Jana ilikuwa sikukuu ya EID. Rais wetu wa Z'bar alikagua gwaride rasmi la Jeshi la Polisi kabla ya kuhutubia baraza la EID. Swali langu, hivi hufanya hivyo hata kwenye sikukuu za x-mas au pasaka? Au kwa vile rais ni islamu kapewa heshima hiyo na siku akiwepo rais mkristo nayeye atakuwa akikagua gwaride kama hilo kwenye sikukuu za x-mas na pasaka? Naambiwa pia rais wetu huteua KADHI.
Hata hivyo Nyerere katika moja ya hotuba zake amewahi kutamka kwamba nchi yetu haina dini lakini watu wake wana dini na kwamba aliwahi kusema maneno hayo mbele ya maaskofu DSM na kurudia maneno kama hoyo kwa mashehe Z'bar....
Wana JF hili limekaaje, mwenye elimu ndefu kwenye hili ebu atuelimishe.
Hata hivyo Nyerere katika moja ya hotuba zake amewahi kutamka kwamba nchi yetu haina dini lakini watu wake wana dini na kwamba aliwahi kusema maneno hayo mbele ya maaskofu DSM na kurudia maneno kama hoyo kwa mashehe Z'bar....
Wana JF hili limekaaje, mwenye elimu ndefu kwenye hili ebu atuelimishe.