Rangi ya Plate number za mabasi ya shule

Rangi ya Plate number za mabasi ya shule

Joined
Oct 26, 2018
Posts
21
Reaction score
25
Habari wakuu,
Naomba kujua kwa mabasi ya shule inabidi yawe na plate number za njano ama plate number nyeupe? Naona baadhi ya magari yana rangi nyeupe na mengine njano.
 
kubeba watoto wa shule inayofanya huduma ya elimu hapo hakuna namna ya biashara?
Nadhani, Kama shule inakodi hilo gari kutoka kwa mtu au taasisi nyingine hapo ndo litahitajika kuweka number plates nyeupe.

Jiulize je basi hilo nikilitumia kubeba wafanyakazi wangu wanaofanya kazi kwenye biashara zangu itanilazimu staff bus yangu iwe na number plate nyeupe???
 
Uhalisia school bus ni gari la biashara sababu hao wanafunzi wanalipia nauli kwa mwezi hata kama linamilikiwa na shule yenyewe!
 
Uhalisia school bus ni gari la biashara sababu hao wanafunzi wanalipia nauli kwa mwezi hata kama linamilikiwa na shule yenyewe!
sio kila gari inayotumika kwenye biashara lazima iwe na namba nyeupe. Mfano wenye maduka ambao wanafanya deliveries mbona gari zao haziwi na number plates nyeupe? Au mfano malori haya si magari ya biashara kwanini hayawekwi number plates nyeupe?
 
sio kila gari inayotumika kwenye biashara lazima iwe na namba nyeupe. Mfano wenye maduka ambao wanafanya deliveries mbona gari zao haziwi na number plates nyeupe? Au mfano malori haya si magari ya biashara kwanini hayawekwi number plates nyeupe?
Kuhusu malori (HGV) sina hakika kama yanahusika na hii sheria ila cases zingine inakuwa ni ukaidi tu na ni kosa!

Noah na Probox/Succeed zishapigwa marufuku kubeba abiria baadhi ya mikoa na hawapewi vibao vyeupe ila zimejaa na vibao vya njano zinapiga routes!
 
Kuhusu malori (HGV) sina hakika kama yanahusika na hii sheria ila cases zingine inakuwa ni ukaidi tu na ni kosa!

Noah na Probox/Succeed zishapigwa marufuku kubeba abiria baadhi ya mikoa na hawapewi vibao vyeupe ila zimejaa na vibao vya njano zinapiga routes!
Hao wa probox wanakiuka kweli taratibu wanatumia gari iliyosajiliwa kwa matumizi ya binafsi kufanya biashara
Ila hapo kwenye school bus naamini hailazimiki kuwa na namba za biashara kama gari hiyo haijakodishwa kutoka kwa mtu baki. Maana ikiwa hivyo itakuwa haileti mantiki; Yaani niwe na basi la matumizi ya shule yangu, likibeba walimu (wafanyakazi wangu) liwe na namba za njano. Ila likibeba wanafunzi wangu kwakuwa ni (wateja) liwe na namba nyeupe. Ni sawa na uniambie nisitumie gari yangu binafsi kumfanyia delivery mteja kwakuwa ina namba za njano huku inaninufaisha kwenye biashara.
 
Habari wakuu,
Naomba kujua kwa mabasi ya shule inabidi yawe na plate number za njano ama plate number nyeupe? Naona baadhi ya magari yana rangi nyeupe na mengine njano.
Kuna makampuni yanakodisha magari na tunatumia kwa muda unaotaka as long as unalipia monthly. So ukiona plate nyeupe jua gari ya biashara au ilokodishwa kwa shule na kampuni za ukodishaji. Ukiona ya njano jua inamilikiwa na shilika husika(shule).
 
Back
Top Bottom