Genius Man
JF-Expert Member
- Apr 7, 2024
- 3,560
- 7,914
Rais wa bunge la ulaya kuja Tanzania kuleta azimio kwa serikali na bunge la Tanzania kuhakikisha haki inapatikana ikiwemo uchaguzi huru na wa haki.
Bunge la ulaya limelaani mauwaji ya kiholela, ukamataji watu hovyo wasio na hatia unaofanywa na jeshi la polisi, matukio ya utakaji na uhalifu kwa wakosoaji wa serikali, umelaani kuwepo kwa kesi za mchongo na za kisiasa zisizokuwa na msingi.
Wanasisitiza haja ya EU kuhakikisha kwamba ushirikiano wake wa kimaendeleo na Tanzania, ikiwa ni pamoja na mpango wa Global Gateway, unaendana na uendelezaji wa haki za binadamu, uhuru wa kujieleza na viwango vya kesi vyenye haki.
Wabunge hao wanamuagiza Rais wake kupeleka azimio hilo kwa Serikali na Bunge la Tanzania pamoja na Umoja wa Afrika.
Azimio hilo linatarajiwa kupigiwa kura na wabunge hao leo Alhamisi tarehe 8.
Bunge la ulaya limelaani mauwaji ya kiholela, ukamataji watu hovyo wasio na hatia unaofanywa na jeshi la polisi, matukio ya utakaji na uhalifu kwa wakosoaji wa serikali, umelaani kuwepo kwa kesi za mchongo na za kisiasa zisizokuwa na msingi.
Wanasisitiza haja ya EU kuhakikisha kwamba ushirikiano wake wa kimaendeleo na Tanzania, ikiwa ni pamoja na mpango wa Global Gateway, unaendana na uendelezaji wa haki za binadamu, uhuru wa kujieleza na viwango vya kesi vyenye haki.
Wabunge hao wanamuagiza Rais wake kupeleka azimio hilo kwa Serikali na Bunge la Tanzania pamoja na Umoja wa Afrika.
Azimio hilo linatarajiwa kupigiwa kura na wabunge hao leo Alhamisi tarehe 8.