jitombashisho
JF-Expert Member
- Jun 11, 2020
- 667
- 2,242
Ni suala la muda tu.
Kwa nyendo zake za mapema tu Samia anaenda kuizika rasmi CCM.
Ikumbukwe uiamara wa CCM ulikuwa umebaki katika ncha ndogo sana ya kuwapigania wanyonge japokuwa haupo ushahidi wa moja kwa moja kama kilifanya hivyo.
Pamoja na yote Hayati Magufuli alijiegemeza katika jambo hilo kwa sababu aliamini ncha hiyo aghalabu ingeendelea kumweka jirani na hao wanaoitwa wanyonge ili tu kwalo CCM iendelee kuwa madarakani.
Sasa kwa muziki wa huyo mama kwanza kuruhusu kulegezwa kwa baadhi ya masharti ambayo yalikuwa yamepewa mkazo na mtangulizi wake yakiwamo vibali vya kazi,kuruhusu wafanyabiashara mafisadi kurejea hiyo ni dalili ya kuwa rasmi tunarejea kwenye zama za unanijua mimi ni nani.
Samia ameamua kucheka na mabua kwa hakika mwisho wa CCM waja tena kwa kasi!
Kwa nyendo zake za mapema tu Samia anaenda kuizika rasmi CCM.
Ikumbukwe uiamara wa CCM ulikuwa umebaki katika ncha ndogo sana ya kuwapigania wanyonge japokuwa haupo ushahidi wa moja kwa moja kama kilifanya hivyo.
Pamoja na yote Hayati Magufuli alijiegemeza katika jambo hilo kwa sababu aliamini ncha hiyo aghalabu ingeendelea kumweka jirani na hao wanaoitwa wanyonge ili tu kwalo CCM iendelee kuwa madarakani.
Sasa kwa muziki wa huyo mama kwanza kuruhusu kulegezwa kwa baadhi ya masharti ambayo yalikuwa yamepewa mkazo na mtangulizi wake yakiwamo vibali vya kazi,kuruhusu wafanyabiashara mafisadi kurejea hiyo ni dalili ya kuwa rasmi tunarejea kwenye zama za unanijua mimi ni nani.
Samia ameamua kucheka na mabua kwa hakika mwisho wa CCM waja tena kwa kasi!