RC Chalamila: Siku Mahakama Ikiamua na Kuwapa Ushindi TANROADS, Sitochelewa Kupeleka Magreda Kubomoa Nyumba Bila Kujali Mtu au Vitu Vilivyopo Ndani

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,076
49,768
Mkuu wa Mkoa wa Dar Albert Chalamila amesema ameshangazwa na watu ambao wameamua Kupeleka kesi Mahakamani kupinga Kuvunjiwa nyumba zao na TanRoads ambao wanataka kujenga Barabara ya Kimala-Kinyerezi-Bonyokwa.

Chalamila amesema ikitokea tuu Mahakama imewapa Ushindi TANROADS,muda huo huo ataingiza magreda Kubomoa Nyumba zilizopo kwenye Hifadhi ya Barabara bila kujalisha mtu au vitu Vilivyopo Ndani.

Chalamila anasema Hatuwezi kuvumilia ujinga wa Kuzuia maendeleo.
===
"Leo nimesikitika sana nilivyopata taarifa eti wapo wananchi wachache ambao wanakusudia kuipeleka TANROADS Mahakamani kwamba, sawa sina tatizo na hilo mimi nawaunga mkono ila siku kesi itakapoamuliwa, ikiamuliwa saa 03:00 kwamba TANROADS wana haki saa 03:15 nitakuwa nimeshaingiza magreda bila kujali aliyepo ndani na bila kujali vitu vilivyoko ndani,

Naomba nirudie tena Mheshimiwa Prof. Kitila (Mbunge wa Ubungo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji) amesema tuko kwenye nchi ya kisheria na mimi naomba niwathibitishie kwamba nitaisubiri Mahakama na kwa kuwa mimi najuwa haya ni maendeleo kwa watu Mahakama itaamua kutokana na weledi wake.

Lakini ikiamua Mahakama saa 05:05 basi saa 05:10 greda litakuwa limeshapiga mtama nyumba zote bila kujali aliyeko ndani wala bila kujali kilichomo ndani, utoto wa namna hii hatuwezi kuufuga kwenye jimbo ambalo watu wamelia kwa muda mrefu wakihitaji maendeleo" -

ChalamilaMkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila amezungumza hayo wakati alipokuwa mgeni rasmi kwenye hafla ya kukabidhi Mkandarasi mradi wa ujenzi wa Barabara ya Kimara - Bonyokwa - Kinyerezi leo, Jumamosi Machi 09.2024


My Take

Wananchi wakubali kuwa maendeleo Yana gharama zake hivyo wachukue fidia ambayo Serikali Iko tayari kuolipa vinginevyo wanaweza kosa vyote.

Tunazuia maendeleo kisa kesi.

View: https://youtu.be/YxGj0X9C760?si=0U7n_oCpF4yDUCn1
 
Wanaomshukuru sio waliovunjiwa ila wanaonufaika.

Magufuli hakulipa hata jero Kwa wahanga,Samia Amekuja kuwalipa na Kuwafuta Machozi.
Ilikuwa ujinga kuwalipa watu ambao wamejenga kwenye hifadhi. Ni upigaji mwingine tu kuwa pesa wamelipwa watu wakati uhalisia nyingi tumegawana.

Kama mtu kaambiwa usijenge hapa, halafu akafanya ukaidi akajenga, apigwe tu nami nasema apigwe. Hakuna kulipia upuuzi... Kila mtu awe makini na sheria.
 
Hapana. Walipwe hela zao zote. Serikali haishindwi kuwalipa. Kwani kabla ya kujenga barabara hwakufanya tathmini ya hizo nyumba?
Walilipwa fidia muda mrefu, wakafuta X wakauza nyumba na viwanja kwa wakujwa wasiofuata sheria.

Hata Gongolambo watu wamefungua akaunti kulipwa fidia kupisha mradi wa mwendokasi, ila bado watu wanauziwa nyumba na viwanja vitakavyolipiwa na serikali. Baadae wajilize wadai Rais awalipe fidia
 
TABROADS ndio wanatoa ruhusa ya ujenzi wa makazi?
Hakuna anaetoa ruhusa ya ujenzi wa makazi kwenye Hifadhi ya Barabara.Kama TanRoads waliingiliwa Kwa nini hawakupa alert au kuwatoa wavamizi Toka Mwanzo? Na kama watu Wana vibali ,iweze iwe Hifadhi ya Barabara?

Mwendazake alikuwa Katilo na asiyefaa.Samia kawalipa Sasa unatakaje?
 
Siyo kazi yake kuangalia watu wanafanyaje. Utakuja sema wakati unafanya uhalifu police walikuwa mbinguni.
Ni kazi yake kwani Hifadhi ya Barabara wanaitumia kwenye kazi yake.Kama sio kazi yake ni kazi ya nani? Unayajua majukumu ya TanRoads?

Acha ujinga,ndio maana laana zimemtoa mapema.
 
Atanaka kiongeza dhambi ajui ni chukizo kwa Mungu.

Ayakumbuke yaliyomkuta yule Mwamba wa awamu ile!
 
Hakuna anaetoa ruhusa ya ujenzi wa makazi kwenye Hifadhi ya Barabara.Kama TanRoads waliingiliwa Kwa nini hawakupa alert au kuwatoa wavamizi Toka Mwanzo? Na kama watu Wana vibali ,iweze iwe Hifadhi ya Barabara?

Mwendazake alikuwa Katilo na asiyefaa.Samia kawalipa Sasa unatakaje?
Mwanzo wa uvamizi ni lini na mwisho wa uvamizi ni lini ili TANROADS iwalipe mwanzo.
 
Back
Top Bottom