Farolito
JF-Expert Member
- Sep 10, 2018
- 11,634
- 26,373
" Watumie kikamilifu kanuni ya GIVE and TAKE. Wakubali kubaki na kidogo na pia kupoteza kidogo. Kama wanataka yawe yao yote, wakae tayari kupoteza yote."
Nakubaliana na maoni yako na hapa nataka nizungumzie hii aya ya mwisho,hapa kwenye Give and take ndio shida ya CCM,hawapo tayari kutoa kidogo na kubaki na kidogo na hili kosa alishalianzisha Mwendazake kwa kuiba uchaguzi mdogo na huu wa wabunge na uraisi kwa kupora majimbo yote ya upinzani.
Kosa lingine linaloenda kufanyika ni hili la kukataa katiba mpya na hapa wanadhani kwamba wenye shida na katiba mpya ni wapinzani kitu ambacho si kweli hapa lipo kundi kubwa sana hata humo CCM wapo.
Na hii katiba mpya si tu kwamba wanaikataa kwa sababu haina maana hapana,wanajua kabisa ni muhimu ila kwa sababu wanajua itaenda kufanya walichokumbatia kipungue mkononi mwao ndio maana wanatumia nguvu kubwa kuikataa.
Sasa hapa wanaosema kwamba CCM haifi wajiulize yafuatayo;
Nini kilimtisha mwendazake mpaka kaamua kupora uchaguzi mpaka watoto wakajua ameiba ?
Kwanini CCM inatumia nguvu kubwa hasa dola kubaki madarakani?
Nini kinasababisha Mama Samia aogope kuruhusu mikutano ya Kisiasa iendelee wakati yeye hagharamii chochote kwenye kwenye hio mikutano?
Ukiangalia vidokezo nilivyoweka hapo juu utaona kabisa ni 'Hofu' ndio iliyojaa kwenye mioyo ya CCM wakijua kabisa Mikutano ya Kisiasa itaamsha watu kifikra juu ya udhaifu wao,Pia itawaamsha hamasa ya watu kudai Katiba mpya kitu ambayo ikipatikana ni wazi kabisa watakuwa hawana chao maana nguvu yao kuu ipo kwenye Dola wala sio wananchi.
Mwisho kabisa,CCM wakubali au wakatae wao ndio wanaenda kupoteza katika hili,maana wapinzani wao hawana chochote cha kupoteza kwa sasa,
CCM ndio wamekumbatia vyote na wanashindana waendelee kubaki navyo na kwa sababu watu wameshaamua,hapa wanaenda kupoteza vyote,ni suala la muda tu watakuja kugundua walishachelewa na hawataamini kama ambavyo hawakuamini siku Magufuli alipopumzishwa kwa amani(kama anayo)huko Chato.
Nakubaliana na maoni yako na hapa nataka nizungumzie hii aya ya mwisho,hapa kwenye Give and take ndio shida ya CCM,hawapo tayari kutoa kidogo na kubaki na kidogo na hili kosa alishalianzisha Mwendazake kwa kuiba uchaguzi mdogo na huu wa wabunge na uraisi kwa kupora majimbo yote ya upinzani.
Kosa lingine linaloenda kufanyika ni hili la kukataa katiba mpya na hapa wanadhani kwamba wenye shida na katiba mpya ni wapinzani kitu ambacho si kweli hapa lipo kundi kubwa sana hata humo CCM wapo.
Na hii katiba mpya si tu kwamba wanaikataa kwa sababu haina maana hapana,wanajua kabisa ni muhimu ila kwa sababu wanajua itaenda kufanya walichokumbatia kipungue mkononi mwao ndio maana wanatumia nguvu kubwa kuikataa.
Sasa hapa wanaosema kwamba CCM haifi wajiulize yafuatayo;
Nini kilimtisha mwendazake mpaka kaamua kupora uchaguzi mpaka watoto wakajua ameiba ?
Kwanini CCM inatumia nguvu kubwa hasa dola kubaki madarakani?
Nini kinasababisha Mama Samia aogope kuruhusu mikutano ya Kisiasa iendelee wakati yeye hagharamii chochote kwenye kwenye hio mikutano?
Ukiangalia vidokezo nilivyoweka hapo juu utaona kabisa ni 'Hofu' ndio iliyojaa kwenye mioyo ya CCM wakijua kabisa Mikutano ya Kisiasa itaamsha watu kifikra juu ya udhaifu wao,Pia itawaamsha hamasa ya watu kudai Katiba mpya kitu ambayo ikipatikana ni wazi kabisa watakuwa hawana chao maana nguvu yao kuu ipo kwenye Dola wala sio wananchi.
Mwisho kabisa,CCM wakubali au wakatae wao ndio wanaenda kupoteza katika hili,maana wapinzani wao hawana chochote cha kupoteza kwa sasa,
CCM ndio wamekumbatia vyote na wanashindana waendelee kubaki navyo na kwa sababu watu wameshaamua,hapa wanaenda kupoteza vyote,ni suala la muda tu watakuja kugundua walishachelewa na hawataamini kama ambavyo hawakuamini siku Magufuli alipopumzishwa kwa amani(kama anayo)huko Chato.