Rais Samia, naomba ajira

My Son drink water

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
4,932
13,283
Rais wangu Samia, naomba ajira, uniteue niwe Mkurugenzi mkuu wa TISS, hii kazi naipenda kuliko kazi zote Duniani.

Naipenda hii kazi kwa sababu naipenda sana nchi yangu Tanzania.

Sina chama chochote cha kiasiasa ninachokifia, Chama changu ni Tanzania.

Ukiniteua kwenye hii nafasi ,nitafanya maajabu kwa muda mfupi tu.

Kwanini nasema nitafanya maajabu kwa muda mfupi tu?

Rais wangu, Idara ya Usalama wa Taifa ktk Taifa lolote lile Duniani ndo Roho ya nchi, Idara ikiwa Dhaifu na Taifa linakuwa Dhaifu.

Uimara wa China kiuchumi kwa muda mfupi tu umetokana na Uimara Intelligence yao.

Hatuwezi kufika popote Kama Taifa bila kuwa na Idara imara.

Kila baada ya miezi miwili au mitatu Idara ya Usalama wa Taifa la Kenya kitengo cha Uchumi hukutana ili kuboresha mbinu za kuhakikisha Tanzania, Uganda, Burundi na Rwanda zinaendelea kununua Bidhaa nyingi za Kenya kuliko zenyewe kuuza Kenya, mambo ni mazito na magumu yanafanyika, na bado mipango mizito inafanywa ili tuendelee kununua zaidi Kenya kuliko kuuza.

Ukiniteua kwenye hii nafasi, nitaunda kikosi kazi maalumu ambacho kazi yake ni kwenda kuiba Technology ya kutengeneza Bidhaa muhimu kiuchumi.

Itahitaji maandalizi ya miaka mitatu au miwili kuandaa hiki kikosi.

Intelligence imara haina muda na Siasa uchwara na wala haitumiki kwa maslahi ya Watawala wasio na Hekima.

Rais wangu Samia, naomba ajira.
 
Tutakupa interview kama:
Una kadi ya CCM,
Unaweza kuiba kura,
Unaweza kuteka, kutesa na kuua,
Unaweza kusikiliza mazungumzo ya Kinana na Nape kwenye simu,
Unaweza kuingia mitandaoni na kutukana na kutishia wote wenye mawazo tofauti na serikali.
Jiandae.
 
Mama mpe kazi huyu. Hivi hawa watu wetu huwa wanafanya ujasusi wa kiuchumi? mfano walishawahi kumu-outsmart nani, na ni vipi huwa tunaingia mikataba ya hovyo miaka na miaka.

Mama hata usipompa kazi huyu, kuna kitu kunatakiwa kufanyika idarani, Hii idara haitakiwi kuwa sehemu ya watu kwenda kupokea mishahara. Agggrrrrh its 2021... tuamke.

Idara imekuwa failure ya hii nchi.
 
Kila baada ya miezi miwili au mitatu Idara ya Usalama wa Taifa la Kenya kitengo cha Uchumi hukutana ili kuboresha mbinu za kuhakikisha Tanzania,Uganda, Burundi na Rwanda zinaendelea kununua Bidhaa nyingi za Kenya kuliko zenyewe kuuza Kenya,mambo ni mazito na magumu yanafanyika,na bado mipango mizito inafanywa ili tuendelee kununua zaidi Kenya kuliko kuuza.
Ukiniteua kwenye hii nafasi,nitaunda kikosi kazi maalumu ambacho kazi yake ni kwenda kuiba Technology ya kutengeneza Bidhaa muhimu kiuchumi.
Hili hapa tayari limekwisha kukosesha hiyo kazi.

Wewe hujui kama huyo hapo ni mtu wao, halafu unaanza kuwasema watu wake unayetaka akupe kazi?

Naona bado unajifunza hiyo kazi.

Hata hivyo ninakubaliana nawe kuhusu hao uliowataja kuhangaika sana na kuiteka Tanzania kwa njia mbali mbali, na kwa kiasi kikubwa wamefanikiwa, ingawaje mara moja moja mipango yao huvurugwa kwa muda, kama alivyoivuruga Magufuli.

Wewe angalia walivyoishikilia Tanzania iwe sehemu yao ya kuchezea: Tanzania inao majirani wengi, lakini ukiangalia kati ya majirani hao, ni Keya tu ndio walio na njia nyingi za kuingilia hapa. Njia moja ipo pale Tanga, sijui huitwa Horohoro, kama sikukosea; ukipanda juu kidogo unakutana na Horiri, pale kwa mama Mgwira, sasa sijui nani anaingia hapo.

Kabla hujaenda mbali unakutana na Namanga, na pale karibu na ziwa kuna Sirari, na huko majini Kisumu wanalilia bandari za Tanzania Mwanza, Bukoba, Musoma ziwe wazi.

Bado kuna njia za uchochoro tele, na hata bado wanalalamika ile njia ya kuingilia kwao hadi Serengeti ifunguliwe, ili waweze kuingiza watalii wao kirahisi.

Na njia zote hizi ni nzuri kabisa na zenye barabara za rami; lakini hawaridhiki. Wanataka ijengwe barabara mpya inayoambaa amba kando ya Bahari ya Hindi, toka huko kwao Malindi, ije hadi ifike Bagamoyo, pamoja na kwamba kuna njia nzuri tu hadi sasa inayoingilia pale Horohoro; na unajua ujenzi wa barabara hizi, ni miko[po tunayotakiwa kuilipa - kwa mfano hii ya kuambaa ambaa ni Benki ya Africa (AfDB) ndio wafadhiri, na pesa kidogo toka EU, washirika wetu wengine wanaopambana sana tuwe sehemu ya hao jamaa unaowazungumzia---, wao watakuwa wana sababu zao kwa nini wanataka iwe hivyo.

Bado nataka nikuonyeshe kiasi gani tunavyofungwa kamba ili tusiwaepuke hao wanaotuvuta kwao: hebu tazama barabara inayotokea Mombasa na kupitia pale Vo, na kuchepuka Taita Taveta kwenda kule kwa mama Mgwira; hiyo barabara ni sehemu inayokwenda hadi Singida, na kukatiza kwenda hadi Burundi. Kuna wakati, hao jamaa zako walidai wamejenga barabara hiyo iwarahisishie kupelka bidhaa zao na zile zinazoshushwa na meli Mombasa hadi Burundi. Wamejizatiti kabisa, na isingekuwa kuwepo kwa ujio wa Magufuli, malori yao na mfumo wao wa REITS wangekuwa tayari wanafanya kazi yao.

Siyo hivyo tu, hiyo barabara inayoingilia kwa mama Mghwira, inachepuka na kupanda kwenda Arusha na kupitiliza hadi Namanga na kwenda tena kushikana na ile inayotoka Mombasa!

Sasa nieleze, ni jirani yetu yupi mwingine tuliye naye mwingiliano kama jirani huyu?

Hawa majirani zetu wengine hatutaki kufanya nao biashara? Kwa nini? DRC, li nchi likubwa kabisa hapo, tena lenye utajiri wa kutisha na idadi kubwa ya watu (soko), mbona wao hatujihangaishi kabisa nao, ila Rais Kiburi aliyeleta fyokofyoko hata kabla hajawekwa shimoni, tayari jamaa wanaleta mwaliko uliokubaliwa harakaharaka!

Ngoja, nisiandike gazeti refu mno, huchukia kusoma magazeti humu.

Hao jamaa zako wanajuwa kwamba Tanzania ndiyo nchi inayotishia majigambo yao ya wao kuwa vinara katika eneo hili. Kama unaona juhudi zao nyingi hizo, juhudi hizo ni za kujihami na kupoza, ili wavute muda kidogo kubaki kileleni.

Lakini hatma yao wanaijuwa wazi.
 
Hili hapa tayari limekwisha kukosesha hiyo kazi.

Wewe hujui kama huyo hapo ni mtu wao, halafu unaanza kuwasema watu wake unayetaka akupe kazi?

Naona bado unajifunza hiyo kazi.

Hata hivyo ninakubaliana nawe kuhusu hao uliowataja kuhangaika sana na kuiteka Tanzania kwa njia mbali mbali, na kwa kiasi kikubwa wamefanikiwa, ingawaje mara moja moja mipango yao huvurugwa kwa muda, kama alivyoivuruga Magufuli.

Wewe angalia walivyoishikilia Tanzania iwe sehemu yao ya kuchezea: Tanzania inao majirani wengi, lakini ukiangalia kati ya majirani hao, ni Keya tu ndio walio na njia nyingi za kuingilia hapa. Njia moja ipo pale Tanga, sijui huitwa Horohoro, kama sikukosea; ukipanda juu kidogo unakutana na Horiri, pale kwa mama Mgwira, sasa sijui nani anaingia hapo.

Kabla hujaenda mbali unakutana na Namanga, na pale karibu na ziwa kuna Sirari, na huko majini Kisumu wanalilia bandari za Tanzania Mwanza, Bukoba, Musoma ziwe wazi.

Bado kuna njia za uchochoro tele, na hata bado wanalalamika ile njia ya kuingilia kwao hadi Serengeti ifunguliwe, ili waweze kuingiza watalii wao kirahisi.

Na njia zote hizi ni nzuri kabisa na zenye barabara za rami; lakini hawaridhiki. Wanataka ijengwe barabara mpya inayoambaa amba kando ya Bahari ya Hindi, toka huko kwao Malindi, ije hadi ifike Bagamoyo, pamoja na kwamba kuna njia nzuri tu hadi sasa inayoingilia pale Horohoro; na unajua ujenzi wa barabara hizi, ni miko[po tunayotakiwa kuilipa - kwa mfano hii ya kuambaa ambaa ni Benki ya Africa (AfDB) ndio wafadhiri, na pesa kidogo toka EU, washirika wetu wengine wanaopambana sana tuwe sehemu ya hao jamaa unaowazungumzia---, wao watakuwa wana sababu zao kwa nini wanataka iwe hivyo.

Bado nataka nikuonyeshe kiasi gani tunavyofungwa kamba ili tusiwaepuke hao wanaotuvuta kwao: hebu tazama barabara inayotokea Mombasa na kupitia pale Vo, na kuchepuka Taita Taveta kwenda kule kwa mama Mgwira; hiyo barabara ni sehemu inayokwenda hadi Singida, na kukatiza kwenda hadi Burundi. Kuna wakati, hao jamaa zako walidai wamejenga barabara hiyo iwarahisishie kupelka bidhaa zao na zile zinazoshushwa na meli Mombasa hadi Burundi. Wamejizatiti kabisa, na isingekuwa kuwepo kwa ujio wa Magufuli, malori yao na mfumo wao wa REITS wangekuwa tayari wanafanya kazi yao.

Siyo hivyo tu, hiyo barabara inayoingilia kwa mama Mghwira, inachepuka na kupanda kwenda Arusha na kupitiliza hadi Namanga na kwenda tena kushikana na ile inayotoka Mombasa!

Sasa nieleze, ni jirani yetu yupi mwingine tuliye naye mwingiliano kama jirani huyu?

Hawa majirani zetu wengine hatutaki kufanya nao biashara? Kwa nini? DRC, li nchi likubwa kabisa hapo, tena lenye utajiri wa kutisha na idadi kubwa ya watu (soko), mbona wao hatujihangaishi kabisa nao, ila Rais Kiburi aliyeleta fyokofyoko hata kabla hajawekwa shimoni, tayari jamaa wanaleta mwaliko uliokubaliwa harakaharaka!

Ngoja, nisiandike gazeti refu mno, huchukia kusoma magazeti humu.

Hao jamaa zako wanajuwa kwamba Tanzania ndiyo nchi inayotishia majigambo yao ya wao kuwa vinara katika eneo hili. Kama unaona juhudi zao nyingi hizo, juhudi hizo ni za kujihami na kupoza, ili wavute muda kidogo kubaki kileleni.

Lakini hatma yao wanaijuwa wazi.
Kenya ni Competitor sio Partner,

Huwezi kucompromise na Competitor.
 
Mkuu!ina maana Bia hazilipi huko kenya?Msalimie Lema mwambie arudi nyumbani jiwe lilishasagwa na mama atambeba mgongoni na kumfuta machozi kwa machungu yote uliyopitia!!!
 
Back
Top Bottom