"Rais wa misiba"

Ona sasa...mwingine huyu kimsingi anasema haoni ubaya wa Magufuli kutokwenda la kama angekuwa na uwezo wa kufufua watu.

Kwake cha muhimu zaidi ni kuangalia namna ya kuepusha ajali kama hiyo iliyotokea....

Lakini si ajabu nawe ukaitwa mkabila.....
Sasa rais hatakikusikia habari mbaya, kashasema hilo.

Mnataka kumlazimisha?

Kama hamumtaki rais wa hivyo mtoeni.

Rais mwenyewe msema ovyo, si ajabu akaja msibani na kusema maneno ya ovyo na kuzua mjadala hasi.

Sijaona Magufuli kwa roho yake ya korosho angefanya nini cha ziada kwenye msiba huo.

Ndiyo maana nikasema labda kama angekuwa ana uwezo wa kufufua watu ningeona ana umuhimuwa kuwepo.

Zaidi ni kuingiza siasa katika msiba tu. Tushaona kina Lema wanazozana na uongoziwa CCM kuweka siasa katika msiba.

Mimi mtu atakayeihoji serikali ya Magufuli inafanya nini kuhakikisha ajali hizi zinadhibitiwa nitamuona anafanya la maana kuliko anayehojikwa nini Magufuli hajaenda msibani.

Hususan kwa sababu kuna muwakilishi mkubwa sana wa serikali kaenda, makamu wa rais.

Kwa hiyo hatuwezi kusema serikali ngazi ya taifa imesusa kwenda msibani.

Kwani lazima msibani aende Magufuli? Tunajuaje kama rais na Makamu hawajagawana majukumu na Makamu kupewa jukumu la kufariji misibani wakati rais anaendelea na kazi nyingine kuhakikisha hiyo misiba haijirudii?
 
Sasa nimeelewa kwa nini kwenye kutoa maoni ya kipima joto wanataka uchague 'Ndio, Hapana au Sijui' maana hawakosi watakaokubali, watakaokataa ama wengine wao hawana la kusema.

Ahahaaaaa....umenichekesha sana aisee.

Sasa kwa taarifa yako, humu humu JF kuna watu washalalamika kwa nini hata huwa wanaweka huo uchaguzi wa 'sijui'.

Kuna watu huwa wanadai hakuna sababu ya kuweka huo uchaguzi [option] maana kwao eti jibu ni lazima liwe la 'ndiyo' au 'hapana' tu.

Binadamu ndivyo tulivyo...haturidhiki hata iweje.

Nina uhakika kabisa kama Magufuli angeenda leo kuna ambao wangelalamika kwa nini kaenda.

Kwanza tayari kuna wanaosema ni bora hajaenda...papo hapo wengine wanamlaani kwa kutokwenda.
 
Watu 32 ni wengi mno,wengi wakiwa wanafunzi wadogo!!Hakuna justification ya Rais kukosa msiba huu!
 

Nakubaliana nawe.

Serikali ngazi ya taifa kweli ilikuwepo.

Na kuhusu serikali inafanya nini kupunguza hizi ajali za kizembe ambazo naamini zinaepukika hata kwangu hilo ndo la msingi zaidi.

Ila mwisho wa siku naamini kuwa, kwenye baadhi ya situations optics matter....it would have been a good thing for him to show up.
 
Kuwa na adabu bac usipende kulaum tu kwan makamu. Wake aliye enda hatoshi hadi liende baraza zima la viongoz kumbuka kuwa nawew pengine hujaenda na kama umeenda shida yako ilikuwa ni kwenda msibani au kuangalia walo hudhuria?
 
Watu 32 ni wengi mno,wengi wakiwa wanafunzi wadogo!!Hakuna justification ya Rais kukosa msiba huu!

Ni kweli.

Na ndiyo maana kama umenisoma vizuri na kuelewa ulichokisoma utaona nimesema kuwa ingekuwa ni vyema kama yeye mwenyewe angeenda kwenye hiyo hafla ya kuwaaga hao maiti.
 
Tatizo moja kubwa la nchi za dunia ya tatu kiujumla, na Africa hususan, ni wananchi kuwaangalia viongozi si kama vijakazi wao, bali kama waokozi wao.

Hivyo badala ya watu kuweka mkazo kuushurutisha uongozi uwasaidie kutatua matatizo, wananchi wanaangalia kiongozi awe kama baba yao aje kuwafuta machozi.

Na kiongozi asipokubali kuwa baba yao kuja kuwafuta machozi anaonekana mbaya, hata kama hakufanya hivyo kwa sababu anatafuta suluhu ya msingi ya tatizo (not that Magufuli is doing that, tomy knowledge so far).

Na kiongozi akiweza kuja kuwafuta machozi anaonekana mzuri sana, hata kama hafanyi lolote kumaliza tatizo la msingi.

Ni utamaduni wa kijinga sana, ndio huu unapelekea watu kumlilia Magufuli aende kwenye msiba kamavile Magufuli ana uwezo wa kufufua watu.
 
Kuwa na adabu bac usipende kulaum tu kwan makamu. Wake aliye enda hatoshi hadi liende baraza zima la viongoz kumbuka kuwa nawew pengine hujaenda na kama umeenda shida yako ilikuwa ni kwenda msibani au kuangalia walo hudhuria?

Hahahaaa....wenzio wanaona namtetea Magu kisa ukabila...wengine wanaona nahalalisha kukosa kwake kwenda kwa kuangalia Kikwete alikuwaje....halafu wewe nawe unaona namlaumu Magu!

Kweli watu tumetofautiana sana kiakili....
 

Magufuli gubegube varuvaru hajui whats good for him, hajui whats good for his people.

Ana muelekeo wake na anaufuata huo huo kama guluguja asiye na uti wa mgongo wala ubongo anayeenda kwa reflex action tu.
 

Hahahaaa mazee....wataokuelewa hapa sidhani kama watazidi idadi ya vidole kwenye kiganja!
 
Braza njaa imekuwa kali sana huko inaonekana biashara ya box imekuwa ngumu umeanza u-Lemutuz. Kila unapotokea msiba wako watu wanaokosa kuhudhuria kwa sababu mbalimbali. Kwa vile wewe haujui sababu za Magufuli kutohudhuria ungetuliza kipago na kupiga kimya. Tatizo ni pale unapotumia hii fursa kujipendekeza na kutengeneza headline kwa manufaa yako binafsi. Nchi nzima haiwezi kuacha kufanya kazi kwa kwenda msibani na ni sahihi kabisa kwa Raisi kutuma mwakilishi ili afanye kazi nyingine. Ndio maana hakutangaza maombolezo ya kitaifa na kubabaishwa na presha zenu za mitandaoni. Sio kila mtu anahudhuria msiba, kama umetingwa unatuma salamu, ndio utamaduni wetu watanzania
 
Ni kweli.

Na ndiyo maana kama umenisoma vizuri na kuelewa ulichokisoma utaona nimesema kuwa ingekuwa ni vyema kama yeye mwenyewe angeenda kwenye hiyo hafla ya kuwaaga hao maiti.
Ila pia ukaeleza Uzuri wa yeye kutokwenda!! Ili tu asijeonekana kuwa ni rais wa misiba! Nimekupata sawia.
 
Na kweli bora hajaenda maana huenda "angechafua hali ya hewa" tena kwa kauli zenye utata.

Bado nakumbuka kauli za kule Bukoba!
 
Ila pia ukaeleza Uzuri wa yeye kutokwenda!! Ili tu asijeonekana kuwa ni rais wa misiba! Nimekupata sawia.

Unaona sasa...

Tatizo la kusoma kitu na kutokukielewa.

Hakuna hata sehemu moja niliyoelezea uzuri wa yeye kutokwenda.

Nilichofanya ni ku speculate sababu ya yeye kutokwenda.

Umeshindwa kusoma na kuelewa ulichokisoma!

Majanga.
 
Kumtetea huyo mtu inabidi uwe na akili ya mwendawazimu.....Huchelewi kusema kikwete pia alikuwa anakula rambirambi za wahanga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…