sinza pazuri
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 2,525
- 7,377
Rayvanny wewe ni brand kubwa umebeba image ya makampuni makubwa yaliyokuamini yakaweka hela ya kutosha.
Dunia nzima inajua Paula na mama yake ni fungu la kukosa hawana nyota ya pesa na ukikaa nao karibu lazima uzame. Ulifanya vizuri kuwakataa wale matapeli wa mjini.
Tanzania nzima inajua Harmonize aliyumbisha image yake kwa kuendekeza drama za awa kina ndala ndefu mtu na mama yake. Damage control ya lile tukio la kuonesha mashine inamsumbua Konde mpaka leo japo nae ni chenga kichwa maji ila lile tukio ni funzo kwa wasanii wengi maana pale ndio mzee small alianza kupoteza upepo wa pesa akabaki mtafuta likes za insta. Moja ya sababu Hamo kuyumba uchumi ni awa mapacha wawili mtu na mama yake.
Naona Rayvanny balozi wa kampuni kubwa zisizotaka kuhusishwa na uchafu uchafu anataka kunasa kwenye mtego alionasa swahiba wake na wanaume wengi hapa mjini.
Kaa mbali na drama zisizoongeza value kwenye brand yako. Endelea kuwa Rayvanny asiye drama boy. Hao mtu na mama yake ni fungu la kukosa hakuna aliyewai kaa nao karibu akastawi. Marioo ameenda kutafuta nyota ila uchumi mdogo aliokuwa nao soon atatubu. Kuna watu wana nyota za dhiki sio wa kuendekeza. Kuwa muangalifu!