Kitchener
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 13,823
- 27,694
Huu ni ushauri wa mtu mwenye nia njema kabisa na wewe. Walio karibu na wewe najua watakushauri usiufuate, ila mimi nakushauri ufuate. Usipofuata, ni hiari yako pia.
- Itisha press, uongee na Taifa. Inakuwaje mambo mengi yanaendelea vibaya, wewe upo kimya? Safisha hali ya hewa, watu watasahau, watarudisha mioyo nyuma na maisha yataendelea vizuri kwako. Kama ni kufuta watu kazi waliokufikisha hapa, usisite. Kama ni kutoa maelekezo kurekebisha mambo, fanya. Jiondoe kwenye lawama huku ukitoa maelekezo ya kuweka mambo sawa before it's too late for you.
- Batilisha ufugwaji wa makanisa. Watu wanakuona wewe kama Rais Muislam, unafanya hivyo kwa sababu una udini. Wanadamu hupishana kauli, ni kitu cha kawaida. Hata kama umenena mengi mabaya juu ya kanisa, jifanye mjinga, siku ipite kuokoa legacy yako. Fungua uhuru wa kuabudu.
- Issue ya Tundu Lissu itakugarimu sana. Elekeza DPP afute hizo kesi kwa sababu unapenda maridhiano. Kuridhiana sio kushindwa, ni kufuata maslahi mapana. Kama adhabu TL umeshampa, inatosha. Dunia nzima haikuelewi kwa sababu yake. Shida nini, kwani?
- Ulikuwa na uwezo kushinda uchaguzi bila hata kumfunga TL, kufuta makanisa, na kuteka na kuua watu. CHADEMA hata wangesema no reform, no election, kulikuwa na namna zingine kufanya kwa amani tu na ungeendelea na urais.
- Au tufanye hata ungeweka reforms, lazima ungeshinda. Hakuna chama cha upinzani kingechukua kiti chako. Wamekushauri tu vibaya. Zaidi sana wangepata wabunge wengi ila ungeendelea kuwa Rais hadi 2030.
- Umoja wa Ulaya watakuwekea vikwazo, utakosa pesa ya kuendesha nchi, maisha mtaani yatakuwa magumu. Watu watabadilika mioyo. Wazungu wakisababisha maandamano tu, watu wengi watakuwa na mwitikio kwa sababu tayari maisha mtaani magumu kutokana na vikwazo. Wataandamana, watakutoa mkuku mkuku madarakani. Hii ndio njia ya wazungu kuwatoa wale wasiowapenda. Hawa hawa machawa wanaokushabikia, wazungu wakiamua wanaweza kuwabadilisha mioyo kwa njia ya vikwazo, ukageukwa, wakaandamana na kukutoa madarakani.
- Tayari ulishajenga jina na kurudisha mahusiano na nchi za nje, lakini kwa kupambania cheo (ambacho hata ingekuwaje ungekipata), umeharibu mahusiano yote uliyoyajenga kwa gharama kubwa ya kodi zetu ulipokuwa unazunguka Ulaya. Haujachelewa, chukua hatua stahiki kujisahihisha. Kijifanya mjinga siku ipite, hautapungukiwa. Tuliza nchi kwa kuondoa yale yanayokera raia.
- Anayekushauri utumie mabavu kwenye kila kitu, mwondoe kwenye washauri wako. Anakupoteza. Hata kama una jeshi, polisi, TISS n.k., wananchi wakichoka huwa wanakuwa tayari hata kufa, hawaogopi. Pia, wazungu wakikuamlia, it will be too late for you. Nakushauri kwa nia njema kabisa.
- Mwisho, nakuomba: fungua makanisa, ni doa kubwa kako. Hao kina Mwamposa wanakudanganya, hata hawahesabiki kama ni Wakristo. Huwa tunawaona ni wapiga dili tu, hata wao wanajijua. Fungua makanisa watu wasali. Futa kikundi cha utekaji na uuaji hicho. Fukuza au badilisha washauri wako. Ukipenda, peleka uchaguzi mbele mwaka mmoja au miwili ili reform zifanyike. Utanishukuru. Mungu akusaidie.