Wewe mwenyewe ndiyo unajidharau. Miaka mitano uchumi ulikuwa na kuvuka kwenda kundi la uchumi wa kati. Hii ni kwa kutumia taarifa za vyombo hivyo hivyo unasema vinatudharau. Kama ilidharaulika wasingekusifu. Ukweli ni kuwa Kenya inaelewa lugha moja "tit for tat". Sasa hivi raisi Kenyatta ameizuga TZ kuwa Watanzania sasa hawatahitaji vibali vya kazi kule KE. Hapo ameishamtega rais SSH. Kinachongojewa ni yeye kutamka Wakenya kuingia na kupata kazi bila vibali. Tukiisha ingia mtego huo, ujuwe bao limefungwa. Ukijaribu kubadili ndiyo kufungiana. Haya mambo hayahitaji maamuzi yam kihemuko. Mama rais SSH inabidi awe na uchambuzi mkubwa kabla ya kutoa matamko ya kisiasa hasa pale hayo matamko yanahusu nchi na nchi. Nafikri huyo anayeitwa gwiji wa mambo ya nje, ni kazi yake kumshauri mama SSH kuhusu athari za matamko ya kisiasa, hasa yale matamko yanayohusu policy kinzani!