tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Rais Samia Suluhu Hassan, ametangaza kulivunja rasmi Bunge Agosti 3, 2025, ili kutoa nafasi kwa uteuzi wa wagombea wa Uchaguzi Mkuu, unaotarajiwa kufanyika Oktoba, mwaka huu.
Taarifa hiyo imetolewa leo, ikiwa ni utekelezaji wa Ibara ya 90(2)(a) ya Katiba ya Tanzania, inayompa Rais mamlaka ya kuvunja Bunge iwapo limemaliza muda wake wa miaka mitano.
Soma pia: Kwa nini Rais ameahirisha shughuli za Bunge badala ya kulivunja kama katiba inavyosema? Kuna tatizo?
Kuvunjwa kwa Bunge kunakuja katika kipindi ambacho vyama vya siasa nchini vinaendelea na michakato ya ndani ya kuwapata wagombea wa nafasi za ubunge, urais na udiwani.
Imeandikwa na Jenifer Gilla, Dar es Salaam
Source: Nipashe
Taarifa hiyo imetolewa leo, ikiwa ni utekelezaji wa Ibara ya 90(2)(a) ya Katiba ya Tanzania, inayompa Rais mamlaka ya kuvunja Bunge iwapo limemaliza muda wake wa miaka mitano.
Soma pia: Kwa nini Rais ameahirisha shughuli za Bunge badala ya kulivunja kama katiba inavyosema? Kuna tatizo?
Kuvunjwa kwa Bunge kunakuja katika kipindi ambacho vyama vya siasa nchini vinaendelea na michakato ya ndani ya kuwapata wagombea wa nafasi za ubunge, urais na udiwani.
Imeandikwa na Jenifer Gilla, Dar es Salaam
Source: Nipashe