Rais Samia ni mponya nchi muungeni mkono tusonge mbele

Twayemba

Member
Jan 29, 2024
12
14
Nikikumbuka tulikotoka, ugumu wa maisha kisiasa na uhalisia wa maisha ya mtu mmoja mmoja, nashawishika kumkubali Samia hadharani bila hata haya wala soni.

Watanzania tuna mengi ya kuridhika kupitia huyu mama kwa kuangalia rekodi za hapo nyuma, ambapo watu wengine waliishi kwa hofu, kutokana pengine na itikadi zao, misimamo tofauti na pengine hata chuki binafsi.

Aidha nakubaliana nae juu ya mabadiliko kadhaa ya sheria zetu zinazohusu namna bora ya uendeshaji siasa zetu, na kwa kweli huu ni mwanzo mzuri kwa demokrasia yetu. Hongera Rais, ni mwanzo mzuri.
 
Hizi tabia za uchawa hata mama zimesha mkera mkuu.
Zamani tuliwaita wapambe, na walikua wakisha sifia kama wewe ulivyo fanya hapa, walikua wanaweka na namba za sim ili wakumbukwe..😜
Lakini,ameandika neno ujue!Unayakumbuka yale maisha wakati tupo na kibaka yule?Hadi kila mtu alisema .."I quit this horrible life"..!
 
Nikikumbuka tulikotoka,ugumu wa maisha kisiasa na uhalisia wa maisha ya mtu mmoja mmoja,nashawishika kumkubali Samia hadharani bila hata haya wala soni.
Watanzania tuna mengi ya kuridhika kupitia huyu mama kwa kuangalia rekodi za hapo nyuma,ambapo watu wengine waliishi kwa hofu, kutokana pengine na itikadi zao, misimamo tofauti na pengine hata chuki binafsi.
Aidha nakubaliana nae juu ya mabadiliko kadhaa ya sheria zetu zinazohusu namna bora ya uendeshaji siasa zetu,na kwa kweli huu ni mwanzo mzuri kwa demokrasia yetu.Hongera Rais,ni mwanzo mzuri.
Huyo ni sehemu uharibifu wa nchi.
Kumbuka, ndiyo Makamu Mwenyekiti wa bunge la Katiba liliharibu Mchakato mzima upatikanaji wa Katiba mpya.
Ndiye Makamu wa rais wa serikali iliyoijeruhi na kuiumiza sana nchi ambayo sasa mnasema kuwa anaiponya.
Anaiongoza serikali ileile iliyoivuruga na kuiumiza nchi huku akiwatumia na kuwarudisha watu walewale amnao ni public enemies.
Mkija kustuka, mtakuta Samia ameimalizia nchi na kuisambaratisha kabisa.
 
Mwanzoni kila mtu alikua na imani nae
Watu walimpenda na kumpa support
Tulimpa nafasi aonyeshe uwezo wake lakini kazingua...!
Kila sekta kairudisha nyuma mara 10
Mimi nipo serikali hao wapinzani ndio walitaka sehemu ya biashara za serikali kubinafsishwa wakidai Magufuli alikuwa anachukua pesa kupitia hizo taasisi.


Baadhi ya taasisi walisema TPA, TASAC ,GPSA ,sasa nan mbaya ? wakati rais Samia alipochukua tu nchi alianza kufanyia kazi hilo na mchakato ulianza ...Alichobugi kuwasikiliza wapinzani haswa kwa hoja zazlizojaa nadharia ipo interview ya Lissu akiongelea hilo suala.

Kashafanya sasa ulitegemea nn?
 
Kwasababu mjinga mmoja analeta akili za kijinga kwenye mambo ya maana

Ujinga ndo unafanya Watanzania kila siku tunalia na ugumu wa maisha kiujumla.
Sasa atumie busara kukufundisha wakati amejua njia nzuri ya kukufundisha uuache ujinga wako?Matumizi mabaya ya busara.Tazama kadiri ya chongo yake.
 
Mimi nipo serikali hao wapinzani ndio walitaka sehemu ya biashara za serikali kubinafsishwa wakidai Magufuli alikuwa anachukua pesa kupitia hizo taasisi.


Baadhi ya taasisi walisema TPA, TASAC ,GPSA ,sasa nan mbaya ? wakati rais Samia alipochukua tu nchi alianza kufanyia kazi hilo na mchakato ulianza ...Alichobugi kuwasikiliza wapinzani haswa kwa hoja zazlizojaa nadharia ipo interview ya Lissu akiongelea hilo suala.

Kashafanya sasa ulitegemea nn?
Akili za kuambiwa changanya na za kwako
Huwezi kua mbumbumbu kila unachoambiwa unafanya bila kutafuta wataalam kuangalia prons na cons halafu uje na hitimisho.

Uliyotoa sio sababu ya msingi ya kufanya yeye afeli kila sekta
Nitajie sekta hata moja tu ambayo inafanya vizuri kwenye utawala wake.
 
Mkuu! Ebu leta hoja kutetea upande wako
Mimi sipo hapa kugombana
Kugombana ni udhaifu wa nafsi na kuomba huruma.Nchi imetulia.Hakuna ujinga.Kinachowakwaza wehu ni kutaka wakiamka wawe na mahela chekwa mifukoni.Haiwezekani.Kama mnayataka maisha ya Myanmaar na myapate.
 
Akili za kuambiwa changanya na za kwako
Huwezi kua mbumbumbu kila unachoambiwa unafanya bila kutafuta wataalam kuangalia prons na cons halafu uje na hitimisho.

Uliyotoa sio sababu ya msingi ya kufanya yeye afeli kila sekta
Nitajie sekta hata moja tu ambayo inafanya vizuri kwenye utawala wake.
Ndio kafeli kwa kuwasikiliza wapinzani ,mbaya zaidi kajazwa sumu za kumchukia Magufuli na hao watu wa ovyo.
 
Back
Top Bottom