Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Rais wa Klabu ya Yanga, Injinia Hersi Said leo Jumamosi, Juni 28, 2025 amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuwania nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Kigamboni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Hersi amechukua fomu hiyo katika Ofisi ya CCM Kigamboni na amekabidhiwa na Katibu wa CCM wa Kigamboni, Stanley Mkandawire.
"Nikiwa kama mwanachama wa CCM nimekuja kutekeleza haki yangu ya kikatiba ya kupata nafasi ya kuchaguliwa na nimekuja kuchukua fomu ya kuomba ridhaa kwa kugombea nafasi ya Ubunge kuwakilisha Jimbo la Kigamboni," amesema Injinia Hersi.
"Nikiwa kama mwanachama wa CCM nimekuja kutekeleza haki yangu ya kikatiba ya kupata nafasi ya kuchaguliwa na nimekuja kuchukua fomu ya kuomba ridhaa kwa kugombea nafasi ya Ubunge kuwakilisha Jimbo la Kigamboni," amesema Injinia Hersi.