Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,566
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo ameonya kuwa vyombo vya dola havitakubali kuwaacha baadhi ya watu kuigeuza Arusha sehemu isiyotawalika akisema kuanzia sasa, yeyote atakayejaribu kuvuruga amani na utulivu kwa njia au sababu yoyote atadhibitiwa kikamilifu bila kujali cheo wala itikadi yake kisiasa.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Mulongo alisema: Mtu yeyote atakayechezea amani na utulivu wa Arusha atakiona cha mtema kuni. Huu ni uamuzi wa kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama. Hatuwezi kukubali baadhi ya watu wafanye Arusha isitawalike.
Mkuu huyo wa mkoa ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati hiyo, pia alizungumzia tuhuma kuwa anaingilia utendaji wa baadhi ya idara ikiwamo polisi na mahakama akisema hizo ni tuhuma zisizomnyima usingizi kutekeleza wajibu na majukumu yake kiutendaji na kuongeza kwamba, uwepo wa shughuli za kisiasa ikiwamo mikutano ya hadhara ya vyama, hauwezi kuvuruga mipangilio yake ya kazi.
Alitoa kauli hiyo baada ya juzi kudaiwa kuonekana maeneo ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha asubuhi kabla ya ombi la kutolewa kwa hati ya kumtoa Lema mahabusu, ili awekewe dhamana kukataliwa na hakimu Judith Kamara na hivyo kuzua taharuki miongoni mwa viongozi, wanachama na wapenzi wa Chadema.
Kweli jana (juzi) nilikwenda mahakamani kulingana na ratiba yangu ambayo haiwezi kuvurugwa na uwepo wa Mbowe au shughuli zozote za kisiasa Arusha. Nilikwenda kumsalimia Jaji Mkuu ambaye ni mmoja wa wakuu wa mihimili ya dola aliyeko hapa kwa kazi za kimahakama. Sijaenda kutoa maelekezo Lema anyimwe dhamana na kusema hivyo ni dharau dhidi ya uhuru wa Mahakama, alisema Mulongo.
Mkuu huyo wa mkoa aliwataka viongozi wa Serikali, watendaji na wale wa vyama vya siasa Arusha kujikita katika harakati za kuwaletea maendeleo wananchi badala ya kuendeleza siasa hata baada ya uchaguzi mkuu kumalizika huku akitamba kuwa pamoja na madai kuwa Arusha haitawaliki, bado anaamini mji na mkoa huo kwa ujumla uko shwari baada ya dola kuimarisha ulinzi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Mulongo alisema: Mtu yeyote atakayechezea amani na utulivu wa Arusha atakiona cha mtema kuni. Huu ni uamuzi wa kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama. Hatuwezi kukubali baadhi ya watu wafanye Arusha isitawalike.
Mkuu huyo wa mkoa ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati hiyo, pia alizungumzia tuhuma kuwa anaingilia utendaji wa baadhi ya idara ikiwamo polisi na mahakama akisema hizo ni tuhuma zisizomnyima usingizi kutekeleza wajibu na majukumu yake kiutendaji na kuongeza kwamba, uwepo wa shughuli za kisiasa ikiwamo mikutano ya hadhara ya vyama, hauwezi kuvuruga mipangilio yake ya kazi.
Alitoa kauli hiyo baada ya juzi kudaiwa kuonekana maeneo ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha asubuhi kabla ya ombi la kutolewa kwa hati ya kumtoa Lema mahabusu, ili awekewe dhamana kukataliwa na hakimu Judith Kamara na hivyo kuzua taharuki miongoni mwa viongozi, wanachama na wapenzi wa Chadema.
Kweli jana (juzi) nilikwenda mahakamani kulingana na ratiba yangu ambayo haiwezi kuvurugwa na uwepo wa Mbowe au shughuli zozote za kisiasa Arusha. Nilikwenda kumsalimia Jaji Mkuu ambaye ni mmoja wa wakuu wa mihimili ya dola aliyeko hapa kwa kazi za kimahakama. Sijaenda kutoa maelekezo Lema anyimwe dhamana na kusema hivyo ni dharau dhidi ya uhuru wa Mahakama, alisema Mulongo.
Mkuu huyo wa mkoa aliwataka viongozi wa Serikali, watendaji na wale wa vyama vya siasa Arusha kujikita katika harakati za kuwaletea maendeleo wananchi badala ya kuendeleza siasa hata baada ya uchaguzi mkuu kumalizika huku akitamba kuwa pamoja na madai kuwa Arusha haitawaliki, bado anaamini mji na mkoa huo kwa ujumla uko shwari baada ya dola kuimarisha ulinzi.