Ze Bulldozer
JF-Expert Member
- Jun 12, 2020
- 1,002
- 524
===
Katika mahojiano yake na EFM redio mkuu wa mkoa Simiyu Mhe David Kafulila amefafanua juu ya maasi yanayoendelea nchi za wenzetu na hatma ya
ukuaji wa uchumi wa Tanzania katika mizozo hiyo,
Mhe Kafulia anachambua Machafuko na matokeo yake kwa nchi zingine na namna yanavyoathiri uchumi wetu, hii ni baadhi ya michango ya RC Kafulila,
Swali, Tanzania tuna somo gani la kujifunza kutokana na machafuko yanayoendelea nchi za wenzetu?....
"Kwanza tukubaliane huwezi kujenga uchumi wala kuleta maendeleo kukiwa na machafuko ndani.
Ndio maana kazi ya kwanza ya Rais yeyote duniani ni kuhakikisha utengamano( stability) kwanza kabla ya agenda yoyote.
Rais wa awamu ya sita, Mhe Samia Suluhu Hassan unaweza kumuona vizuri katika hili na namna alivyoituliza nchi kwa sasa,
Maono yake Mhe Samia Suluhu Hassan ni kujenga Taifa ambalo wote tunakuwa sehemu ya ujenzi bila kujali tofauti za vyama, rangi, kabila wala asili yoyote bali uwezo tu wa muhusika.
Wote tunajenga kwapamoja , "Upinzani na CCM" Kwa kujenga pamoja nchi yetu kwa Upendo na Amani,
Mzee Makamba anasema tunakula asali kwa pamoja kwa maana ya "Ustawi wa Taifa kuwanufaisha watu wote",
Na hii ndio nguvu asilia ya Chama cha Mapinduzi CCM.
CCM ni chama kikongwe lakini wakati wote kinaonekana ni "chama cha kisasa" ni kutokana na kujibadilisha badilisha ili kukidhi mahitaji ya wakati husika,
Kwamfano tu,Leo hii Wakosoaji wa CCM huwezi kuwakusanya kuanzia awamu ya kwanza mpaka ya hii ya sita ukawaweka kapu moja.
Kwani wanabadilika awamu moja na nyingine, CCM inawa' swap'...
Tanzania,ndio maana ni ngumu kutengeneza 'Mass' inayoipinga CCM kutosha kuiondoa madarakani kwasababu , waliokuwa wakosoaji wa CCM awamu moja wanaweza kuwa mashabiki awamu nyingine na kinyume chake.
Hii ndio 'hirizi' ya CCM. Hakuna muujiza zaidi ya kujibadilisha kukidhi mahitaji ya wakati na hili linaifanya CCM itawale kwa miaka mingi zaidi ijayo,