Samia ni Rais na pia ni Mwenyekiti wa CCM. Hivyo chochote kinachofanywa na Serikali au CCM, kinamgusa moja kwa moja.
Kwa upande mwingine, sura ya CCM na Serikali, inabebwa na aina ya viongozi waliopo (serikalini na kwenye CCM), watu wanaoitetea na kuisifia kwa kila jambo serikalini na kwenye CCM, kwenye mazingira yote (mitandaoni, bungeni, mitaani, n.k.). Sura ya CCM na Serikali inabebwa na vyombo kama Polisi na Tiss, ambavyo vimeamua kuilinda CCM na Serikali kwa nguvu zote zilizo halali na za kiharamia, badala ya kuilinda Jamhuri, ambalo lilistahili kuwa jukumu lao la msingi. Taswira ya vyombo hivi inaambukiza na kuwa taswira ya Serikali, CCM na Rais. Tutazame taswira za kila kimoja:
POLISI
Polisi ya Tanzania, taswira yake kwa umma, ni chombo cha kuwaonea wananchi (wanabambikia kesi watu - hata Rais amewahi kulisema hili). Ni chombo cha mauaji holela (Rais hivi karibuni amekemea uharamia unaofanywa na chombo hiki hadi kufikia kuua watuhumiwa kwenye mahabusu zao). Ni chombo cha utesaji (Zaidi ya 90% ya waliowahi kukaa kwenye mahabusu za polisi kwaajili ya upelelezi, watakuambia waliteswa sana, na wakati fulani watu hao hawakuwahi kuwa na hatia). Kwa hiyo watu wanawaona polisi ni kaka genge la majambazi lililopewa uhalali na Serikali na CCM. Kwa sababu haiba ya chombo hiki inaambukiza kwa mmiliki wake, taswira hii ya Polisi imeambukiza, na kuifanya CCM, Serikali na Rais, waonekane hivyo hivyo.
WATETEZI NA WAIMBA MAPAMBIO
Ukiwaangalia na kuwasikiliza wapambe wengi wa CCM ni watu wenye uelewa mdogo (CCM inapendwa zaidi na watu wajinga - taarifa ya TWAWEZA), wanafiki, wasaka fursa, wasio na upeo, na watu wanaofurahia mauaji, mateso na uonevu (mfano humu JF, mtazame Iboya, USSR, n.k.) dhidi ya watu wasio na hatia. Msikilize mtu kama Doto James, aliyedai kuwa walishindwa kumwua Lisu kwa risasi, safari hii watamwua kwa sindano. Kwa kauli hizi, CCM inaonekana ni chama cha wauaji. Na taswura hii inaambukiza kwa Serikali na Rais mwenyewe. CCM ya leo inajivunia uwezo wake wa kuua watu wasio na hatia ili tu kubakia madarakani.
VIONGOZI
Wasikilize baadhi ya viongozi wa CCM/serikali. Mtazame Mwigulu, Kibajaji, Musukuma, Japipo, n.k. Ni watu wenye upe mdogo, wanaoamini kuwa sifa ya kiongozi ni kuwa mbabe, mwongo, na wakati fulani uwa kama mwendawazimu. Mwigulu aliwahi kuwaambia watu wanaolalamikia tozo, wahamie Burundi (hii ni kauli ya kiwendawazimu kwa kiongozi). Japipo naye alisema kuwa Magufuli asipotaka kuwa Rais kwa zaidi ya vipindi 2, watamkamata na kumlazimisha. Unapokuwa na viongozi wenye kauli za kiwendawazimu, wao wenyewe wanaonekana ni wendawazimu, lakini taswira yao hiyo huambukiza kwa Chama, Serikali na Rais.
Huwezi ukatetewa au kushangiliwa na jambazi, halafu watu wakakuthamini. Ukishangiliwa au kutetewa na jambazi, taswira inayopelekwa kwa watu ni kuwa na wewe ni jambazi.
Kwa upande mwingine, sura ya CCM na Serikali, inabebwa na aina ya viongozi waliopo (serikalini na kwenye CCM), watu wanaoitetea na kuisifia kwa kila jambo serikalini na kwenye CCM, kwenye mazingira yote (mitandaoni, bungeni, mitaani, n.k.). Sura ya CCM na Serikali inabebwa na vyombo kama Polisi na Tiss, ambavyo vimeamua kuilinda CCM na Serikali kwa nguvu zote zilizo halali na za kiharamia, badala ya kuilinda Jamhuri, ambalo lilistahili kuwa jukumu lao la msingi. Taswira ya vyombo hivi inaambukiza na kuwa taswira ya Serikali, CCM na Rais. Tutazame taswira za kila kimoja:
POLISI
Polisi ya Tanzania, taswira yake kwa umma, ni chombo cha kuwaonea wananchi (wanabambikia kesi watu - hata Rais amewahi kulisema hili). Ni chombo cha mauaji holela (Rais hivi karibuni amekemea uharamia unaofanywa na chombo hiki hadi kufikia kuua watuhumiwa kwenye mahabusu zao). Ni chombo cha utesaji (Zaidi ya 90% ya waliowahi kukaa kwenye mahabusu za polisi kwaajili ya upelelezi, watakuambia waliteswa sana, na wakati fulani watu hao hawakuwahi kuwa na hatia). Kwa hiyo watu wanawaona polisi ni kaka genge la majambazi lililopewa uhalali na Serikali na CCM. Kwa sababu haiba ya chombo hiki inaambukiza kwa mmiliki wake, taswira hii ya Polisi imeambukiza, na kuifanya CCM, Serikali na Rais, waonekane hivyo hivyo.
WATETEZI NA WAIMBA MAPAMBIO
Ukiwaangalia na kuwasikiliza wapambe wengi wa CCM ni watu wenye uelewa mdogo (CCM inapendwa zaidi na watu wajinga - taarifa ya TWAWEZA), wanafiki, wasaka fursa, wasio na upeo, na watu wanaofurahia mauaji, mateso na uonevu (mfano humu JF, mtazame Iboya, USSR, n.k.) dhidi ya watu wasio na hatia. Msikilize mtu kama Doto James, aliyedai kuwa walishindwa kumwua Lisu kwa risasi, safari hii watamwua kwa sindano. Kwa kauli hizi, CCM inaonekana ni chama cha wauaji. Na taswura hii inaambukiza kwa Serikali na Rais mwenyewe. CCM ya leo inajivunia uwezo wake wa kuua watu wasio na hatia ili tu kubakia madarakani.
VIONGOZI
Wasikilize baadhi ya viongozi wa CCM/serikali. Mtazame Mwigulu, Kibajaji, Musukuma, Japipo, n.k. Ni watu wenye upe mdogo, wanaoamini kuwa sifa ya kiongozi ni kuwa mbabe, mwongo, na wakati fulani uwa kama mwendawazimu. Mwigulu aliwahi kuwaambia watu wanaolalamikia tozo, wahamie Burundi (hii ni kauli ya kiwendawazimu kwa kiongozi). Japipo naye alisema kuwa Magufuli asipotaka kuwa Rais kwa zaidi ya vipindi 2, watamkamata na kumlazimisha. Unapokuwa na viongozi wenye kauli za kiwendawazimu, wao wenyewe wanaonekana ni wendawazimu, lakini taswira yao hiyo huambukiza kwa Chama, Serikali na Rais.
Huwezi ukatetewa au kushangiliwa na jambazi, halafu watu wakakuthamini. Ukishangiliwa au kutetewa na jambazi, taswira inayopelekwa kwa watu ni kuwa na wewe ni jambazi.