Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 751
- 1,802
Mkuu wa Mkoa wa Arusha ,Mrisho Gambo ameendelea kuonyesha umwamba Mkoani Arusha pale alippotumia nafasi yake ya U RC kumtimua DC wa Arumeru Alexander Mnyeti kwa madai ya kuchelewa dakika kumi kwenye kikao cha Kamati ya ulinzi na usalama .
Kikao hicho kilifanyikia katika ofisi yake Gambo alionyesha kutofurahia ujio wa Mnyeti tena akiwa amechelewa na kumwambia arudi nyumbani kwake akalale baada ya kujitetea kuwa alichelewa sababu alikesha kwenye operesheni ya kuteketeza bangi katika Kijiji cha Losinoni kilichopo Arumeru.
Kwa kipindi kirefu kumekuwepo na sintofahau ya mahusiano kati ya RC Gambo na Dc Mnyeti kiasi cha kufikia kutozungumza jambo ambalo linaelezwa kuzorotesha maendeleo katika Mkoa wa Arusha .
Baadhi wa wadau wa maendeleo wameshauri Rais aangalie Uwezekano wa kuwabadilisha maeneo yao ya kazi ili Mkoa ubaki salama.
Dc Mnyeti amekiri kuondolewa kwenye kikao kwa madai kwamba alichelewa akiwa kwenye oparesheni ya kusaka wakulima wa bangi .
Kikao hicho kilifanyikia katika ofisi yake Gambo alionyesha kutofurahia ujio wa Mnyeti tena akiwa amechelewa na kumwambia arudi nyumbani kwake akalale baada ya kujitetea kuwa alichelewa sababu alikesha kwenye operesheni ya kuteketeza bangi katika Kijiji cha Losinoni kilichopo Arumeru.
Kwa kipindi kirefu kumekuwepo na sintofahau ya mahusiano kati ya RC Gambo na Dc Mnyeti kiasi cha kufikia kutozungumza jambo ambalo linaelezwa kuzorotesha maendeleo katika Mkoa wa Arusha .
Baadhi wa wadau wa maendeleo wameshauri Rais aangalie Uwezekano wa kuwabadilisha maeneo yao ya kazi ili Mkoa ubaki salama.
Dc Mnyeti amekiri kuondolewa kwenye kikao kwa madai kwamba alichelewa akiwa kwenye oparesheni ya kusaka wakulima wa bangi .