.
IMG-20190728-WA0025.jpeg
 
Huu ni utawala wa mchwa, yaani mpaka awamu hii iishe nchi itakuwa imebaki gofu ,maana hawa viwavi jeshi ni wanakula balaa...Kuanzui baba lao Jiwe, njoo bashite na hivyo vipanya vingine....Yaan niwaambie ndugu zangu NCHI INALIWA...

Halo wameitwa geresha tu kuambiwa wasiaibishane hadharani badala yake wasuluishe mambo yao kimya kimya si kila MTU ajue...

We hushangai, lini Takukuru wakaita mtu.. Mara nyingi wakiteka mtu alafu watu wakajua utaskia KAKAMTWA NA TAKUKURU
 
Taarifa kutoka Takukuru zinadai kwamba viongozi hao wameitwa mnamo Agosti 6 mwaka huu katika ofisi za Takukuru mkoani Manyara ili waweze kutoa maelezo ya kina kuhusu tuhuma hizo.


Hao PCCB kwanini wasifanye haraka kutompa mwanya wa kupoteza ushahidi??? Au nao ni walewale!!!
 
Hatahivyo, Mnyeti naye alimtuhumu Ole Milya kuwatishia kwa silaha ya moto (bastola) baadhi ya wafanyabiashara wa madini mkoani humo huku akienda mbali na kudai kwamba ana kesi tano ambazo zimewasilishwa mezani kwake zinazomhusu.


Kwanini ana kaa na hayo malalamiko mezani badala ya kuyafikisha kwenye mamlaka husika!!! au ni hofu ya mwaga ugali nimwage mboga
 
Hatahivyo taarifa zinadai kwamba tayari mkuu wa wilaya ya Simanjiro mkoani humo, Zephaniah Chaula ameanza kuwapigia simu baadhi ya wafanyabiashara kwa agizo la Mnyeti ili wajitokeze mbele ya Takukuru kutoa maelezo kwamba walitishiwa silaha na Ole Milya.


Vodacom!!! fursa nyingine hiyo changamka!!!
 
Shauri yao! Wachapane risasi tu, tuzike. Itakuwa good riddance to bad garbage
 
Kiufupi Mnyeti ndio Mla rushwa mkubwa ila ni mtoto wa baba kama makonda.
Makonda anabadilisha magari kila siku wapi mliona akinyooshewa kidole?
Takukuru wawe makini sana wasije wakakuta hizo Hoteli ni za Jpm na ile timu ni ya jpm.

Nyie hamjiulzi ile team na ule uwanja ingekuw Ni ya January laZima angetajwa kwenye speech.
 
Tumeliwa Sana Ndugu Zangu
Tuchezewa Sana Ndugu Zangu
Tumegongwa Sana Ndugu Zangu
Ukikubali Kulaliwa Mwisho Utapasuka Utakuwa Kama Pono.
Vyovyote Mtakavyosema Lakini Mmenielewa
 
Waliitwa Agosti 6 mwaka huu,leo trh 4 Agosti mwaka huu.Hii imekaaje mleta uzi?
Mwandishi wetu, Manyara

Siku chache baada ya Mbunge wa jimbo la Simanjiro mkoani Manyara, James Ole Milya na mkuu wa mkoa huo kushutumiana kwa rushwa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) imewaita ofisini.

Ole Milya na Mnyeti walishutumiana hivi Karibuni mbele ya Waziri wa madini, Dotto Biteko wakati wa uwasilishwaji wa Ripoti ya migogoro ya mipaka baina ya Tanzanite One na wachimbaji wadogo.

Katika shutuma hizo Ole Milya alimtuhumu hadharani Mnyeti kupokea rushwa kutoka kampuni ya Tanzanite One kwa lengo la kuwakandamiza wachimbaji wadogo huku akihoji ukaribu wa kiongozi huyo na wakurugenzi wa kampuni hiyo.

Hatahivyo, Mnyeti naye alimtuhumu Ole Milya kuwatishia kwa silaha ya moto (bastola) baadhi ya wafanyabiashara wa madini mkoani humo huku akienda mbali na kudai kwamba ana kesi tano ambazo zimewasilishwa mezani kwake zinazomhusu.

Taarifa kutoka Takukuru zinadai kwamba viongozi hao wameitwa mnamo Agosti 6 mwaka huu katika ofisi za Takukuru mkoani Manyara ili waweze kutoa maelezo ya kina kuhusu tuhuma hizo.

Hatahivyo taarifa zinadai kwamba tayari mkuu wa wilaya ya Simanjiro mkoani humo, Zephaniah Chaula ameanza kuwapigia simu baadhi ya wafanyabiashara kwa agizo la Mnyeti ili wajitokeze mbele ya Takukuru kutoa maelezo kwamba walitishiwa silaha na Ole Milya.

Hatahivyo, Takukuru pia inachunguza taarifa kuhusu utajiri wa Rc Mnyeti aliojipatia ghafla akiwa mkuu wa mkoa wa Manyara na endapo mali hizo ameziorodhesha Serikalini katika orodha ya mali anazomiliki.

Miongoni mwa mali hizo ni hoteli ya kitalii anayojenga kanda ya ziwa, shule ya sekondari, klabu ya soka ya Gwambina FCpamoja na mabasi mbalimbali ya kusafirisha abiria.

Mwisho. View attachment 1171729
 
Mnyeti na rushwa ni damdam hawezi kuacha sababu ana baraka zoote toka juu, ukuu wa mkoa aliupata baada ýa kufañikisha mradi wa rushwa
 
Back
Top Bottom