Rais Samia kuitikisa Mwanza Tarehe 30 Januari

Rais Samia kuitikisa Mwanza Tarehe 30 Januari

Mnajivunia wizi tu!! Hamna lolote, kwani ccm imewahi kushinda chaguzi zipi kwa halali??? Mpo kwenye mamlaka kwa hisani ya polisi na tume ya uchaguzi ambayo ni yenu
Hata ije Tume ya uchaguzi kutoka marekani bado CCM itapita na kushinda kwa kishindo kikuu kitakacho itetemesha Dunia nzima
 
Kambi au ofisi ni popote kwa taasisi ya urais. Hivyo tamko zito zaidi linaweza kutolewa jijini Mwanza.


TAARIFA RASMI

26 January 2024

RAIS SAMIA MGENI RASMI UGAWAJI BOTI NA VIZIMBA VYA SAMAKI MWANZA



View: https://m.youtube.com/watch?v=tnREURIM_Lo
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amebainisha Ujio wa Rais Samia Suluhu Hassan

Ni Ziara ya kikazi ya Siku mbili kuanzia Jumatatu 29-30, 2024 ambapo atazindua Ugawaji wa Boti na Vizimba vya Samaki.

RC CPA Makalla amesema hayo mapema leo januari 26, 2024 wakati wa Mkutano wake na Waandishi wa Habari uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa ukimhusisha pia Ujumbe wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Kufuatia Ugeni huo CPA Makalla amewakaribisha wananchi wa Mwanza na Mikoa ya jirani kufika kwenye Uwanja wa Ndege wa Mwanza siku ya jumatatu kwa ajili ya kumpokea na kumlaki pamoja na siku ya jumanne kwenye uwanja wa Nyamagana.

"Tarehe 30 januari, 2024 Mhe. Rais atazindua Ugawaji wa zana za Uvuvi za Kisasa kwa ajili ya Uvuvi endelevu vikiwemo Boti na Vizimba pamoja na kuzungumza na wananchi wa kanda ya Ziwa kwenye viwanja vya Nyamagana, hivyo basi nawaalika wananchi wote wa Mkoa wa Mwanza." CPA Makalla.

Aidha, amefafanua kuwa Rais Samia baada ya kuwasili Mwanza siku ya Jumatatu atatumia barabara kuu ya kuelekea mjini hivyo wananchi wanaalikwa kumlaki barabarani kuanzia Sabasaba, Pasiansi, Bwiru na Kwenye Mzunguko wa Ziro ili kumshangilia na kumlaki.

Source : Mwanza RS TV
 
Naona anakuja kupima upepo/ kazi aliyompa MAKONDA kama imefanikiwa,maana wana mwanza hawataki kumskia wala kumuona
Mwanza wakimsikia Rais Samia anakwenda huko wanatetemeka na kulipuka kwa shangwe na furaha kubwa sana katika mioyo yao.ndio maana hufurika kwa wingi sana kumpokea
 
Sasa mbona hamhitaki hiyo tume huru kama mnajiamini???? Mnajua kabisa uwanja sawa asubuhi ccm haipo madarakanj
 
Alama zake ndio kama hizi sukari kuuzwa sh 5000 kwa kilo?!
Serikali inaleta nchini tani za sukari zaidi ya laki moja ambazo zitasambazwa nchini kwote na hivyo bei ya sukari kushuka chini kama jani la mti
 
RC CPA Makala nadhani haitakuwa mwamvuli wa kuficha tukio kama alivyojaribu RC wa DSM Albert Chalamila ....


1706292120005.png
 
TOKA MAKTABA :

WAENDESHA PIKIPIKI BODABODA HATUKO TAYARI KUSHIRIKI KTK SIASA

Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Pikipiki (Bodaboda) mkoani Mwanza kada Makoye John amesema Jumuiya hiyo inalaani vikali Maandamano yaliyopangwa na vyama vya upinzani kwamba yatafanyika kwenye sehemu mbalimbali nchini januari 24, 2024.


View: https://m.youtube.com/watch?v=B0dB4SmQq2g
 
Toka maktaba :

MACHINGA WA JIJI LA MWANZA WASEMA KUNA KIPINDUPINDU, HATUTAKI MIKUSANYIKO YA KISIASA WALA MAANDAMANO


Mwenyekiti wa Shirikisho la Umoja wa Machinga Mkoa wa Mwanza (CHIUMA) Mohamed Dauda amesema wafanyabiashara wadogo Mkoa huo (Machinga) hawataandamana Janauri 24, 2024


View: https://m.youtube.com/watch?v=YBtOQhSI0FM

kama inavyohamasishwa na vyama vya siasa.Dauda ametoa tamko hilo mapema leo tarehe 22, Januari 2024 wakati wa mkutano wa shirikisho hilo pamoja na waandishi wa Habari uliofanyika kwenye Stendi ya Mabasi Nyegezi....
 
Je wenye Bodaboda na machinga tarehe 29 January 2024 wataandamana kumpokea rais, kama mkuu wa mkoa wa Mwanza RC CPA Amos Makala alivyotoa wito
 
Mwanza kwa sababu ndo kunafikika kirahisi kuliko Rukwa na kumbuka mwanza kuna watanzania wengi kuliko Rukwa. Hivyo ukihtaji kuongea / kuonana na watanzania wengi ukiachana na dsm basi nenda mwanza.
Alaaah ni hivyo kumbe sikujua!
 
Soko la Kariakoo linaeleka kuisha, soko la mwanza mjini lililoanza kujengwa mapema, bado
 
Yeye kakazana Monduli na Mwanza!
Rais wetu atafika kila sehemu ndugu yangu. Endelea kuwa na imani na mheshimiwa Rais wetu.anatupenda sana watanzania na mikoa yote anaipenda sana .ndio maana amepeleka maendeleo kila mkoa mabilioni kwa mabilioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo
 
Back
Top Bottom