PostGE2025 RC Chalamila: Hatukusema Wananchi wakae ndani

PostGE2025 RC Chalamila: Hatukusema Wananchi wakae ndani

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections
Hawakusema mbwa huyo!
Wakati leo wamenizuia minaki nisimpelekee mgonjwa chakula ,
Na mbaya zaidi boda boda baadhi wamepigwa bakora kwenye kizuizi cha minaki.

Hii serikali kwa kifupi hatuitambui wacha iendelee tu na ubabe ila!!!
 
Waziri alizungumzia tz kwa ujumla sasa huyu anazungumzia dar peke yake au inchi nzima.
 
RC Chalamila sio muongo.
Ni kweli, Kauli ya PM alisema "tunashauri wananchi wote ambao hawatakuwa na dharura kubakia nyumbani...." Hotuba ya PM mwigulu ipo mtandaoni hata YouTube.

Hapa kuwa na Amri ya kubaki nyumbani (Kukaa ndani), bali ushauri kwa wasio na dharura ya kutoka.
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amezungumza na Global TV na kuelezea hali ya ulinzi na usalama ilivyo jijini Dar es Salaam. Msikilize alichokisema hususan kuhusu baadhi ya watu ambao hawakuelewa kilichoelezwa na Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba.
 
Maccm yanaruka na kukanyagana haijilikani msemaji wa serikali ni waziri mkuu wakuu wa mikoa au kabitu wa wizara ya habari au kabudi?
 
Ni kweli hakuna sehemu wamesema watu wakae ndani ni wananchi wema wameamua kukaa ndani kuwaacha nyumbu wezi na waharibifu wa mali watoke kufanya maandamano yao uchwara waliyodhamiria lakini nyumbu na zenyewe zimejiongeza
 
Serikali ina kauli za kimitego mitego sana muda mwingine na hii kitu kuna mtu aliweka uzi humu jana
 
Wanaendesha nchi kihuni sana. Jana nilisema humu ndani, wanataka faida za curfew bila kutangaza hiyo curfew waziwazi.

Wanasema wanatoa ushauri ila ni amri ili baadae warudi kama hivi wajisifu nchi ilikuwa imetulia na hatukuwalazimisha watu wakae ndani.

Kesho utawaambia watu tena kwamba unawashauri wakae ndani watakugomea maana watakumbuka uliwahi kusema hivyo baadae ukawaambia haukuwalazimisha kukaa ndani.

Nchi ina ombwe kubwa la kiuongozi. Shida ni kwamba, mtaongoza nchi kwa njia za janja janja kama hivi mpaka lini?
Hakuna mamlaka iliyosema watu wasitoke ndani, muwe mñasikiliza na kuelewa
 
Back
Top Bottom