RC Makonda kwa hili hapana..

RC Makonda kwa hili hapana..

Baada ya meya wa Dar kusema wataangalia utaratibu mpya boda boda waingie taoo na yy kadakia tena na mikopo juu, watatuheshimu tu sisi wenye kula zao,,,,,
 
Ni aibu kwa taifa changa kama Tanzania kutokujua namna ya kuwageuza vijana kuwa mtaji wa maendeleo ya taifa hadi kubaki tunawalalamikia pale wanapoamua kuacha kupiga ngeta na kufanya shughuli halali za kujipatia riziki.
Tujaribu kuwa na dira ya maendeleo ya kiuchumi yenye kuainisha maeneo ambayo nchi inahitaji nguvu kazi zaidi ili kufanikiwa,halafu tuweke miundombinu kama elimu,mitaji n.k ili kuwasukuma vijana kuajiriwa au kujiajiri kwenye maeneo hayo ya kiuchumi,then tuone kama wataendelea kukimbilia bodaboda.
Taifa linalolalamika vijana kuwa mzigo ni taifa linaloelekea kaburini.
Taifa hai hufurahia kizazi chake kwa kuwa ni mtaji wa maendeleo.
Nikipita mitaa ya fire huwa nawaangalia wale madogo ombaomba na kujisemea moyoni,"hiki ndicho walichofundishwa na kutumwa na wazazi wao ambao pia ni ombaomba",halafu nawaza,what if mzazi wao angekuwa serikali na kuwafundisha jambo fulani la maendeleo na kisha kuwatuma nchi nzima wakalifanye baadae wakiwa wakubwa?
Tuwageuze vijana kuwa mtaji wa maendeleo ya taifa.
Tusilalamike,tuwawezeshe.
Tusikae humu tunawazungumzia kama vile wao ni majini toka kuzimu.
Tumewazaa sisi wenyewe.
Waafrika tuache hulka ya kudharau vijana na kuwaona raia wa daraja la pili.
Kabla hujamlaumu mtoto kwa tabia mbaya jiulize unamleaje.
 
Anayefikilia bodaboda kuwa ajira ana mawazo mgando vijana hawa hawana maisha marefu kwa kuwa watakufa kwa kuugua vifua, watatua kwa ajari, ujambazi, pia ni waathirika wakubwa wa virutubisho vya nguvu za kiume kwani sehemu yao ya siri hukaa ikichemka na kujigongagonga kwenye tenk la mafuta kuzifanya mbegu zisitulie kwa ajiri ya matumizi ya baadaye
 
Jimbo gani analitaka??
Kwa hizi kauli za kiajabuajabu nani ampe jimbo! Aangalie utendaji wake pale alipo hakuna siasa, kama bado hajalijua hilo aanze kutafakari. Kwani bodaboda ushakuwa usafiri rasmi? Au ni kutokana na kutokuewpo na mipangilo mizuri ya miji na kiusafirishaji? Hili suala la bodaboda wengi wanalichukulia kama ndio usafiri rasmi, kuna sababu zingishapatiwa ufumbuzi wenyewe watatoweka taratibu. Ajaribu kuwa mbunifu kwa kuona hali halisi ya baadae!
 
K
Anayefikilia bodaboda kuwa ajira ana mawazo mgando vijana hawa hawana maisha marefu kwa kuwa watakufa kwa kuugua vifua, watatua kwa ajari, ujambazi, pia ni waathirika wakubwa wa virutubisho vya nguvu za kiume kwani sehemu yao ya siri hukaa ikichemka na kujigongagonga kwenye tenk la mafuta kuzifanya mbegu zisitulie kwa ajiri ya matumizi ya baadaye
.....ni kweli bro....
 
…""Kazi yangu ni boda boda, Ninaipenda bodaboda""..( In Linex's voice ).
 
Mimi kwa hili nimpongeze Mh. Makonda kukutana na hawa vijana wa boda boda na kuongea nao namna ya kutatua changamoto zao japo kuna sehemu alikuwa anashambulia kisiasa zaidi badala ya nafasi yake ya utendaji.
Huwa nategemea mh. akikutana na watu aweke siasa pembeni kwa ndie top wa mkoa kwa hiyo aangalie kazi yake asigawe wananchi kwa misingi hiyo.

Pili Mh.Makonda bodaboda ni sehemu ndogo tu ya vijana wanaoishi dar es salaam bado kina makundi mbalimbali yanayofanya kaz zingine sasa ni wakati wa kuwatembelea wate kulingana na Nazi zao.
Mfano ni sisi vijana tunaofanya biashara ya kuuza nyama bei ya jumla ktk machinjio ya ukonga.
Sisi tuna umoja wetu unaojulikana kama 'UMOJA WA KUUZA NYAMA BEI YA JUMLA'(UWANJU).
Mheshimiwa nimelazimika kupitia uzi huu kwa sababu tunakabiliwa na changamoto nyingi sana ktk eneo tunalo fanyia kazi.
Kwa ufupi machinjio ya Ukonga ni machinjio yanayomilikiwa na watu binafsi ambao wanajulikana kwa jina la UWEMA kwa umoja wao maanake sisi UWANJU tunafanya biashara chini ya eneo hilo kwa hiyo sisi ni kama wapangaji wa eneo hilo.
Lakini sisi kama wapangaji tunasumbuliwa sana na hawa wamiliki wa eneo hili.
Kimsingi machinjio ya Ukonga ni machinjio kubwa kwa jiji la dar es salaam ikifatiwa na Vingunguti ambayo ni machinjio ya serikali, na ktk machinjio haya zaidi ya vijana 2000 wamejiajiri ktk sekta hii.
Kero zetu ni pamoja na kutokuwa na uhakika na shughuli tunayofanya eneo la kazi kwani huwa machinjio yanafungwa mara kwa mara licha ya pesa nyingi tunayolipa kwa wamiliki hao, hivyo kutusababishia usumbufu mkubwa kwetu sisi na familia zetu.
Pia kuna baadhi ya mazao yanayotokana na hiyo inayochinjinjwa tunadhulumiwa na hao wamiliki ambapo kimsingi ni mali yetu mfano ni zao la damu inayotoka kwenye ng'ombe, ukiuliza au ukidai unatishiwa kufukuzwa au kufungiwa biashara yako ktk eneo hilo.
Suala lingine ni ushuru mkubwa tunaolipishwa kwa kila ng'ombe tena bila majadiliana kati yetu wafanyabiashara na hao wamiliki wa eneo hilo, mfano tunawalipa Tsh.5300/- kwa kila ng'ombe ambayo inaenda moja kwa moja kwa wamiliki hao, lakini pia tunalipia manispaa Tsh 2500 kila ng'ombe lakini mwisho wa siku machinjo yanafungwa eti hayakidhi vigezo wa kuhaika zaidi ni sisi maana tunategemea shughuli hiyo.
Na machinjio hiyo ipo toka mwaka 1974 kibaya zaidi hela tunayolipa manispaa 2500/- hatuoni mrejesho wake kwetu kwani sisi ndio tunaoitoa moja kwa moja sio wamiliki.
Kwa siku machinjio yetu yanauweza wa kuchinja ng'ombe zaidi ya 400 kwa siku ukizidisha kwa kwa hiyo 2500 ya manispaa kwa mwaka ni mamilion ya hela lkn nina hakika hata mkurugenzi wa manispaa wa Ilala analielewa hilo lkn sijawahi kusikia akaja kukaa na sisi ili timueleze hizo changamoto, wakati wakati mwingine anakutana na wamiliki ambao hiyo hela ya 2500 haiwagusi hata kidogo.
Wamiliki wao wakishachukua 5300 yao kutoka kwetu wanafanyia yao wanayoweza wenyewe.
Pia kuna kutokuelewana kati ya hawa wamiliki (UWEMA) na sisi wafanya biashara
( UWANJU) japo tunahitaji undugu mkubwa kufanya biashara yetu kwani Uwema wanapambana ili kuua umoja wetu Uwanju ili wapate kututawala zaidi wakiwaattack viongozi hata kutishia kuwakataza kufanyia biashara ktk eneo lao.
Pamoja na mengine mengi ambayo ungetufikia kama uwanju tungeweza kuongea mheshimiwa.
Lakini kubwa tulikuwa na ombi kwako kama ulivyosema wakati unaongea na vijana wa Bodaboda kuwa wewe ndie rais wa Dar es salaam kwa kushirikiana na Manispaa ya Ilala TUJENGEE MACHINJIO MAPYA YATAKAYOMILIKIWA NA SERIKALI YATAKAYOKIDHI VIGEZO ILI UTUEPUSHE NA USUMBUFU WA WATU BINAFISI, sisi vijana wenzako tunateseka wakati tunauwezo wa kuibadili dar kuwa kivutio cha majiji yote dar.
Kama serikali hamna uwezo tutafutie wafadhili watujengee machinjio ya kisasa kwa udhamini wenu sisi tunauwezo wa kulipa mkopo huo.
Tuna damu inayotokana na mifugo hiyo kwa mwezi huwa hawa wamiliki huwa wanapokea zaidi ya Million 100 kwa ajili ya mauzo ya damu hiyo.
Hiyo 5300 tunayowalipa wamiliki tutatumia kulipia mkopo mtakaotudhamini kwa mda mtakao tupa, huo mkopo ukiisha hiyo hela na damu za mifugo zitatumika kutuendeleza kiuchumi.
Tuna mbolea ambayo inaweza kutumika kuzalisha umeme (bio electric power) kama tutaumiliki mradi kwa ufanisi hiyo mheshimiwa itakuwa credibility kubwa kwako.
Lakini kikubwa tunakuomba tutembelee sisi wafanya biashara wa Uwanju sio wamiliki ambao wageni wakija kututembelea hawataki tueleze kero zetu ukieleza wanakufanyia figisu figisu.

Mawasiliano;
Uwanju.
Tel 0715535587; katibu.

0714404272; mjumbe.
Moderator tunaomba utufikishie ujumbe kwa Mheshimiwa Makonda.
d
 
RC Makonda wew ni kijana wa mfano kwa sasa, umeonyesha kufanya mengi mazuri.

Kwa hili la bodaboda ebu tafakali kwanza na jaribu kupata mawazo ya wadau hasa Polisi na raia kwa ujumla. hata sisi tunafurahi kuwepo kwa bodaboda maana ni ajira pia zinalahisisha usafiri, bodaboda ni ajira kwa vijana wengi lakini lazima tuangalie changamoto za ajira hii kwa umakini zaidi..

Boda boda kwa makusudi wameuwa watu kwa umoja wao, wanashiriki katika matukio ya uhalifu, wanajeshi lao na wanajiona kuwa wako juu ya sheri, hawataki kufuata sheria. Kwa hiyo kutafuta namna ya kuwaongeza jijini ni kuhatalisha maisha ya wakazi wa Dar.

Kutaka kuongeza bodaboda jiji la Dar esalaam ni kuongeza matatizo kwa raia na pia ni kuwaita vijana walioko vijijini na miji mingine midogo kuja dar. Hii hali itaongeza population dar na baadhi ya matendo mabaya kuongezeka.

Ni vyema sasa ujitahidi kuziondoa pikipiki jiji la dar na sio kuziongeza, tafuta namna ya kuwasaidia vijana kwa njia nyingine na siyo hii ya bodaboda.


Nakubaliana na wewe, bodaboda ni hatari. Vijana wa bodaboda ni watu wa hatari kwa usalama wa raia. Maeneo ya ubungo yanatisha kwa sababu ya bodaboda. Bodaboda sehemu za ubungo wanaendesha bodaboda zao kwenye sehemu za waenda kwa miguu, na wakimgonga raia wanakuja zaidi ya 20 na bodaboda zao na kuleta vitisho.
 
anasema atawapa mikopo ya bodaboda kwa marejesho ya tsh 2500 kwa wiki... kwa maana hiyo kila kijana anayetaka kupata bodaboda atapata..kitakachofuata sijui..
2,500 kwa wiki?! ina maana kwa mf. bodaboda ya mil. 1,800000 ya kichina marejesho ni miaka 15!!! amaizing! inachekesha! ngoja tuone huyu rc anapoelekea! teh teh!
 
RC Makonda wew ni kijana wa mfano kwa sasa, umeonyesha kufanya mengi mazuri.

Kwa hili la bodaboda ebu tafakali kwanza na jaribu kupata mawazo ya wadau hasa Polisi na raia kwa ujumla. hata sisi tunafurahi kuwepo kwa bodaboda maana ni ajira pia zinalahisisha usafiri, bodaboda ni ajira kwa vijana wengi lakini lazima tuangalie changamoto za ajira hii kwa umakini zaidi..

Boda boda kwa makusudi wameuwa watu kwa umoja wao, wanashiriki katika matukio ya uhalifu, wanajeshi lao na wanajiona kuwa wako juu ya sheri, hawataki kufuata sheria. Kwa hiyo kutafuta namna ya kuwaongeza jijini ni kuhatalisha maisha ya wakazi wa Dar.

Kutaka kuongeza bodaboda jiji la Dar esalaam ni kuongeza matatizo kwa raia na pia ni kuwaita vijana walioko vijijini na miji mingine midogo kuja dar. Hii hali itaongeza population dar na baadhi ya matendo mabaya kuongezeka.

Ni vyema sasa ujitahidi kuziondoa pikipiki jiji la dar na sio kuziongeza, tafuta namna ya kuwasaidia vijana kwa njia nyingine na siyo hii ya bodaboda.
bodaboda haiwezi kua ndio usafiri wa umma dar wala suluhisho la ajira mijini kwa vijana sio bodaboda. viwanda ndio suluhisho... jeshi la bodaboda laweza kuja kua tishio sio kwa usalama barabarani tu ila kijamii na kisiasa. yafaa kua makini kuhusu kuendeleza usafiri wa bodaboda mijini badala yake tuimarisha usafiri wa umma na kujenga barabara za kisasa kama flyovers kuondoa msongamano.
 
Najua mtanipinga ila huu ndo ukweli wenyewe...kwa kiasi kikubwa sana ajali za bodaboda zinachangiwa na madereva uchwara wa magari,madereva ambao hawajui sharia za barabarani,maderevea ambao reseni wamepata kimagumashi,madereva wa auto..mnakosea sana mnapowatupia lawama bodaboda pekee kana kwamba izo ajali uwa wanagongana wao kwa wao...miundombinu mibovu sio rafiki kwa bodaboda,ubabe wa waendesha magari kuona wao ndo wao barabarani na mengineyo pia yanachangia sana..tusitoe lawama 100% kwa bodaboda tu,njia pekee ya kuziondoa bodaboda ni kutozipanda....aya msipande sasa tuone kama mtadumu na ivo vibarua vyenu vya ofisini
 
Huyu atakuja kutuletea tatizo kubwa sana kama asipodhibitiwa, vijana wanahitaji muongozo bila hivyo ni shida
Amesifiwa kavimba kichwa anaona yeye ndio Kila kitu kumbe anaharibu.amekuja na wazo la kitoto sana na kimsingi linahatarisha usalama na ustawi wa jiji la Dar
 
Mwache ajidanganye! Hivi hajasikia Ma-DC wanavyotimuliwa kwenye mabaraza ya madiwani maana wao siyo wajumbe! Hata yeye siyo mjumbe hivyo hakika atakuwa anasikia tu kwamba leo meya wa jiji anagawa hela ya mikopo bila yeye kujua! Hii ndo shida ya vijana wakipewa madaraka makubwa! Ukuu wa mkoa wapewe watu ambao ni wakomavu kiakili na kimwili!
Huyu Makonda atawaharibia vijana kupewa nafasi kubwa maana anadhani waliomtangulia wote hawafikiri ila yeye.anapanga kuwaruhusu bodaboda waingie katikati ya jiji bila kujiuliza kwanini waliomtangulia waliwazuia.huyu kijana in hatari.
 
2,500 kwa wiki?! ina maana kwa mf. bodaboda ya mil. 1,800000 ya kichina marejesho ni miaka 15!!! amaizing! inachekesha! ngoja tuone huyu rc anapoelekea! teh teh!
Inashangaza sana!
 
Matatizo ya nchi/jiji hayawezi kutatuliwa na Mwanasiasa mfano wa PAUL MAKONDA, ISIPOKUWA wataalamu tu!!
Huyu kijna ana mihemko ya Kupenda sifa na kujifanya anafahamu kila kitu!!

Tunawaomba MIPANGO MIJI +SUMATRA+ POLISI +JWTZ+TISS waachiwe suala la bodaboda.
 
awape



alitakiwa awape training za busness.. alafu awape mikopo na awatume wakafanye busness machinga complex.. swala la pikipiki linatakiwa liwekewe ugumu wa kumiliki.. yaani kumiliki pikipiki iwe vigumu kama kumiliki silaha..bodaboda ni shida kubwa sana.. majambazi wamejificha humo..
Pale machinga complex hakuna biashara ya kufanya pale ndo maana hata waliopewa vizimba vya kufanya biashara wengi wamevitelekeza na kurudi mtaani! Jamani hivi shughuli za kufanya ni umachinga, uchuuzi na bodaboda tu? hii ni kuwapumbaza tu, tunataka kuona vijana wanazalisha mali sio kuwafanya wachuuzi
 
RC Makonda wew ni kijana wa mfano kwa sasa, umeonyesha kufanya mengi mazuri.

Kwa hili la bodaboda ebu tafakali kwanza na jaribu kupata mawazo ya wadau hasa Polisi na raia kwa ujumla. hata sisi tunafurahi kuwepo kwa bodaboda maana ni ajira pia zinalahisisha usafiri, bodaboda ni ajira kwa vijana wengi lakini lazima tuangalie changamoto za ajira hii kwa umakini zaidi..

Boda boda kwa makusudi wameuwa watu kwa umoja wao, wanashiriki katika matukio ya uhalifu, wanajeshi lao na wanajiona kuwa wako juu ya sheri, hawataki kufuata sheria. Kwa hiyo kutafuta namna ya kuwaongeza jijini ni kuhatalisha maisha ya wakazi wa Dar.

Kutaka kuongeza bodaboda jiji la Dar esalaam ni kuongeza matatizo kwa raia na pia ni kuwaita vijana walioko vijijini na miji mingine midogo kuja dar. Hii hali itaongeza population dar na baadhi ya matendo mabaya kuongezeka.

Ni vyema sasa ujitahidi kuziondoa pikipiki jiji la dar na sio kuziongeza, tafuta namna ya kuwasaidia vijana kwa njia nyingine na siyo hii ya bodaboda.


Nahisi EL angekuwa raisi halafu akachukua maamuzi ya kuwafungulia bodaboda mjini inawezekana mtoa post ungesifia (samahani, nimehisi tu).
Tukiondoa hisia, ngoja nirudi kwenye point:
Mimi namuunga mkono Makonda kwa sababu zifuatazo:
1. Akitengeneza utaratibu mzuri kama aliosema wa kuunda vikundi na kuwavalisha jezi inaweza ikaondoa tatizo
2. Ukiwatumia vizuri bodaboda ni walinzi shirikishi wazuri
3. Wapo wachache wanaoharibia bodaboda wote sifa kwa wizi. Ila nilishuhudia bodaboda wakimshushia kipigo mwenzao pale Kinondoni baada ya kugundulika amehusika kumpora dada mmoja pochi halafu hakujua kwamba huyo dada anamfahamu na anaishi Kino. Jamaa wakasema hawa ndio wanatuharibia sifa, polisi ndio walikuja kuokoa mtu
3. Bodaboda ni ajira na ina changamoto zake, njia bora ni kuzikabili na sio kuzikwepa
NB: Sina maslahi yeyote ya moja kwa moja na bodaboda wa Dar
 
Wakuu..
Hii hoja ya Ndugu RC Makonda embu tuitazame kwanza kwa upande chanya kisha tuamie huko kwenye changamoto..
Mimi kwa maono yangu ve+, naona nijambo jema pale Litakapo ekewa utaratibu dhabiti, hakuna linaloshindikana kama wadau wote watakua na nia na kuheshmiana/kuheshimu miiko itakayokua imewekwa..
 
Back
Top Bottom