sinza pazuri
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 2,522
- 7,368
Kuna siku niliweka thread nikisema Rayvanny ndio Mangwea wa kizazi cha sasa, wakatokea watu wakanishambulia sana.
Sasa niwaambie movement za sasa za Ray ndio standard tunayopaswa kwenda nayo kama tunataka kutoboa soko la international.
Ukisikia EP yake mpya inaitwa New Chui unaona kabisa hii ndio njia ya kutobolea bongofleva. Ni EP ambayo amejaribu kuunganisha muziki wetu na muziki unaofanya vizuri duniani na bado ukisikia unasema yes hii ndio sanaa yenye quality tunazotaka.
Kuna kasumba kwamba ukiimba kizungu sana utoboi soko la bongo, ila mniamini mimi kama wasanii wakifanya kwa namna ya Rayvanny kwenye new chui mbona watu wataelewa na tutatoboa kotekote nyumbani na mbele.
Btw hongera kwa Rayvanny kupiga show kwenye stage ya MTV Europe.... history uliyoweka ni wajukuu zetu ndio watakuja kukuappreciate.
Wewe ni international level artist, dunia inakuelewa.