Philipo Mwakibinga
Senior Member
- May 13, 2013
- 111
- 175
RAIS WA JMT MAMA SAMIA KUMSTAAFISHA UENYEKITI WA CHADEMA NDUGU FREEMAN MBOWE IFIKAPO MWAKA 2023.
Na; Philipo Mwakibinga
Muda kidogo nilijiuliza sana bila kupata majibu juu ya azma na uamuzi wa Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Mbowe (Mwamba) kutangaza kuwa ifikapo Mwaka 2023 atang'atuka uenyekiti wa Chama hicho kinachopoteza uwezo wake kila uchao. Mambo yaliyonifanya nishangae na kupata sintofahamu ni;
Uchaguzi wa Serikali za mitaa utakua Mwaka 2024. Swali nikawa najiuliza iweje Mh Mbowe aukimbie uchaguzi huu muhimu sana katika nchi yetu? Kwanini asiongoze chama katika jambo hilo ili awavushe wale wanaoimba kila siku kuwa, Mwamba tuvushe×2?
Uchaguzi Mkuu 2025. Hapa pia nilijiuliza sana iweje Mwamba ninayemfahamu aingize chama kwenye uchaguzi Mkuu wa kihistoria bila yeye kuwa Mwenyekiti? Nani CHADEMA yuko tayari kusikia hilo? Mbaya zaidi sijasikia Mwanachadema yeyote aliyelalamikia uamuzi wa Mwamba tofauti na miaka yote anayobeep kujifanya hagombei halafu anatengeneza watu wanajifanya wamemchukulia form. Nikajiuliza nikweli Wanachadema wamemchoka Mwamba kiasi hicho cha kumuacha aendezake?
Suala la Michango ya Kadi Moja kuwa Laki Mbili. Hili nalo, lilinifanya nibaki na uvulivuli katika fikra zangu, kwani nilibaki nashangaa imekuaje Mwamba aanzishe uvunaji mkubwa wa Pesa kiasi hicho halafu asiwepo katika nafasi ya kuamua nini kitumike wapi kwa namna gani kama ilivyo kawaida yake?
LEO NIMEGUNDUA KUMBE MWAMBA ALISHAMSOMA RAIS MAMA SAMIA
Hapa imebidi nikumbuke Dr Slaa aliposema sasa kwa aina ya uongozi wa Rais Mama Samia, ndiye anakuja kuunyima ajenda upinzani kabisa bora hata aliyepita aliwapa ajenda za kuzungumza kwa mfumo wake aliotumia. Nimekubali! Mfano ukifuatilia namna maono na mipango yake unagundua kabisa kuwa Upinzani utakosa cha kulalamika na kuungwa mkono. Kama ulifuatilia kongamano la leo utagundua kuwa VIJANA SASA WANAMUELEWA MAMA SAMIA NA WOTE WANAENDELEA KUMUUNGA MKONO.
Mbowe kaona bora kushindwa kwa chama chake kwa mara nyingine kusiwe katika mikono yake. Bora aepuke lawama na kulinda heshima yake kuliko kuendelea kuwa Mwenyekiti aliyeshindwa mara nyingi zaidi baada ya Lipumba. MBOWE NI MUUNGWANA. Maana waswahili wanasema haja ya mja kunena lakini Muungwana ni vitendo. Kaka kaonesha kitendo cha kukimbia mapema ili kujitoa lawamani.
Huwezi kushindwa kumuelewa na kufanyakazi na Rais huyu kwasababu anapenda kuona Wananchi wote wanapenda kufanikiwa na wanatengeneza miundombinu ya kufikia mafanikio. Vijna wamepata somo kubwa sana leo ambalo matokeo yake yatakua ni utekelezaji wa maazimio ya kwenye kongamano.
Viongozi wengi wa Afrika wamekua wakiogopa kuongea na vijana kwani ndiyo kundi lenye mahitaji mengi sana pamoja na kuwa ndiyokundi linalotegemewa sana. Wengi wameishia kuongea na Wazee na akinamama tu.
TANZANIA TANZANIA TANZANIA.
Na; Philipo Mwakibinga
Muda kidogo nilijiuliza sana bila kupata majibu juu ya azma na uamuzi wa Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Mbowe (Mwamba) kutangaza kuwa ifikapo Mwaka 2023 atang'atuka uenyekiti wa Chama hicho kinachopoteza uwezo wake kila uchao. Mambo yaliyonifanya nishangae na kupata sintofahamu ni;
Uchaguzi wa Serikali za mitaa utakua Mwaka 2024. Swali nikawa najiuliza iweje Mh Mbowe aukimbie uchaguzi huu muhimu sana katika nchi yetu? Kwanini asiongoze chama katika jambo hilo ili awavushe wale wanaoimba kila siku kuwa, Mwamba tuvushe×2?
Uchaguzi Mkuu 2025. Hapa pia nilijiuliza sana iweje Mwamba ninayemfahamu aingize chama kwenye uchaguzi Mkuu wa kihistoria bila yeye kuwa Mwenyekiti? Nani CHADEMA yuko tayari kusikia hilo? Mbaya zaidi sijasikia Mwanachadema yeyote aliyelalamikia uamuzi wa Mwamba tofauti na miaka yote anayobeep kujifanya hagombei halafu anatengeneza watu wanajifanya wamemchukulia form. Nikajiuliza nikweli Wanachadema wamemchoka Mwamba kiasi hicho cha kumuacha aendezake?
Suala la Michango ya Kadi Moja kuwa Laki Mbili. Hili nalo, lilinifanya nibaki na uvulivuli katika fikra zangu, kwani nilibaki nashangaa imekuaje Mwamba aanzishe uvunaji mkubwa wa Pesa kiasi hicho halafu asiwepo katika nafasi ya kuamua nini kitumike wapi kwa namna gani kama ilivyo kawaida yake?
LEO NIMEGUNDUA KUMBE MWAMBA ALISHAMSOMA RAIS MAMA SAMIA
Hapa imebidi nikumbuke Dr Slaa aliposema sasa kwa aina ya uongozi wa Rais Mama Samia, ndiye anakuja kuunyima ajenda upinzani kabisa bora hata aliyepita aliwapa ajenda za kuzungumza kwa mfumo wake aliotumia. Nimekubali! Mfano ukifuatilia namna maono na mipango yake unagundua kabisa kuwa Upinzani utakosa cha kulalamika na kuungwa mkono. Kama ulifuatilia kongamano la leo utagundua kuwa VIJANA SASA WANAMUELEWA MAMA SAMIA NA WOTE WANAENDELEA KUMUUNGA MKONO.
Mbowe kaona bora kushindwa kwa chama chake kwa mara nyingine kusiwe katika mikono yake. Bora aepuke lawama na kulinda heshima yake kuliko kuendelea kuwa Mwenyekiti aliyeshindwa mara nyingi zaidi baada ya Lipumba. MBOWE NI MUUNGWANA. Maana waswahili wanasema haja ya mja kunena lakini Muungwana ni vitendo. Kaka kaonesha kitendo cha kukimbia mapema ili kujitoa lawamani.
Huwezi kushindwa kumuelewa na kufanyakazi na Rais huyu kwasababu anapenda kuona Wananchi wote wanapenda kufanikiwa na wanatengeneza miundombinu ya kufikia mafanikio. Vijna wamepata somo kubwa sana leo ambalo matokeo yake yatakua ni utekelezaji wa maazimio ya kwenye kongamano.
Viongozi wengi wa Afrika wamekua wakiogopa kuongea na vijana kwani ndiyo kundi lenye mahitaji mengi sana pamoja na kuwa ndiyokundi linalotegemewa sana. Wengi wameishia kuongea na Wazee na akinamama tu.
TANZANIA TANZANIA TANZANIA.