ungonella wa ukweli
JF-Expert Member
- Mar 27, 2012
- 4,210
- 556
Mkuu kikatiba mbunge ni msimamizi wa serikali na mshauri wa mambo mbalimbali yanayofanywa na serikali jimboni kwake. Pia mkuu barabara hazijengwi na chama chochote cha siasa. Barabara zinajengwa na serikali kwa kutumia kodi za wananchi wote bila kujali wenye vyama na wasio na vyama. Hivyo lema pia atachangia katika kurejesha mkopo huo kama mtanzania. PIA lema kama mbunge ana mamlaka ya kukagua miradi yote inayojengwa na serikali jimboni kwake sio barabara tu. Hivyo si kweli kwamba kazi ya mbunge ni kujenga barabara!