Ratiba ya mapokezi ya Lema kesho Arusha!

Ratiba ya mapokezi ya Lema kesho Arusha!

Curriculum Specialist

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2007
Posts
2,732
Reaction score
750
Ratiba ya Lema Kesho:

Mapokezi KIA kuanzia Philips saa 2:00 Asubuh

Kwenda kufungua ofisi ya Mbunge kuanzia saa 5:00 Asubuhi

Ukaguzi wa Barabara Zilizojengwa kuanzia saa 6:00 Mchana

Kusalimia akina mama waliomuombea sokoni 7:00 Mchana

Mkutano Kilombero saa 8:00 Mchana

WOOTE MNAKARIBISHWA!

Msafara utakuwa unaongozwa na Wabunge wa Chadema toka Dar es salaam na utahutubiwa na viongozi wa Kitaifa. Msafara huo pia utaongozwa na Helkopta, pikipiki, magari, baiskeli na watembea kwa miguu, maandamano yataanzia Philips hadi ofisi za Mbunge kuelekea viwanja vya kilombero!

Peeoplesssssss!
 
Hiyo ratiba ya kwenda kuwasalimia akina Mama wa soko la NMC itakuwa ya Hisia kali sana, wallahi nasema kuna watu hapo watalia machozi ya damu.

Hawa akina mama kwa mamia ni watu walioteseka sana kwa shuruba za polisi na wagambo wa ccm.

Wamekimbia sana wanawake hawa, wameumizwa, wamepoteza fedha na jewellery, kisa kuwakwepa wagambo wanaowatimua huku wakiwa wamebeba vichwani bidhaa zao.

Akina mama hawa bila kujali kupoteza muda, bila kujali nini kingewatokea, bila kujali dini zao, makabila, ukanda, asili, wala umri, walikusanyika kupiga MAOMBI YA AJABU pale NMc, wakimsihi Mungu atawalaye, asimamie hukumu ya G.Lema ili isiingiliwe na maamuzi ya akili za kibinadamu.

Imagine katika mazingira kama hayo, huyo m'baba kesho anafika eneo hilo kwaajili ya KuWASALIMIA TUakina mama hao.

Ni kipengele kipengele kitakachokuwa na mvuto ajabu.
 
Kibali kimeshaombwa au?

Jihadharini na intellijensia za Polisi. Otherwise nawatakieni heri Arusha
 
Ha ha Nape akisoma hii akawii kusema vurugu za Arusha zimeanza tena.
 
Interenjesia ya KOVA iko vipi,maana hachelewi kusema interenjesia.au mtu kupigwa na kitu chenye ncha kali
 
Hongereni wakuu!! Kila la heri na polisi wakae kando hakuna CDM ina fujo AR. Wakikaa pembeni kila kitu kitaenda salama kabisa ila wakianza kusukuma watu na kurusha vile vya ncha kali tutawashangaa sana.
 
Back
Top Bottom