Rasmi Timu Ya Kagera Sugar Imeshuka Daraja

Rasmi Timu Ya Kagera Sugar Imeshuka Daraja

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
781
Reaction score
1,831
Timu ya Kagera Sugar FC ya mjini Bukoba, imeshuka rasmi daraja na hatutakuwanayo msimu ujao kwenye ligi kuu kufuatia ushindi wa Pamba jiji iliopata leo dhidi ya KenGold FC.

Kwa ushindi wa leo, Pamba jiji imefikisha alama 30 kwenye nafasi ya 11, ikifuatiwa na Tanzania Prisons nafasi ya 12 pointi 30, KMC FC nafasi ya 13 pointi 30, Fountain Gate nafasi ya 14 pointi 29 na Kagera Sugar iko nafasi ya 15 na alama 22.

Kagera Sugar imebakiza mechi mbili ambazo hata ikishinda zote, haiwezi kufikisha alama alizonazo wa juu yake ambaye ni Fountain Gate (29).

Kwahiyo, Kagera Sugar itaungana na KenGold SC kwenye NBC Championship msimu ujao 2025/26 huku Mtibwa Sugar na Mbeya City wakirejea ligi kuu na kuchukua nafasi zao…

Neno moja kwao…..

#NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #KageraSugar #NBCChampionship
 
Lilikuwa ni suala la muda tu, wameponea chupuchupu misimu ya karibuni, hatimaye jahazi limezama...
 
Ule uwezekezaji wa Uwanja pale Kaitaba imebaki White Elephant. Hii ndiyo shida ya Ubinafsi wa Viongozi wetu wa leo.

Jamal Malinzi akiwa Rais wa TFF mradi wa Maana kabisa akaamu kwenda kuuweka kwao ili ndugu zake wafaidi na sasa Uwaanja utabaki shamba la kuvuna Senene tu. Mpaka Kagera aje azinduke Maintanace Cost ya huo Uwanja ni kichomi.
 
Ule uwezekezaji wa Uwanja pale Kaitaba imebaki White Elephant. Hii ndiyo shida ya Ubinafsi wa Viongozi wetu wa leo.

Jamal Malinzi akiwa Rais wa TFF mradi wa Maana kabisa akaamu kwenda kuuweka kwao ili ndugu zake wafaidi na sasa Uwaanja utabaki shamba la kuvuna Senene tu. Mpaka Kagera aje azinduke Maintanace Cost ya huo Uwanja ni kichomi.
Utatumika kwa mechi za championship
 
Kwa kumbukumbu zangu timu kongwe zilizokaa muda mrefu ligi kuu ukiachana na simba na yanga walikua Mtibwa sugar sasa naona na kagera sugar wameshuka, sasa wamebaki Tanzania Prisons ambao washawahi kushuka daraja japo wakapanda mwaka 2005 kama sijakosea na mpaka Leo wapo... timu zingine zilizobaki ni kizazi kipya..
 
Back
Top Bottom