Rais wa Zambia: Nimekuta hazina haina fedha kabisa

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,947
141,925
Rais wa Zambia aliyechaguliwa hivi karibuni na kuapishwa juzikati kwa mbwembwe na vigelegele amedai ameikuta Hazina ya nchi nyeupe yaani haina fedha.
===
Rais mpya wa Zambia ameambia BBC kwamba amerithi hazina "tupu", wakati " kiasi cha kutisha" cha pesa kikiibwa.

"Watu bado wanajaribu kuhamisha fedha hata dakika hizi za mwisho hatua ambayo hairuhusiwi kwani pesa hizo sio zao," Rais Hakainde Hichilema alisema.

Alimshinda mpinzani wake Edgar Lungu katika uchaguzi wa urais mwezi uliopita.

Bwana Hichilema hakutaja maafisa wowote. Bwana Lungu hapo awali alikanusha makosa yote.

BBC imetka tamko kutoka kwa chama chake. Bwana Lungu aliliongoza taifa hilo lenye utajiri wa shaba tangu 2015. Alisifiwa sana kwa mabadiliko mazuri ya madaraka kwenda kwa Bwana Hichilema, ambaye alishinda urais baada ya majaribio matano bila kufaulu

Deni kamili ‘halijafichuliwa’
Bwana Hichilema alishinda uchaguzi huo kwa ahadi ya kukabiliana na ufisadi, na kumaliza mgogoro wa kiuchumi ambao umesababisha deni la Zambia kuongzeka .

Katika mahojiano na BBC, rais mpya alielezea hazina hiyo kuwa "tupu kabisa".

Aliongeza kuwa "shimo ni kubwa zaidi kuliko tulivyotarajia" na hali ya deni ilikuwa "haijafichuliwa kabisa" na serikali ya zamani.

"Kuna uharibifu mwingi, kwa bahati mbaya," Bwana Hichilema alisema.

Aliongeza kuwa serikali yake "haitovumilia kabisa" ufisadi, na itachunguza alichokiita harakati zinazokiuka sheria za kuhamisha fedha .

"Sitaki kusema mengi ... tunachokichukua ni cha kutisha," rais alisema.

"Utahisi hakuna mtu anayeweza kufanya kitu kama hicho lakini inafanyika. Watu wamefanya hivyo. Bado wanajaribu kufanya hata sasa."

Bwana Hichilema ameteua mchumi na mshauri wa zamani wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Situmbeko Musokotwane kama waziri wa fedha.

"Iiwapo hatutafanya chochote kwa bajeti, basi bajeti itakuwa hasa kwa ajili ya kulipa mishahara na pia kulipia madeni," Bw Musokotwane alinukuliwa na shirika la habari la Reuters akisema mara tu baada ya kuteuliwa.

Zambia inadaiwa wastani wa $ 12bn (£ 8.6bn), ripoti za awali zilisema.

Inatumia angalau 30% ya mapato yake kwa malipo ya riba, kulingana na kampuni ya viwango vya mkopo S&P Global.

Mwaka jana, Zambia ilikosa ulipaji wa riba, na kuifanya kuwa nchi ya kwanza ya Kiafrika kukosa kulipa mkopo wakati wa janga la Corona .

Pia inakabiliwa na ugumu wa kulipa mikopo mingine

Chanzo: BBC
 
Rais wa Zambia aliyechaguliwa hivi karibuni na kuapishwa juzikati kwa mbwembwe na vigelegele amedai ameikuta Hazina ya nchi nyeupe yaani haina fedha.

Source: BBC
Una kichwa kibovu, sasa maneno ya mbwembwe na vigelegele yanatoka wapi? umeyaandika kama kejeli vile.... It is as if you are blaming him for this bancrapcy! Amekuta hakuna kitu jikoni, basi simple!
 
wanafikiri kuongoza hizi nchi za Africa ni kazi rahisi sana, utafanya hivi mara vile nchi itaendelea overnight na watu kuishi kama ulaya.

Maendeleo yana stages, na stage ngumu sana ambayo Africa bado hatujaiapply tumeiruka na bado hatutaki kuambiwa ukweli ni KUFANYA KAZI KWA BIDII TUKIJENGA NCHI ZETU KWA JACHO NA DAMU...
 
wanafikiri kuongoza hizi nchi za Africa ni kazi rahisi sana, utafanya hivi mara vile nchi itaendelea overnight na watu kuishi kama ulaya.

Maendeleo yana stages, na stage ngumu sana ambayo Africa bado hatujaiapply tumeiruka na bado hatutaki kuambiwa ukweli ni KUFANYA KAZI KWA BIDII TUKIJENGA NCHI ZETU KWA JACHO NA DAMU...
Mwendazake alijaribu hio njia, Alitukanwa sana
 
Mwendazake alijaribu hio njia,Alitukanwa sana

hana kwenye ukuaji binadamu ukiruka stage lazima huko mbele ikusumbue maana "Life is the process" pia...ndivyo ilivyo pia hata kwenye maendeleo, kuna stages zake, zipo ngumu na rahisi.. ili uzifikie zile rahisi lazima upitie stages ngumu kwanza ikiwemo watu kufanya kazi kwa bidii ikiwezekana kufa kabisa, watu kuacha siasa kwanza, vipindi vya utawala kwa mtu mmoja viwe vya muda mrefu, wapumbavu na wajinga wauwawe nk....ukivuka hizo stages ndio zinakuja stages rahisi sasa....demokrasia, uhuru wa kuongea, watu kulipa kodi bila shuruti nk...
 
Habari mbona fupi sana!?
Zambia ina deni lilosimama kwenye dola Bilioni 12.8

Njia pekee ni kubinya zaidi yaani "austerity measures" ambazo zitaleta zahma zaidi na wananchi wataanza kelele.

Kumpatia kitita cha kuanza kazi IMF wamemwambia atengeneze upya mfumo wa mishahara serikalini, aongeze bei ya mafuta ya petroli na dizeli,

Hiyo yaitwa "debt restructure plan" ambayo yaendana na masharti yao hao IMF.

Hivyo wazambia tarajie maamuzi magumu na yasiyo rafiki kuikomboa nchi hiyo.

Kwenye kubadili sera za madini ni kuendana na mabadiliko ya matumizi ya mawe ( battery) badala ya madini kama Copper ili kupunguza uazi joto duniani.

Nchi kama Marekani, Uingereza na zingine tayari zinajiandaa kuanza kutengeneza hayo mawe kuanzia mwaka 2030 hivyo magari mengi yatatengenezwa ya kutumia umeme wa batteries.

Magari mengi ya umeme yanatumia Copper kwa wingi hivyo kudai uzalishaji mwingi.

Hivyo kwa kuwa Mchina tayari yupo pale nchi za magharibi zitajaribu kuisaidia Zambia kurekebisha sheria zake za madini kwa manufaa ya Zambia.

Hivyo Mr HH anahitaji "stable policies" kwa wawekezaji wa nje na kuwasadia ndugu zetu wale "jerabos" ambao ni wachimbaji wadogo lakini wenye nguvu kubwa nchini Zambia.
 
Rais wa Zambia aliyechaguliwa hivi karibuni na kuapishwa juzikati kwa mbwembwe na vigelegele amedai ameikuta Hazina ya nchi nyeupe yaani haina fedha.
===
Rais mpya wa Zambia ameambia BBC kwamba amerithi hazina "tupu", wakati " kiasi cha kutisha" cha pesa kikiibwa.

"Watu bado wanajaribu kuhamisha fedha hata dakika hizi za mwisho hatua ambayo hairuhusiwi kwani pesa hizo sio zao," Rais Hakainde Hichilema alisema.

Alimshinda mpinzani wake Edgar Lungu katika uchaguzi wa urais mwezi uliopita.

Bwana Hichilema hakutaja maafisa wowote. Bwana Lungu hapo awali alikanusha makosa yote.

BBC imetka tamko kutoka kwa chama chake. Bwana Lungu aliliongoza taifa hilo lenye utajiri wa shaba tangu 2015. Alisifiwa sana kwa mabadiliko mazuri ya madaraka kwenda kwa Bwana Hichilema, ambaye alishinda urais baada ya majaribio matano bila kufaulu

Deni kamili ‘halijafichuliwa’
Bwana Hichilema alishinda uchaguzi huo kwa ahadi ya kukabiliana na ufisadi, na kumaliza mgogoro wa kiuchumi ambao umesababisha deni la Zambia kuongzeka .

Katika mahojiano na BBC, rais mpya alielezea hazina hiyo kuwa "tupu kabisa".

Aliongeza kuwa "shimo ni kubwa zaidi kuliko tulivyotarajia" na hali ya deni ilikuwa "haijafichuliwa kabisa" na serikali ya zamani.

"Kuna uharibifu mwingi, kwa bahati mbaya," Bwana Hichilema alisema.

Aliongeza kuwa serikali yake "haitovumilia kabisa" ufisadi, na itachunguza alichokiita harakati zinazokiuka sheria za kuhamisha fedha .

"Sitaki kusema mengi ... tunachokichukua ni cha kutisha," rais alisema.

"Utahisi hakuna mtu anayeweza kufanya kitu kama hicho lakini inafanyika. Watu wamefanya hivyo. Bado wanajaribu kufanya hata sasa."

Bwana Hichilema ameteua mchumi na mshauri wa zamani wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Situmbeko Musokotwane kama waziri wa fedha.

"Iiwapo hatutafanya chochote kwa bajeti, basi bajeti itakuwa hasa kwa ajili ya kulipa mishahara na pia kulipia madeni," Bw Musokotwane alinukuliwa na shirika la habari la Reuters akisema mara tu baada ya kuteuliwa.

Zambia inadaiwa wastani wa $ 12bn (£ 8.6bn), ripoti za awali zilisema.

Inatumia angalau 30% ya mapato yake kwa malipo ya riba, kulingana na kampuni ya viwango vya mkopo S&P Global.

Mwaka jana, Zambia ilikosa ulipaji wa riba, na kuifanya kuwa nchi ya kwanza ya Kiafrika kukosa kulipa mkopo wakati wa janga la Corona .

Pia inakabiliwa na ugumu wa kulipa mikopo mingine

Source: BBC
HH hana haja ya kulalamika bali kumkamata Edgar Lungu na mawaziri wake ili wamuonyeshe ilipokwenda fedha ya umma. SImpo.
 
Back
Top Bottom