Rais wa Msumbiji kwanini haongei Kiswahili?

Rais wa Msumbiji kwanini haongei Kiswahili?

Atahutubia bunge leo kwa lugha gani?
 
Raisi wenywewe wenzake wakija kwetu kama yule raisi wa china alikuwa anaongea kichina raisi aliongea kiingereza ni aibu
 
Kichekesho cha nchi hii bana. unakuta kiongozi analazimisha sijui wanafunzi wajifunze kiswahili yeye anapeleka watoto wake kwenye shule ya kiingereza. Ajira zikitoka wanapewa wale wanaoujua kiingereza kwanza!!!
 
Jamani acheni majungu kwani Kireno ni lugha ya asili ya Msumbuji? Yeye Katumia Kireno wa kwetu Kiingereza tatizo liko wapi? Wote wametumia lugha za kikoloni. Kwa hiyo basi wote wawili wamekuwa influenced na cultural imperialism mmoja anamtukuza bawana wake mreno na mwenzake anamtukuza bwaba wake Mwingereza hapo ngoma draw. Kama Rais wa Msumbiji angeongea kimakonde ningeona kuna pointi lakini kwa sasa prezida wetu hajafanya kosa lolote. Wao wanajitutumua kwa Kireno na sisi tuna jitutumua kwa Kiingereza. Chezea sisi wewe!
Huyu rais wa Msumbiji nasikia elimu ya msingi ameipata hapa Tanzania, kwanini hatakikuongea Kiswahili?.

Anaongea lugha ya kwao tu, lakini viongozi wetu wanaongea kiingereza badala ya kiswahili.

Mgeni akija kwetu ningependa Rais wetu nae aongee kiswahili ili huyo mgeni aelewe kupitua mkalimani, sio kupiga makelele tu kuhamasisha kiswahili kwa Maneno, tunataka vitendo na kiongozi mkuu wa nchi Rais, yeye ndio awe mfano.
 
Nilijisikia vibaya sana juzi my prezidaa kazungumza kingereza
Sijapenda kwa kweli acha tu niwe mkweli kwa hili


kazungumza kiingereza halafu akawa anakosea kusoma..alibabaika sana kutamka neno institutionalize..plus kile kigugumizi ni sheeeedaaaa
 
kiswahili ni lugha ya sokoni. mambo ya kitaalam hayaongeleki kwa kiswahili
 
Kichekesho cha nchi hii bana. unakuta kiongozi analazimisha sijui wanafunzi wajifunze kiswahili yeye anapeleka watoto wake kwenye shule ya kiingereza. Ajira zikitoka wanapewa wale wanaoujua kiingereza kwanza!!!

Ajabu sana mkuu.
 
JK kwa nini haongei Kireno?

Jk, hajui kireno, huyo wa msumbiji anajua kiswahili vizuri, na hata elimu ya msingi ameipata hapahapa, tena yeye ni mgeniwetu ingekuwa vizuri akaongea kiswahili ilikuinyesha heshima katika nchi aliyo kulia.
Alie haribu zaidi ni huyu wakwetu kwa kutoongea kiswahili karibu kila mikutano inayo fanyika hapa nchini kwetu.
 
Jamani acheni majungu kwani Kireno ni lugha ya asili ya Msumbuji? Yeye Katumia Kireno wa kwetu Kiingereza tatizo liko wapi? Wote wametumia lugha za kikoloni. Kwa hiyo basi wote wawili wamekuwa influenced na cultural imperialism mmoja anamtukuza bawana wake mreno na mwenzake anamtukuza bwaba wake Mwingereza hapo ngoma draw. Kama Rais wa Msumbiji angeongea kimakonde ningeona kuna pointi lakini kwa sasa prezida wetu hajafanya kosa lolote. Wao wanajitutumua kwa Kireno na sisi tuna jitutumua kwa Kiingereza. Chezea sisi wewe!

Msumbiji kireno nikama lugha ya taifa, wamakonde karibu woote wa msumbiji wanajua kireno. Kwahiyo kuongea kwake kireno sio bahati mbaya, naamini huenda hata hicho kimakonde hakijui kama anavyo jua kireno kwahiyo yeye kwake ni fahari kuongea kireno.
 
huyo mshakaji anapiga kiswahili kuliko hata wengi wetu humu tena kilichoiva. nampendea tu yuko karibu sana na watz hata most his friends are ze bongos hata kabla ya kuingia madarakani
 
Msumbiji kireno nikama lugha ya taifa, wamakonde karibu woote wa msumbiji wanajua kireno. Kwahiyo kuongea kwake kireno sio bahati mbaya, naamini huenda hata hicho kimakonde hakijui kama anavyo jua kireno kwahiyo yeye kwake ni fahari kuongea kireno.

kimakonde anapiga sana tu ila nashindwa elewa kwanini hawaelewani na guebuza maana hata wakat wa kura za maonj waliondoka wamenunuiana
 
Jk, hajui kireno, huyo wa msumbiji anajua kiswahili vizuri, na hata elimu ya msingi ameipata hapahapa, ...
Kusoma hapa Tanzania hakuhalalishi kujua Kiswahili. Kuna shule nyingi tu zinatumia syllabus za kigeni ikiwa ni pamoja na lugha ya kufundishia. Raisi Nyusi wa Msumbiji alisoma shule ya Msingi Frelimo iliyopo wilayani Tunduru na baada ya hapo alirudi kwao kwa masomo ya sekondari na kuendelea. Ni vyema ukajiridhisha kama hiyo Frelimo Primary School ilikuwa inatoa elimu kwa kutumia lugha gani!
 
Hivi issue hasa inayojadiliwa hapa ni nini?
 
Huyo Rais inawezekana anajua Kiswahili cha kawaida ila sio kwa maneno ya kiufundi(technical terms)

Mfano akitaka kusema Mswada wa sheria inawezekana akawa hana huo msamiati,itabidi aseme Bill of Law. Hapo ndio inambidi atumie lugha ambayo yuko comfortable nayo,Kireno.

Vile vile JK akisema aongee Kiswahili anaweza 'mpoteza' mwenzie linapokuja suala la msamiati wa kiswahili mgumu.
Naona ni sahihi JK anapotumia English kwa vile ninaamini Nyusi anajua Kireno zaidi kisha Kiingereza kisha Kiswahili (sijahusisha lugha zake nyingine) hivyo basi English ni 'common languaje' kwao kuelewana.
 
Kama ni hivyo kwa nini kimakonde ambacho kinajulikana na wengi kisiwe lugha ya taifa kama sisi kilivyo Kiswahili despite our ethnic diversity? Kumbuka Kiswahili hapo awali ilikuwa lugha iliyokuwa ikifahamika na kutumiwa zaidi na Waswahili yaani watu wa mwambao wa pwani ya hindi. Baadaye wakati wa kupigania uhuru kilitumika kama Lingua Franca kutuunganisha watu wote. Kama Kimakonde kinafahamika na watu wengi wa Msumbiji kwa kini kisiwe promoted kama Kiswahili na kutumika kama lugha ya taifa? Hapo ndugu yangu kuna ukoloni mamboleo tutake tusitake. Kwa nini mtu aone ufahari kutumia Kireno badala ya kimakonde? Kwa mtazamo wangu Kireno na Kiingereza vyote vina status sawa kwamba ni lugha za wakoloni. Kumbuka mtumwa humwabudu sana bwana wake. Acha tu tuwaabudu maana ni mabwana zetu!
 
Wakati mwingine kama sio mara zote hii inatokana na Mkalimani! Je, wakati tunamtaka JK azungumze Kiswahili, huyo Mkalimanyi anakifahamu Kiswahili vizuri?
 
Back
Top Bottom