Mr_Teacher
JF-Expert Member
- Feb 28, 2021
- 362
- 334
Posho USD6700/= kwa siku? duuh, au ni typing error.Wanabodi Shaloom!
Ninakuomba kama itakupendeza futilia mbali Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ili fedha za umma zinazoteketea kuligharamia zitumike kwingine. Ni kitengo cha upigaji.
Nikukumbushe: mwaka 2005 baada ya Jakaya kuingia madarakani ndipo kitengo hiki kiliundwa mahsusi kumpa Salvatory Rweyemamu ulaji kwa kazi kubwa aliyoifanya kumpamba Jakaya na kuwachafua wapinzani wake kupitia gazeti la RAI Nguvu ya Hoja.
Nafasi za Ubunge, Uwaziri, U-DC au RC hazikuonekana "kumtosha" Salva ndipo alipopendekeza kuwepo na Kurugenzi hiyo ili asafiri na Rais popote duniani na posho ya dola 6700 kwa siku kwa kila safari nje ya nchi.
Rais Magufuli alipoingia naye akaridhi kitengo hiki cha upigaji hela za umma akimweka Gerson Msigwa ambaye naye akawaalika "washikaji" wake kujazana hapo bila kazi maalum zaidi ya kupiga hela. Ofisi ina watu 13 lakini uliza kazi ya kila mmoja ni nini?
Magufuli alisambaratisha kitengo cha Jikoni-Ikulu iliyokuwa na watu zaidi ya 100 akisema, "nitapikiwa na mke wangu". Kilikuwa cha upigaji sawa na hii Kurugenzi.
Unajiuliza Rais anaye Katibu wake, Mwandishi wake wa Habari, Mpigapicha, nini kazi ya Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu? Hivi kuandika barua za teuzi na tenguzi ni za kuajiri Mkurugenzi na Idara hewa chini yake? Nini kazi ya Msemaji Mkuu wa Serikali?
Sasa tunaona Msigwa ndiye Msemaji wa Serikali na wakati huo ndiye Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu (Serikali). Huku ni kuchanganya Mawasiliano ndio maana tulishuhudia JPM akikana uwepo wa Covid-19 na Dk. Abbas akikiri kuwepo Corona. Ikulu vs Idara ya Habari MAELEZO.
Fedha za kugharamia Kurugenzi hii zielekezwe kwenye matumizi mengine. Nawasilisha!
#FreedomIsBack
anyway, sidhani kama ni sahihi sana kufuta hiyo kurugenzi, kwanza watu wamepata Ajira hapo, ni jambo jema kwa watanzania kupata ajira kadha wa kadha. lakini pia haouliowataja katibu wa Rais, waandish wake wa habari wana majukumu yao ambayo ni tofauti na ya Kurugenzi ya mawasiliano, hivyo si sahihi kuifuta. lakini kwa kua et kurugenzi hiyo haikuwepo kabla ilianzishwa na JK ndo sasa ifutwe, kwahyo ndio ksema vitu vinavyostahili kuwepo ni vile vilivyokuwepo tangu enzi za Nyerere tu? haifai kuboresha?
lakini ningekubaliana na ww kuwa Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ifanye zaidi ya inavyofanya sasa. mfano imuandalie Rais kuwa anaongea na wananchi mfano kwa hotuba za kila mwisho wa mwez kama wkt wa BWM, iwe pia inakutana na wanahabari na kutoa taarifa mbali mbali na kujibu maswali lakini pia mitandaoni (mfano twitter) wanakua wanaandaa siku na masaa kadhaa Rais anakua anajb tweets za wananchi papo kwa papo n.k ila sio kuifuta Kurugenzi, iendelee ila tuiboreshe