Rais wa Ushelsheli atangaza hali ya dharura kufuatia mafuriko na mlipuko

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,502
9,282
Rais Wavel Ramkalawan wa Ushelsheli ametangaza hali ya tahadhari Alhamisi, akiwaamuru raia wote isipokuwa wafanyakazi muhimu kubaki nyumbani, baada ya mlipuko katika duka moja la vilipuzi na mafuriko kutokana na mvua kubwa.

Taarifa ya Ikulu mjini Victoria, imetolewa kufuatia mlipuko mkubwa kwenye duka la vilipuzi la CCCL katika mtaa wa viwanda kwenye kisiwa kikuu cha Mahe na kusababisha uharibifu mkubwa na kumsababisha rais kutangaza hali ya dharura.

Shule zote zimefungwa na wafanyakazi wa idara muhimu tu na watu wanaosafiri ndio wanaruhusiwa kutembea kwa nafasi. Hii ni kuruhusu idara za dharura kutekeleza kazi muhimu taarifa hiyo iliongeza.

Ushelsheli ambayo ni kituo muhimu cha utali ina jumla ya visiwa 115 na wakazi wapatao 100,000 kwenye bahari ya Hindi, mashariki mwa Afrika.

VOA Swahili
 
  • Thanks
Reactions: PFA
Back
Top Bottom