Mchangila Bakari
New Member
- Oct 13, 2017
- 2
- 1
JE KATIBA MPYA NI SULUHISHO??
suala la kupatikana kwa katiba mpya ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ni jambo ambalo limekuwa likisemwa sana kwenye vinywa vya watanzania na kwenye mitandao ya kijamii pia, kuna wengine wanaamini kwamba katiba ya warioba ndio muarobaini wa matatizo au mapungufu yanayotokea na ambayo yataendelea kutokea katika taifa letu.
Binafsi mimi pia ni miongoni mwa watu wanaopenda au wanaotaka katiba yetu ifanyiwe marekebisho kwasababu kwanza katiba hii ni katiba ambayo ilipatikana kipindi ambacho kulikuwa na utawala wa chama kimoja, hivyo katiba ambayo ilipatikana kipindi cha utawala wa chama kimoja haiwezi kuendana na mfumo wa siasa za sasa ambao ni mfumo wa siasa za zinazohusisha vyama vingi, licha ya kuwa muumini wa katiba mpya, bado kuna muda nakosa majibu hasa hasa nikijiuliza kwamba "Je katiba mpya ndio muarobaini wa matatizo ya taifa hili". Kila nikitafakari huwa ninajikuta nakuja na majibu ambayo yanapingana na uumini wangu, na muda mwingine huwa nabadilika na kuanza kuamini kwamba katiba mpya(ya warioba) haiwezi kuwa suluhisho la matatizo ya taifa hili na nitatoa sababu zangu ili nawewe kama utakuwa na mawazo tofauti pia utoe sababu zako kwasababu lengo ni kueleweshana.
Licha ya kuwa muumini wa katiba, bado naamini kwamba katiba sio suluhisho la matatizo yetu, badala yake suluhisho litakuwa ni watu ambao tunawachagua kusimamia katiba husika, kwa maana hiyo kitu cha kwanza tunachotakiwa kufanya ni kuchagua viongozi ambao tunaamini kutoka katika sakafu ya nyoyo zetu kwamba wanauwezo na utayari wa kuiongoza nchi kwa kufuata utaratibu au sheria zetu tulizojiwekea katika taifa letu, nitatoa mifano kadhaa kuthibitisha hili,
Mfano wa kwanza; Katiba yetu ya sasa imehalalisha(imeruhusu) maandamano au mikutano ya kisiasa kwa nchi nzima, lakini kwa sasa jeshi la polisi limepiga marufuku mikusanyiko hiyo endapo mtu atakamatwa akiwa anafanya jambo hili anaweza akaambulia kula virungu vya polisi na na kukamatwa na wakati mwingine kuwekwa ndani, sasa hapa watanzania wenzangu nawaomba munisaidie swali langu kwamba je hapa tatizo ni katiba au tatizo ni jeshi la polisi?? maana katiba imeruhusu ila polisi wamekataza, kwa upande wangu mimi naona katiba sio tatizo.
Mfano wa pili; watu wengi wamekuwa wakilalamika kwamba kuna tatizo kwenye mahakama zetu, kwamba haziko huru hivyo tunahitaji katiba mpya ambayo itaziweka mahakama huru, lakini mimi najiuliza kwamba je tatizo liko kwenye mahakama zetu au tatizo ni watu wengine, kwa mfano juzi mahakama ilitoa order ya kusitisha ubomoaji kwenye baadhi ya maeneo lakini wabomoaji walienda kubomoa, ikumbukwe kwamba mahakama ikishatoa order ndio inakuwa imemealiza kazi yake, mahakama haina jukumu la kwenda kuzuia ubomoaji huo, wanachotakiwa wao ni kutoa "notisi" zuio la mahakama lilipaswa kuheshimiwa na kila mtanzania mpaka amiri jeshi mkuu, sasa kama mahakama imeweza kutoa zuio la ubomoaji wa nyumba halafu wabomoaji wakaenda kubomoa ni sahihi kusema kwamba mahakama haiko huru, kwasababu kwa kutoa tu notisi wanakuwa wameshatimiza wajibu wao, je hapa tatizo ni mahakama au wabomoaji?
Lakini pia wapo watu wengi ambao wamewahi kuishtaki serikali na wakaishinda kupitia hizi hizi mahakama zetu, na mahakama ikasema serikali iwalipe fidia, endapo mahakama itasema serikali iwalipe fidia watu hawa halafu serikali ikakaidi kuwalipa fidia hizo, je tatizo litakuwa liko kwa mahakama?? sasa je tunaposema mahakama haziko huru ni sahihi? gazeti la mwanahalisi liliwahi kufungiwa wakaenda mahakamani na wakashinda, na mahakama ikawaagiza serikali iwalipe fidia, na walishinda kupitia hizi hizi mahakama zetu, sasa tunaposema mahakama haziko huru tunakuwa tunakosea au tuko sahihi??
Kutokana na mifano ambayo nimeieleza hapo juu, na mingine mingi ambayo sijaisema, uumini wangu au imani yangu ya kudai katiba mpya kama suluhisho la matatizo ya taifa hili inazidi kupungua, kwasababu kama kufanya mikutano ya kisiasa ni jambo halali katika katiba yetu lakini leo sehemu hiyo ya katiba inavunjwa, basi ata tukirekebisha hii na tukapata nyingine bora zaidi, mvunjaji akiamua kuvunja ataivunja tu kama anavyoivunja ya sasa.
USHAURI WANGU
Kwanza ifahamike kwamba katiba sio msaafu, inaweza kubadilishwa kwa wakati wowote, ni suala tu la kupeleka muswada bungeni na kama wabunge wengi wakiridhia bas inabadilishwa, hakuna haja ya kubadilisha katiba leo halafu baada ya mwaka mmoja wabunge wa chama fulani wapeleke muswada bungeni wa kubadilisha kipengele fulani cha sheria tulichokiweka leo na wakafanikiwa kwasababu ya wingi wao, kinachotakiwa kufanyika sasa hivi ni wapinzani wakazane kuongeza idadai ya wabunge bungeni, kwanza wawe wengi ili hata tukipata katiba mpya isiwe rahisi kubadilishwa kwa maslahi ya chama fulani, kama sheria ya kuonyesha bunge live ilivyobadilishwa, ndio hivyo hivyo katiba mpya ambayo tutaipata itawezwa kubadilishwa tena kama wabunge wa chama kimoja watazidi kuwa wengi bungeni kwa maslahi ya chama chao.
Kwasasa hakuna haja ya wapinzani kuwekeza nguvu nyingi kwenye kuurafuta uraisi au kudai kwamba matokeo ya uraisi yaweze kupingwa mahakani, sasa hivi kuna malalamiko kwamba wagombea wa upinzani wa nafasi ya ubunge wengi waliporwa ushindi wao na wakati huo huo matokeo ya ubunge yanaweza kupingwa mahakamani, kwanini wasianze kwa kupigania haki za hawa wabunge walioporwa haki zao katika mahakama, kama wameshindwa kuwapigania hawa wabunge mahakamani na wakapa haki, endapo matokeo ya uraisi yakiruhusiwa kupingwa mahakamani wataweza kuyapinga???
Watuaminishe kwanza kwa wabunge halafu ndio waje waseme wanataka kupinga matokeo ya uraisi mahakamani.
Lakini ni mawazo yangu tu nawewe pia unaweza ukatoa yako.
Na Mchangila Bakari.
suala la kupatikana kwa katiba mpya ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ni jambo ambalo limekuwa likisemwa sana kwenye vinywa vya watanzania na kwenye mitandao ya kijamii pia, kuna wengine wanaamini kwamba katiba ya warioba ndio muarobaini wa matatizo au mapungufu yanayotokea na ambayo yataendelea kutokea katika taifa letu.
Binafsi mimi pia ni miongoni mwa watu wanaopenda au wanaotaka katiba yetu ifanyiwe marekebisho kwasababu kwanza katiba hii ni katiba ambayo ilipatikana kipindi ambacho kulikuwa na utawala wa chama kimoja, hivyo katiba ambayo ilipatikana kipindi cha utawala wa chama kimoja haiwezi kuendana na mfumo wa siasa za sasa ambao ni mfumo wa siasa za zinazohusisha vyama vingi, licha ya kuwa muumini wa katiba mpya, bado kuna muda nakosa majibu hasa hasa nikijiuliza kwamba "Je katiba mpya ndio muarobaini wa matatizo ya taifa hili". Kila nikitafakari huwa ninajikuta nakuja na majibu ambayo yanapingana na uumini wangu, na muda mwingine huwa nabadilika na kuanza kuamini kwamba katiba mpya(ya warioba) haiwezi kuwa suluhisho la matatizo ya taifa hili na nitatoa sababu zangu ili nawewe kama utakuwa na mawazo tofauti pia utoe sababu zako kwasababu lengo ni kueleweshana.
Licha ya kuwa muumini wa katiba, bado naamini kwamba katiba sio suluhisho la matatizo yetu, badala yake suluhisho litakuwa ni watu ambao tunawachagua kusimamia katiba husika, kwa maana hiyo kitu cha kwanza tunachotakiwa kufanya ni kuchagua viongozi ambao tunaamini kutoka katika sakafu ya nyoyo zetu kwamba wanauwezo na utayari wa kuiongoza nchi kwa kufuata utaratibu au sheria zetu tulizojiwekea katika taifa letu, nitatoa mifano kadhaa kuthibitisha hili,
Mfano wa kwanza; Katiba yetu ya sasa imehalalisha(imeruhusu) maandamano au mikutano ya kisiasa kwa nchi nzima, lakini kwa sasa jeshi la polisi limepiga marufuku mikusanyiko hiyo endapo mtu atakamatwa akiwa anafanya jambo hili anaweza akaambulia kula virungu vya polisi na na kukamatwa na wakati mwingine kuwekwa ndani, sasa hapa watanzania wenzangu nawaomba munisaidie swali langu kwamba je hapa tatizo ni katiba au tatizo ni jeshi la polisi?? maana katiba imeruhusu ila polisi wamekataza, kwa upande wangu mimi naona katiba sio tatizo.
Mfano wa pili; watu wengi wamekuwa wakilalamika kwamba kuna tatizo kwenye mahakama zetu, kwamba haziko huru hivyo tunahitaji katiba mpya ambayo itaziweka mahakama huru, lakini mimi najiuliza kwamba je tatizo liko kwenye mahakama zetu au tatizo ni watu wengine, kwa mfano juzi mahakama ilitoa order ya kusitisha ubomoaji kwenye baadhi ya maeneo lakini wabomoaji walienda kubomoa, ikumbukwe kwamba mahakama ikishatoa order ndio inakuwa imemealiza kazi yake, mahakama haina jukumu la kwenda kuzuia ubomoaji huo, wanachotakiwa wao ni kutoa "notisi" zuio la mahakama lilipaswa kuheshimiwa na kila mtanzania mpaka amiri jeshi mkuu, sasa kama mahakama imeweza kutoa zuio la ubomoaji wa nyumba halafu wabomoaji wakaenda kubomoa ni sahihi kusema kwamba mahakama haiko huru, kwasababu kwa kutoa tu notisi wanakuwa wameshatimiza wajibu wao, je hapa tatizo ni mahakama au wabomoaji?
Lakini pia wapo watu wengi ambao wamewahi kuishtaki serikali na wakaishinda kupitia hizi hizi mahakama zetu, na mahakama ikasema serikali iwalipe fidia, endapo mahakama itasema serikali iwalipe fidia watu hawa halafu serikali ikakaidi kuwalipa fidia hizo, je tatizo litakuwa liko kwa mahakama?? sasa je tunaposema mahakama haziko huru ni sahihi? gazeti la mwanahalisi liliwahi kufungiwa wakaenda mahakamani na wakashinda, na mahakama ikawaagiza serikali iwalipe fidia, na walishinda kupitia hizi hizi mahakama zetu, sasa tunaposema mahakama haziko huru tunakuwa tunakosea au tuko sahihi??
Kutokana na mifano ambayo nimeieleza hapo juu, na mingine mingi ambayo sijaisema, uumini wangu au imani yangu ya kudai katiba mpya kama suluhisho la matatizo ya taifa hili inazidi kupungua, kwasababu kama kufanya mikutano ya kisiasa ni jambo halali katika katiba yetu lakini leo sehemu hiyo ya katiba inavunjwa, basi ata tukirekebisha hii na tukapata nyingine bora zaidi, mvunjaji akiamua kuvunja ataivunja tu kama anavyoivunja ya sasa.
USHAURI WANGU
Kwanza ifahamike kwamba katiba sio msaafu, inaweza kubadilishwa kwa wakati wowote, ni suala tu la kupeleka muswada bungeni na kama wabunge wengi wakiridhia bas inabadilishwa, hakuna haja ya kubadilisha katiba leo halafu baada ya mwaka mmoja wabunge wa chama fulani wapeleke muswada bungeni wa kubadilisha kipengele fulani cha sheria tulichokiweka leo na wakafanikiwa kwasababu ya wingi wao, kinachotakiwa kufanyika sasa hivi ni wapinzani wakazane kuongeza idadai ya wabunge bungeni, kwanza wawe wengi ili hata tukipata katiba mpya isiwe rahisi kubadilishwa kwa maslahi ya chama fulani, kama sheria ya kuonyesha bunge live ilivyobadilishwa, ndio hivyo hivyo katiba mpya ambayo tutaipata itawezwa kubadilishwa tena kama wabunge wa chama kimoja watazidi kuwa wengi bungeni kwa maslahi ya chama chao.
Kwasasa hakuna haja ya wapinzani kuwekeza nguvu nyingi kwenye kuurafuta uraisi au kudai kwamba matokeo ya uraisi yaweze kupingwa mahakani, sasa hivi kuna malalamiko kwamba wagombea wa upinzani wa nafasi ya ubunge wengi waliporwa ushindi wao na wakati huo huo matokeo ya ubunge yanaweza kupingwa mahakamani, kwanini wasianze kwa kupigania haki za hawa wabunge walioporwa haki zao katika mahakama, kama wameshindwa kuwapigania hawa wabunge mahakamani na wakapa haki, endapo matokeo ya uraisi yakiruhusiwa kupingwa mahakamani wataweza kuyapinga???
Watuaminishe kwanza kwa wabunge halafu ndio waje waseme wanataka kupinga matokeo ya uraisi mahakamani.
Lakini ni mawazo yangu tu nawewe pia unaweza ukatoa yako.
Na Mchangila Bakari.